Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Halmashauri ya Mji wa Tarime imebahatika kuwa na Uwanja wa Ndege wa Magena ambao umekuwa ukitumiwa na watalii wanaokwenda Mbuga ya Serengeti, viongozi mbalimbali na hata Mgodi wa Acacia. Miundombinu ya uwanja pamoja na barabara zake ni mbovu sana. (a) Je, ni lini Serikali itapanua uwanja huu na kurekebisha miundombinu yake ili ndege nyingi ziweze kutua kwa ajili ya watalii waendao Serengeti? (b) Je, ni kwa nini Serikali haijajenga jengo la Uhamiaji katika uwanja huo ili kutoa urahisi wa watalii wanaotumia uwanja huo?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Hili swali la kuuliza kuhusu uwanja wa ndege na kuiomba Serikali ione umuhimu wa kuupandisha hadhi huu uwanja utoke kwenye Halmashauri na uende kwenye Tanzania Aviation Authority; kwa sababu kwa sasa hivi ilivyo kumkodisha Coastal Aviation kwa milioni 20 kwa mwaka anakuwa ana-monopolize na kodi ambazo anawataja aviation zingine wanavokuja kutoa pale ni nyingi sana; kwa hiyo Serikali tunapoteza mapato mengi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali, ni kwa nini sasa Serikali haioni umuhimu wa kupandisha hadhi huu uwanja na kuukarabati kwa sababu tunapata watalii kutoka maeneo mbalimbali, lakini pia unaweza kutumika kwa ndege kutoka pale kwenda hata nchi jirani ya Kenya? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili ni kwa nini sasa wameeleza hapa kwamba wamekarabati barabara ya kilometa 1.2, lakini kuna barabara ya kutoka Tarime kupita Magena unaenda mpaka Kata ya Mwema kule ambapo kuna daraja la Mto Moli ni bovu sana hata Clouds Tv walionesha…..
…linahatarisha maisha watu wanaotumia ile barabara. Ni lini sasa Serikali itaweza kujenga daraja lile la Mtomoli sambamba na ile barabara ambayo inaenda Magena kwenye huu uwanja?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, dhana ya kuomba kupandishwa uwanja huu kuchukuliwa na iwe miongoni mwa viwanja ambavyo vinamilikiwa kitaifa haina ubaya. Hata hivyo ni vizuri tukajua chimbuko la uwanja huu. Uwanja huu mwanzo ulikuwa unatumiwa na kampuni hii ambayo inajiita COGFA ambao wanajenga barabara ya kutoka Sirari kwenda Makutano. Na wao baada ya kumaliza matumizi yake walimkabidhi Mkuu wa Wilaya, lakini baadae bali katika kugawanyika Halmashauri ya Mji na halmashauri ya Tarime Town Council na DC ikaonekana kwamba uwanja ule ambao uko kilometa tisa ubaki chini ya umiliki. Ukitazama katika mkataba wao ambao ni suala la wao ndani ya Halmashauri, kwa sababu mkataba umeingiwa kati ya Coastal Aviation na Halmashauri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo linaongeleka, kwa kadri watakavyopisha kwenye vikao vyao na wakaridhia kwamba sasa ownership ihame sisi kama Serikali hatuna ubishi na hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, juu ya swali la pili la kujenga daraja, kama ambavo tumekuwa tukitengeneza miundombinu kwa kadri bajeti inavyoruhusu, naomba nimehakikishie Mbunge bajeti ikiruhusu tuna kila sababu ya kuhakikisha kwamba mazingira rafiki kwa ajili ya watalii kwenda mbuga yanajenga, ni pamoja na kujenga kwa daraja.

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Halmashauri ya Mji wa Tarime imebahatika kuwa na Uwanja wa Ndege wa Magena ambao umekuwa ukitumiwa na watalii wanaokwenda Mbuga ya Serengeti, viongozi mbalimbali na hata Mgodi wa Acacia. Miundombinu ya uwanja pamoja na barabara zake ni mbovu sana. (a) Je, ni lini Serikali itapanua uwanja huu na kurekebisha miundombinu yake ili ndege nyingi ziweze kutua kwa ajili ya watalii waendao Serengeti? (b) Je, ni kwa nini Serikali haijajenga jengo la Uhamiaji katika uwanja huo ili kutoa urahisi wa watalii wanaotumia uwanja huo?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Tatizo la uwanja ambalo limeongelewa na Mheshimiwa Matiko ni sawa sawa kabisa na tatizo la Uwanja wa Ndege wa Songea, uwanja ambao unahudumia Mkoa wa Ruvuma na Mkoa wa Njombe. Tangu mwezi wa tatu mwaka huu uwanja huo umefungwa na hautumiki tena. Jitihada za Serikali kuleta ndege hazisaidii kwa sababu ndege haziwezi kutua katika uwanja huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu ni, je, ni lini uwanja huo utafanyiwa ukarabati na kuanza kutumika ili kuwanufaisha wananchi wa Mkoa wa Ruvuma na Mkoa wa Njombe?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua umuhimu wa huduma hii ya usafiri wa ndege katika Mkoa wa Ruvuma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niliarifu tu Bunge kwamba tulishapata mkandarasi wa kufanya ukarabati wa uwanja huu; taratibu za manunuzi zilikuwa zinakamilishwa ili ujenzi kwa haraka ufanyike. Sambamba na ukarabati wa uwanja huu wa Songea tutafanya pia uwanja wa ndege wa Iringa ili lengo sasa la kuweza kufanya haya mashirika ya ndege yaweze kujiendesha kwa faida kwa maana ya viwanja vyote vitatu cha Mtwara, Ruvuma pamoja na Iringa kwa pamoja tukikarabati tutafanya na wao waweze kufanya kazi kwa tija.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo Mheshimiwa vuta subira, tuko tayari kufanya matengezo kwenye uwanja huo. (Makofi)

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Halmashauri ya Mji wa Tarime imebahatika kuwa na Uwanja wa Ndege wa Magena ambao umekuwa ukitumiwa na watalii wanaokwenda Mbuga ya Serengeti, viongozi mbalimbali na hata Mgodi wa Acacia. Miundombinu ya uwanja pamoja na barabara zake ni mbovu sana. (a) Je, ni lini Serikali itapanua uwanja huu na kurekebisha miundombinu yake ili ndege nyingi ziweze kutua kwa ajili ya watalii waendao Serengeti? (b) Je, ni kwa nini Serikali haijajenga jengo la Uhamiaji katika uwanja huo ili kutoa urahisi wa watalii wanaotumia uwanja huo?

Supplementary Question 3

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilifanya upanuzi wa uwanja wa ndege wa Dodoma na wananchi ambao wanaishi karibu na uwanja ule nyumba zao ziliwekwa alama ya “X” kwa maana kwamba zile nyumba zitavunjwa kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege. Hata hivyo baadhi ya wananchi wamelipwa na baadhi ya wananchi hawalipwa fidia kutokana na nyumba zao kuwekwa alama “X”. Naomba kujua ni lini wananchi ambao hawalipwa watalipwa fidia ili waende wakayafanye maendele ya ujenzi wa nyumba kwenye maeneo mengine?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI, UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tu nimtaharifu Mheshimiwa Mbunge kwamba kuanzia kesho hao wananchi ambao wanadai fidia zao wataanza kulipwa kupitia Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, ahsante.

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Halmashauri ya Mji wa Tarime imebahatika kuwa na Uwanja wa Ndege wa Magena ambao umekuwa ukitumiwa na watalii wanaokwenda Mbuga ya Serengeti, viongozi mbalimbali na hata Mgodi wa Acacia. Miundombinu ya uwanja pamoja na barabara zake ni mbovu sana. (a) Je, ni lini Serikali itapanua uwanja huu na kurekebisha miundombinu yake ili ndege nyingi ziweze kutua kwa ajili ya watalii waendao Serengeti? (b) Je, ni kwa nini Serikali haijajenga jengo la Uhamiaji katika uwanja huo ili kutoa urahisi wa watalii wanaotumia uwanja huo?

Supplementary Question 4

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mji wa Njombe una uwanja wa ndege lakini wa nyasi; lakini katika ule uwanja kuna wananchi wana nyumba pembezoni mwa ule uwanja. Hakuna mipaka ya uwanja na hawaruhusiwi kuendeleza maeneo yao. Je ni lini Serikali itaenda kufanya utambuzi na kuwalipa fidia wale wananchi ili wapishe ule uwanja?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwalongo jirani yangu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunatambua changamoto zilizokuwepo kwenye Uwanja wa Ndege wa Njombe na hata hivi karibuni Mheshimiwa wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano amefika Njombe kwa ajili ya kuona namna bora ya kuweza kukamilisha na kuweka mipaka katika eneo hili. Kilichokuwa kimetuchelewesha ilikuwa pia ni wazo la Mkoa kuweza kuomba kuhamisha uwanja katika eneo hili. Hata hivyo baada ya mazungumzo nafikiri sasa tuko tayari kuweka mipaka hiyo ili na ukarabati wa uwanja huu kati ya viwanja 11 uweze kufanyika.