Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Wilaya ya Lushoto ina hospitali moja ya Wilaya ambayo inabeba mzigo mkubwa sana wa watu. Aidha, wodi ya wajawazito ni chumba kidogo sana na hakuna kabisa wodi ya mama na mtoto. Je, ni lini Serikali itajenga vyumba hivyo?

Supplementary Question 1

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri. Pia nashukuru kwa kuona hilo kwamba kweli Hospitali ya Wilaya ya Lushoto ina msongamano mkubwa sana.
Je, Serikali haioni sasa kuwa ipo haja ya kumalizia vituo vya afya vilivyoanza kujengwa kwa nguvu za wananchi ambavyo ni Ngwelo, Makanya ambayo ni zahanati inayotakiwa ipandishwe hadhi iwe kituo cha afya, pamoja na Gare ili kupunguza msongamano uliopo katika Hospitali ya Wilaya ya Lushoto?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa x-ray machine iliyopo katika Hospitali ya Wilaya ya Lushoto haina uwezo mkubwa wa kuhudumia watu wengi na hivyo kuzidiwa na kuharibika mara kwa mara na wagonjwa kukosa huduma hiyo muhimu; je, ni lini Serikali itapeleka x-ray machine ya kidijitali katika Hospitali ya Wilaya ya Lushoto na kupunguza usumbufu uliosababishwa na ubovu wa mashine hiyo? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Shekilindi katika swali lake la kwanza kuhusu kumalizia maboma kwenye vituo vya afya vitatu kikiwemo kimoja ambacho wanataka kukipandisha hadhi; nimwambie tu kwamba Serikali inaunga mkono. Mimi naomba sana katika fedha za ruzuku ambazo tutazipeleka hivi karibuni, Halmashauri iweke kipaumbele kikubwa kwenye hivyo vituo ambavyo Mheshimiwa Mbunge amevitaja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu x-ray, naomba tuendelee na mawasiliano, mwaka wa fedha mpya unaoanza ili angalau ifikapo mwezi wa kumi tuwe tumeshafanya maendeleo mazuri kwenye upande wa x-ray.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Wilaya ya Lushoto ina hospitali moja ya Wilaya ambayo inabeba mzigo mkubwa sana wa watu. Aidha, wodi ya wajawazito ni chumba kidogo sana na hakuna kabisa wodi ya mama na mtoto. Je, ni lini Serikali itajenga vyumba hivyo?

Supplementary Question 2

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, kutokana na swali namba 424.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wa ziara ya Mheshimiwa Waziri Mkuu alikuja Kijiji cha Chiwale na tulifanya pale uzinduzi wa jengo la mama na mtoto, lakini hata hivyo, Kituo cha Afya cha Chiwale tulipewa ahadi ya gari ambayo hatujajua itatekelezwa lini na sasa hivi kile kituo kimekuwa kikubwa na kinahudumia watu wengi sana wa kata zile kwa sababu Jimbo la Ndanda lina Kituo cha Afya kimoja tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nataka kufahamu kutoka kwa Mheshimiwa Waziri: Je, ni nini mpango wao wa kuweza kutusaidia pale kuweza kupata angalau mobile x- ray ili kuwasaidia watu wa jirani? Kwa sababu kwenye Kata zote 16 tuna kituo cha afya kimoja tu, kwa hiyo, ni safari ndefu sana kutoka Chiwale kwenda Masasi kwa ajili ya kwenda kupata huduma za afya kwenye Hospitali ya Wilaya ilipo sasa hivi na wenyewe x-ray yao ni mbovu. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mwambe amezungumza mambo mawili ndani ya swali moja; amezungumzia ahadi ya gari la wagonjwa; nimwambie kwamba tuendelee na mawasiliano ya karibu ili kusudi hiyo ahadi iweze kutekelezwa, kwa sababu nia ya Serikali ni kutekeleza ahadi zake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili hili la x-ray, na mimi nimwombe sana kwamba pamoja na kuweka kipaumbele cha Halmashauri kwenye bajeti zake kwa mwaka ujao wa fedha katika fedha za ruzuku ambazo mwaka ujao zitapatikana mapema zaidi, kama zisipotosha, basi naomba tuwe na mawasiliano ya karibu na ofisi yetu.

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Wilaya ya Lushoto ina hospitali moja ya Wilaya ambayo inabeba mzigo mkubwa sana wa watu. Aidha, wodi ya wajawazito ni chumba kidogo sana na hakuna kabisa wodi ya mama na mtoto. Je, ni lini Serikali itajenga vyumba hivyo?

Supplementary Question 3

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Lupembe, Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, lina vituo vya afya vinne na kati ya vituo hivyo tumeanza kutoa huduma ya theater kwenye kituo kimoja cha Lupembe kwa kupitia fedha za ndani lakini pia michango ya wananchi na Mbunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya kukamilisha majengo mengine kwenye kituo hiki na kituo kimojawapo ambacho tumeomba cha Kichiwa, kiweze kupata huduma ya theater na kukamilisha majengo yale ya Lupembe kwa kuwa tumeomba muda mrefu na hatujapata fedha yoyote? Tumekosa shilingi milioni 500, tumekosa shilingi milioni 400 na vituo vyote hivi havina hata gari la wagonjwa. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kukamilisha majengo, Serikali inatambua kwamba yapo majengo mengi sana ambayo yameanzishwa kwa nguvu za wananchi na vilevile kwa uwezo wa Halmashauri na bado hayajakamilika. Nazidi kutoa wito kwamba naomba sana Halmashauri zote nchini ziweke kipaumbele cha kwanza kabisa kumalizia majengo ambayo yameanzishwa. Pale ambapo fedha yoyote ya ruzuku au fedha ya ndani inapokuwa imepatikana, basi waweke kipaumbele sana kukamilisha majengo. Kuhusu gari la wagonjwa naomba tuendelee kuwasiliana na ofisi yetu ili tuweze kukamilisha kazi hiyo.

Name

Grace Sindato Kiwelu

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Wilaya ya Lushoto ina hospitali moja ya Wilaya ambayo inabeba mzigo mkubwa sana wa watu. Aidha, wodi ya wajawazito ni chumba kidogo sana na hakuna kabisa wodi ya mama na mtoto. Je, ni lini Serikali itajenga vyumba hivyo?

Supplementary Question 4

MHE. GRACE S. KIWELU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Hospitali ya Mkoa wa Kilimanjaro imekuwa kwenye ujenzi wa wodi ya wazazi zaidi ya miaka mitano sasa na wodi hiyo haijakamilika na kusababisha gharama za ujenzi kuongezeka. Je, ni lini Serikali itatoa pesa za kutosha kukamilisha wodi hiyo ya wazazi? Ahsante. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI na kwa niaba ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, napenda nitoe ahadi kwamba tutawasiliana ndani ya Serikali ili tuweze kutimiza matarajio ya Mheshimiwa Mbunge katika Hospitali ya Mkoa wa Kilimanjaro.