Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MHE. ALHAJ A. BULEMBO (K.n.y MHE. HUSSEIN N. AMAR) aliuliza:- Taasisi za umma na taasisi binafsi zimeitikia wito wa Mheshimiwa Rais wa kutengeneza madawati kwa ajili ya shule zetu nchini:- Je, Serikali na mamlaka husika zimejipanga vipi katika kuhakikisha utunzaji bora wa madawati hayo?

Supplementary Question 1

MHE. ALHAJ ABDALAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Swali la kwanza, kwa kuwa suala la madawati limekuwa ni tatizo la muda mrefu na historia iko wazi, kila mtoto akianza shule anaenda na madawati, madawati hayo huwa yanaenda wapi?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, Serikali ina mkakati gani wa kuweza kuyatunza yale madawati yanapokuwepo shuleni ili angalau na wengine wanaokuja waweze kuyakuta ili ugonjwa wa madawati uweze kuisha katika nchi hii?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA):
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Alhaj Abdalah Bulembo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, inashangaza kama yeye mwenyewe ambavyo ameonesha kushangaa kwamba shule inatengenezewa madawati ya kutosha halafu baada ya muda mfupi au baada ya muda baadhi ya madawati yanaonekana hayapo. Mimi nisisitize kwamba ni jukumu la msingi la Mkuu wa Shule au Mwalimu Mkuu kuhakikisha kwamba mali za shule zinatunzwa ipasavyo na tutalifuatilia hili. Kuanzia sasa hivi tunaiweka katika vigezo vya tathmini ya mwalimu kuhakikisha kwamba vifaa vya shule ikiwemo madawati vinatunzwa kikamilifu.
Mheshimiwa Spika, nadhani na swali lake la pili nakuwa nimeijibu kwa namna hiyo. Ahsante sana.

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALHAJ A. BULEMBO (K.n.y MHE. HUSSEIN N. AMAR) aliuliza:- Taasisi za umma na taasisi binafsi zimeitikia wito wa Mheshimiwa Rais wa kutengeneza madawati kwa ajili ya shule zetu nchini:- Je, Serikali na mamlaka husika zimejipanga vipi katika kuhakikisha utunzaji bora wa madawati hayo?

Supplementary Question 2

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Pamoja na jitihada nzuri za Serikali ikiwemo Bunge kuchangia utengenezaji wa madawati katika shule zetu za msingi na sekondari lakini madawati haya katika shule nyingi hayakuzingatia mahitaji ya kundi maalum, yaani watoto wenye ulemavu. Napenda tu kufahamu sasa ni mkakati gani unafanya ili tunapotengeneza au tunapofanya kitu chochote kuzingatia kundi hili maalum kwa sababu watoto wengine hawawezi kukaa hata kwenye hayo madawati ya jumla? Ahsante. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA):
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Amina Mollel, kwa kumwambia kwamba maoni aliyoyatoa tunachukua kuwa ni ushauri kwa Serikali kwa ajili ya kuufanyia kazi. Ahsante sana.