Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO) aliuliza:- Serikali imekuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha maendeleo ya michezo mbalimbali lakini sheria inayosimamia michezo ya mwaka 1967 ina upungufu makubwa sana. (a) Je, kwa nini Serikali haijatunga sheria mpya ya michezo ambayo itakwenda sambamba na mahitaji ya jamii kwa sasa? (b) Je, kwa nini Serikali haina bajeti kwa ajili ya Timu za Taifa zinazobeba bendera kwa ajili ya kuitangaza nchi Kimataifa?

Supplementary Question 1

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba niulize maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa utatuzi wa migogoro katika sekta ya michezo bado ni changamoto kubwa sana; je, Serikali haioni sasa kuna haja ya kuanzisha chombo ambacho kitakuwa chini ya BMT ili kuweza kusaidia kutatua migogoro badala ya kuacha watu wanaenda mpaka FIFA kwenda kufuata haki zao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. kwa kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inasisitiza suala la uimarishaji na ujenzi wa viwanda na michezo ni moja ya kiwanda kikubwa; je, Serikali sasa itakuwa tayari kuandaa kongamano la Waheshimiwa Wabunge wanamichezo na wadau ili kujitathmini tulikotoka, tulipo na tunakokwenda?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO:
Mheshimiwa Mwenyekiti, bado mpaka sasa sijaona kama utaratibu tuliouweka chini ya Baraza la Michezo Tanzania na chini ya Mashirikisho yanayohusika ya michezo kwamba umeshindikana kiasi cha kuunda chombo kingine kipya. Sisi kama Wizara tuko tayari kupokea maoni kutoka kwa wanamichezo kama Mheshimiwa Mwamoto, tuweze kuelewa umuhimu wa kuunda chombo kipya sasa hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kuhusu kuandaa kongamano, namwomba Mheshimiwa Mwamoto, yeye mwenyewe anaweza kuanzisha hilo, na sisi tutamuunga mkono kwa sababu suala la kongamano ni kujadiliana tuweze kusonga mbele katika michezo.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO) aliuliza:- Serikali imekuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha maendeleo ya michezo mbalimbali lakini sheria inayosimamia michezo ya mwaka 1967 ina upungufu makubwa sana. (a) Je, kwa nini Serikali haijatunga sheria mpya ya michezo ambayo itakwenda sambamba na mahitaji ya jamii kwa sasa? (b) Je, kwa nini Serikali haina bajeti kwa ajili ya Timu za Taifa zinazobeba bendera kwa ajili ya kuitangaza nchi Kimataifa?

Supplementary Question 2

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ligi yetu ya Tanzania imekuwa ikitumia gharama kubwa sana hata kwenye usajili wa zaidi ya shilingi bilioni moja kwenye timu kadhaa, lakini wanaenda kupokea shilingi milioni 86 na wamecheza kwa mwaka mzima.
Je, Serikali ina mkakati gani kuifanya ligi hii ya Tanzania kuwa ina ushindani? (Makofi)

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, sijui kama nimemwelewa vizuri Mheshimiwa Sima kuhusu usajili na ushindani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tu nimweleze Mheshimiwa Sima kwamba sisi kama Wizara bado hatujaona tatizo la usajili na ushindani katika ligi, lakini kama ni matumizi ya pesa, kwa kweli soka la leo ni la pesa. Usipokuwa na pesa, huwezi kabisa ukaendesha mchezo wowote wa mpira. Ndiyo maana unaweza kuona maendeleo mazuri ya timu kama Singida United, nao naomba niwapongeze kwa kazi nzuri ambayo wameifanya Kenya na tuwaombee kama ambavyo tunawaombea Simba waweze kufanya vizuri wawe washindi wa tatu katika mashindano ya Kenya.

Name

Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO) aliuliza:- Serikali imekuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha maendeleo ya michezo mbalimbali lakini sheria inayosimamia michezo ya mwaka 1967 ina upungufu makubwa sana. (a) Je, kwa nini Serikali haijatunga sheria mpya ya michezo ambayo itakwenda sambamba na mahitaji ya jamii kwa sasa? (b) Je, kwa nini Serikali haina bajeti kwa ajili ya Timu za Taifa zinazobeba bendera kwa ajili ya kuitangaza nchi Kimataifa?

Supplementary Question 3

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Michezo ni pamoja na viwanja. Naipongeza sana Serikali kwamba tuna uwanja mzuri sana, Uwanja wa Taifa, lakini uwanja ule kwenye eneo la VIP na juzi wananchi wote na Mheshimiwa Rais walikwenda pale kushuhudia mechi ya Simba na mechi ya Kagera. Eneo lile halina kibanda au kinga ya jua au mvua wakati hali ya hewa inabadilika.
Je, Serikali ina mpango gani sasa kuhakikisha kuwa eneo lile sasa linawekewa kibanda maalum kuzuia mvua kwa watazamaji wa kawaida na viongozi wa Kitaifa watakapokwenda kutazama mpira?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba kuna upungufu katika Uwanja wetu wa Taifa na ndiyo maana tulipokuja mbele ya Bunge lako tukufu kuomba tutengewe pesa kwa ajili ya ukarabati wa Uwanja wa Taifa, hiyo ni moja ya upungufu ambao utatatuliwa kwa pesa ambayo tumeiomba na ambayo inakidhi viwango vya CAF na FIFA.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata walipokuja juzi, tulipowaeleza kwamba matarajio yetu ni kutumia hiyo shilingi bilioni moja kwa ajili ya marekebisho ya aina hiyo katika Uwanja wa Taifa, walitukubalia. Kwa hiyo, mabadiliko kama hayo tuyategemee katika Uwanja wa Taifa katika muda sio mrefu kutoka sasa.

Name

Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO) aliuliza:- Serikali imekuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha maendeleo ya michezo mbalimbali lakini sheria inayosimamia michezo ya mwaka 1967 ina upungufu makubwa sana. (a) Je, kwa nini Serikali haijatunga sheria mpya ya michezo ambayo itakwenda sambamba na mahitaji ya jamii kwa sasa? (b) Je, kwa nini Serikali haina bajeti kwa ajili ya Timu za Taifa zinazobeba bendera kwa ajili ya kuitangaza nchi Kimataifa?

Supplementary Question 4

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Wizara na Baraza la Michezo zimekuwa zikiweka nguvu katika kuushughulikia mchezo mmoja tu wa mpira wa miguu na kusahau michezo mingine na ndiyo maana hata wakati uwanja mkubwa wa Taifa unajengwa, tuliambiwa kwamba inajengwa sports centre, lakini imejengwa football ground. Kwa maana hiyo, wenye michezo mingine wanashindwa kutumia miundombinu hiyo. (Makofi)
Je, Serikali itakuwa tayari sasa kutenga ukumbi mmoja kati ya kumbi zilizokuwa kwenye Uwanja wa Taifa kuwa Boxing Academy ili wacheza ngumi na wenyewe waweze kupata sehemu ya kufanya michezo?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna jumla ya michezo 38 iliyosajiliwa hapa nchini na tuna michezo mipya kabisa tisa ambayo mingine nikiitaja hapa wengine hatuwezi kuielewa. Kwa hiyo, kutokana na hiyo, sisi Kiwizara tunapanga mipango yetu kwa mahitaji na jinsi ambavyo michezo yenyewe inavyoendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, siyo kwamba kuna mchezo mwingine tunaupendelea, hapana, ni kutokana na wadau wenyewe.
Kwa mfano, leo hii hatuwezi tukasema tuweke katika mipango yetu namna ya kuendelea na mchezo wa freese B ambao ni mchezo wa kisahani umeingia nchi, kuna mchezo wa kabadi, kuna mchezo wa kengele (goal ball), kuna mchezo wa roll ball, kuna mchezo wa wood ball; sasa hiyo michezo tunawategemea wadau mwiendeleze ifikie kiwango ambacho tunasema tunaweza kuwa na ushindani katika nchi hii na tukaweza kuifanyia utaratibu kamili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wazo la Mheshimiwa Mtolea ni zuri kwamba tuna maeneo makubwa sana Uwanja wa Taifa, lakini pale penye mahitaji, wadau wenyewe waeleze na sisi tunaweza kutoa maeneo hayo kuweza kuyaendeleza kwa michezo mingine.