Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA (K.n.y. MHE. BONIPHACE M. GETERE) aliuliza:- Serikali imekuwa na mpango wa kufanya maboresho ya Vituo vya Afya nchini na Kituo cha Afya cha Ikizu ambacho kinahudumia kata zaidi ya 13, majengo yake licha ya kuwa hayatoshelezi hasa wodi ya akina mama wajawazito na watoto, lakini pia yamechakaa sana. Je, Serikali inatoa tamko gani kuhusu maboresho ya kituo hicho?

Supplementary Question 1

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali juu ya kituo hiki. Nina maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa kituo hiki kilijengwa siku nyingi tangu 1970; na kwa kuwa majengo mengi yamechakaa; na hivi karibuni, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano alipopita katika eneo hilo aliwaahidi Wanabunda wa kituo hiki kwamba kituo hiki kitakarabatiwa haraka; ni lini Serikali itakarabati kituo hiki ili kiweze kuwahudumia wananchi wa Bunda?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa Makambako tuna kituo cha afya ambacho kinahudumia wananchi wa Mji wa Makambako; na kwa kuwa mwaka 2017 Serikali ilitupa fedha kwa ajili ya kununua vifaa tiba, hasa vya upasuaji na kwa sababu sasa hivi kituo hakina x-ray, ultrasound na vifaa tiba. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha ambazo iliahidi shilingi milioni 500, kwa ajili ya kununua vifaatiba na hela za kujengea wodi ili wananchi hawa wasipate adha ya kwenda kupimwa sehemu nyingine?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya cha Ikizu ni miongoni mwa vituo bora kabisa katika Wilaya ya Bunda ambayo kinatoa huduma ya upasuaji. Pale wana mpaka ambulance na mortuary ya kisasa kabisa. Lakini pia naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba azma ya Serikali ya kukarabati vituo vyetu vya afya vilivyochakaa bado iko pale pale. Kutegemeana na upatikanaji wa fedha, tutaendelea kufanya ukarabati na maboresho.
Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili Mheshimiwa Sanga anataka kujua lini vifaa kama x-ray pamoja na ultrasound vitapelekwa katika kituo chake cha afya cha Makambako? Naomba nimhakikishie kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI imepeleka fedha MSD kwa ajili ya kununulia x-ray pamoja na ultrasound. Ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba vituo vyote vya afya vinavyokarabatiwa vinatoa huduma ya upasuaji pamoja na vipimo kwa kutumia x-ray. Kwa hiyo, nawataka wananchi wa Makambako wahakikishe katika ujenzi unaofanyika, pia na jengo la x-ray liwepo. (Makofi)

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA (K.n.y. MHE. BONIPHACE M. GETERE) aliuliza:- Serikali imekuwa na mpango wa kufanya maboresho ya Vituo vya Afya nchini na Kituo cha Afya cha Ikizu ambacho kinahudumia kata zaidi ya 13, majengo yake licha ya kuwa hayatoshelezi hasa wodi ya akina mama wajawazito na watoto, lakini pia yamechakaa sana. Je, Serikali inatoa tamko gani kuhusu maboresho ya kituo hicho?

Supplementary Question 2

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi hii.
Kwanza kabisa naipongeza Serikali kwa kutupatia shilingi milioni 800 ambazo maboresho makubwa ya Hospitali ya Wilaya ya Nzega yanaendelea. Sasa nataka kuuliza kwamba Serikali mna mpango gani na Vituo vya Afya vya Itobo na Bukene ambavyo vina tatizo kubwa sana la wodi. Je, baada ya kumaliza maboresho ya Hospitali ya Wilaya, mtakuwa tayari sasa kuelekeza nguvu kwenye Vituo vya Afya vya Itobo na Bukene?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, kimsingi tutakuwa tayari kama ambavyo tumekuwa tayari siku zote. Hatua kwa hatua tukimaliza vituo hivi ambavyo tumeanza navyo tutakwenda na Vituo vingine vya Afya.

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA (K.n.y. MHE. BONIPHACE M. GETERE) aliuliza:- Serikali imekuwa na mpango wa kufanya maboresho ya Vituo vya Afya nchini na Kituo cha Afya cha Ikizu ambacho kinahudumia kata zaidi ya 13, majengo yake licha ya kuwa hayatoshelezi hasa wodi ya akina mama wajawazito na watoto, lakini pia yamechakaa sana. Je, Serikali inatoa tamko gani kuhusu maboresho ya kituo hicho?

Supplementary Question 3

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Mpanda Town Clinic ni kituo ambacho kinaisaidia sana Hospitali ya Manispaa ya Mpanda, lakini kwa bahati mbaya kituo hiki ilikuwa kikarabatiwe kwa kupitia fedha za ruzuku kwa maana ya miradi viporo. Naomba kuiuliza Serikali, ni lini watatusaidia fedha hiyo ili tuweze kukisaidia kituo hiki? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, nilipata bahati ya kutembelea Mkoa wa Katavi na Manispaa ya Mpanda nimeitembelea. Pale jirani na stand, kuna ujenzi wa Kituo kipya cha Afya, lengo ni kuhakikisha kwamba msongamano katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda unapungua.
Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Kapufi, naye ni shuhuda, tulikuwa wote pamoja; ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba huduma ya afya inasogezwa kwa wananchi.