Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Serikali imekuwa na mpango kabambe wa kupeleka umeme vijijini:- Je, ni lini Serikali itawapelekea umeme wananchi wa Kata Itandula, Nyololo Shuleni, Maduma, Udumka, Kilolo, Kiyowole na Idete?

Supplementary Question 1

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali na nitoe pongezi kwa mkandarasi ambaye amepangwa kwenye Jimbo langu la Mufindi Kusini kwa kazi nzuri anayoifanya. Tulikuwa tuna tatizo la transfoma pale Ihowanza baada ya kumpa taarifa nimepata taarifa kwamba ameshaipeleka na pale Mbalamaziwa tulikuwa tuna tatizo la transfoma ameshaipeleka na sasa hivi mkandarasi yupo site. Kwa kazi hiyo nzuri, naipongeza sana Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na pongezi naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali langu la kwanza kuna vitongoji vingi sana kwenye Jimbo langu la Mufindi Kusini ambavyo havikufanyiwa survey na tulikuwa tumeandika hata majina tukapeleka pale TANESCO, je, vile vitongoji ambavyo vilikuwa vimerukwa mara ya kwanza na vyenyewe vitapewa umeme?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ningemuomba Waziri kama atapata nafasi kwa sababu kwenye Jimbo langu la Mufindi Kusini hawajaja, je, atakuja sasa kufanya mkutano akielezea vizuri matumizi haya ya umeme?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mendrad Lutengano Kigola, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tumepokea pongezi za Mheshimiwa Mbunge kwa namna ambavyo miradi ya REA III inavyoendelea katika Wilaya ya Mufindi hususani katika jimbo lake. Namshukuru kwa kulithibitishia Bunge lako kama mkandarasi yupo anaendelea vizuri na kweli mkandarasi Sengerema ni miongoni wa wakandarasi ambao wanafanya kazi zao vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia nimpongeze yeye mwenyewe Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia masuala ya nishati katika jimbo lake, anafanya kazi vizuri. Ndiyo maana katika maswali yake ya nyongeza amekiri kwamba kulikuwa na tatizo la transfoma kwenye kata alizozitaja na kutokana na maelekezo ya Mheshimiwa Waziri transfoma hizo zimeshafika katika maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake moja ameuliza ni lini vitongoji ambavyo havijafikiwa na umeme vitapata? Nataka nilitaarifu Bunge lako Tukufu na Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inaendelea kufanya upembuzi yakinifu kwenye Mradi wa densification II baada ya kufanikiwa kwa densification I, ambayo itahusisha mikoa 17 pamoja na Mkoa wa Iringa na katika vitongoji ambavyo vitasalia vitapatiwa umeme katika mradi wa ujazilizi awamu ya pili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusu kutembelea katika Jimbo lake la Mufindi Kusini na hususan Wilaya ya Mufindi, nataka nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba baada ya Bunge hili kwa kweli tutatembelea Mkoa wa Iringa kwa sababu mpaka sasa hivi tuna vijiji takribani 20 vinatakiwa kuwashwa umeme lakini pia kuna mradi ambao unaendelea wa BTIP ambao kwa kweli umefanya vizuri. Hivyo, nataka nilitaarifu Bunge ipo kazi ya kufanya katika huo Mkoa wa Iringa na Jimbo lake la Mufindi Kusini, kwa hiyo, tutakuja. Ahsante sana.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Serikali imekuwa na mpango kabambe wa kupeleka umeme vijijini:- Je, ni lini Serikali itawapelekea umeme wananchi wa Kata Itandula, Nyololo Shuleni, Maduma, Udumka, Kilolo, Kiyowole na Idete?

Supplementary Question 2

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nichukue nafasi hii nimpongeze Naibu Waziri pamoja na Waziri husika kwa kazi nzuri ambayo mnafanya ya kuhakikisha wananchi wanapata umeme. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri aliwahi kufika baadhi ya vijiji kikiwemo Kijiji cha Kihesa Mgagao na umeme tayari umeshafika. Naomba awaondoe wasiwasi wananchi wa sehemu umeme umefika hasa vitongoji kwamba umeme watapata au hawatapata?
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna Kata za Ukwega, Kising’a, Nyanzwa, Udekwa na Winome hawajapata umeme haujapimwa kabisa. Naomba niulize ni lini wataenda kupimiwa ili nao wawe na uhakika wa kuingia kwenye nchi mpya ya viwanda?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali. Kwa kweli mradi wa REA III unaendelea vizuri na umeshaanza katika mikoa yote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwamoto, napenda kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mwamoto anavyofuatilia masuala ya umeme katika Jimbo lake la Kilolo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nilifika katika Jimbo la Mheshimiwa Mwamoto na kijiji cha Nghuruwe pamoja na Kihesa Mgagao kulikuwa na changamoto kubwa sana. Kijiji cha Nghuruwe kilishapata umeme na sasa wanaendelea kupeleka umeme katika Kijiji cha Kihesa Mgagao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mwamoto kabla ya mwezi huu kuisha vitongoji vyote vya Kijiji cha Kihesa Mgagao vitakuwa vimeshawashwa umeme. Kadhalika bado vitongoji vyake saba katika maeneo ya karibu na Kihesa Mgagao, navyo tutavitembelea wiki ijayo namhakikishia kwamba na vyenyewe vitapata umeme kabla ya mwisho wa mwezi ujao. Nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)

Name

Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Serikali imekuwa na mpango kabambe wa kupeleka umeme vijijini:- Je, ni lini Serikali itawapelekea umeme wananchi wa Kata Itandula, Nyololo Shuleni, Maduma, Udumka, Kilolo, Kiyowole na Idete?

Supplementary Question 3

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na mimi kunipa nafasi hii niweze kuuliza swali moja tu la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya ya Chemba kwenye Kata za Kidoka, Jangalo na Msaada pamoja na maeneo ya vijiji vyake, kumekuwa na nyaya za umeme kwa muda mrefu lakini tatizo lililopo sasa ni kuwasha tu. Je, Serikali inanipa majibu gani ya uhakika kwamba ni lini maeneo haya yatapelekewa transfoma ili kuwasha umeme katika maeneo hayo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mheshimiwa Nkamia anavyofuatilia masuala ya umeme katika Jimbo lake la Chemba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpe taarifa Mheshimiwa Nkamia, nivyoongea hivi sasa transfoma tatu zinakwenda katika Kijiji cha Kidoka kwa ajili ya kuwasha umeme, lakini kesho pia wataendelea kupeleka nguzo pamoja na transfoma na nyaya katika Kijiji cha Msaada. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kijiji cha Jangalo, namwomba Mheshimiwa Mbunge tushirikiane baada ya vijiji hivi kuwashwa tutaendelea na Kijiji hicho. Wakati kazi hizo zinavyoendelea kule Kwa Mtoro nimhakikishie Mheshimwa Mbunge yapo magenge sita yanafanya kazi hivi sasa ili na yenyewe kabla ya mwisho wa mwezi wa kumi iweze kuwashiwa umeme. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Nkamia anavyoshirikiana na Serikali. Ahsante.