Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Hivi karibuni Serikali kupitia JKT imeanzisha tena mafunzo ya vijana wa kujitolea na wale wa mujibu wa sheria waliomaliza kidato cha sita au kutoka vyuo hapa nchini. • Je, ni kweli kuwa JKT wanachukua wanafunzi kwa mujibu wa sheria kutoka katika shule na vyuo vya Serikali tu? • Je, Serikali haioni kuwa vijana kutoka shule na vyuo binafsi wanahitaji pia mafunzo muhimu ya uzalendo na kujiendeleza kiuchumi? • Je, ni vijana wangapi kwa mujibu wa sheria kwa mwaka 2017/2018 wamechukuliwa na JKT katika shule na vyuo binafsi nchini?

Supplementary Question 1

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri sana leo ya Waziri wa Ulinzi ndugu yangu Mheshimiwa Mwinyi nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa vile idadi inayochukuliwa kwa mwaka ni ndogo sana ukilinganisha na idadi ya wanafunzi wanaomaliza shule form six na vyuo. Je, Serikali haioni umuhimu wa kupanua kiasi idadi ya wanafunzi hawa ili wapate mafunzo ambayo tunafikiri kwamba ni ya maadili na uzalendo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa vile vijana wengi wanaotoka baada ya mafunzo kutoka JKT husahau au kuacha mafunzo mazuri na maadili waliyofundishwa kule JKT. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwafuatilia vijana hawa ili wasisahau mafunzo na kuacha maadili mazuri ya wananchi?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Almas Maige kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu idadi ndogo ya vijana tunaowachukua kwa mujibu wa sheria, ni kweli kwamba wahitimu sasa hivi wanazidi 60,000, lakini uwezo wetu wa kuchukua inakadiriwa kuwa ni kama 20,000 peke yake. Kwa hiyo iko mikakati ya kuhakikisha kwamba tunaongeza idadi ya vijana wanaochukuliwa kwenda JKT kwa kuboresha miundombinu katika kambi tulizonazo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaendelea kuziboresha ili ziweze kuchukua vijana wengi zaidi na ni matumaini yetu kwamba kila mwaka tutaendelea kuongeza idadi. Hata hivyo, hivi karibuni tu tumefungua kambi mpya tano katika Mikoa ya Rukwa kule Milimbikwa na Ruwa, Mpwapwa Dodoma, Makuyuni Arusha, Itaka pamoja na Kibiti. Kwa hivyo ni mategemeo yetu kwamba, kwa kuongeza kambi hizi mpya idadi ya vijana tunaoendelea kuwachukua itaongezeka ili hatimaye wote wanaomaliza form six waweze kujiunga kwanza na JKT kabla hawajaanza vyuo vikuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali la pili la kufuatilia vijana ili wasisahau maadili nadhani hili ni wazo zuri. Mpaka sasa hivi hakuna mkakati wa kuwarudisha tena lakini tunalipokea tutaangalia njia bora zaidi ya kulifuatilia.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Hivi karibuni Serikali kupitia JKT imeanzisha tena mafunzo ya vijana wa kujitolea na wale wa mujibu wa sheria waliomaliza kidato cha sita au kutoka vyuo hapa nchini. • Je, ni kweli kuwa JKT wanachukua wanafunzi kwa mujibu wa sheria kutoka katika shule na vyuo vya Serikali tu? • Je, Serikali haioni kuwa vijana kutoka shule na vyuo binafsi wanahitaji pia mafunzo muhimu ya uzalendo na kujiendeleza kiuchumi? • Je, ni vijana wangapi kwa mujibu wa sheria kwa mwaka 2017/2018 wamechukuliwa na JKT katika shule na vyuo binafsi nchini?

Supplementary Question 2

MHE. SUSAN A. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Majibu ya Mheshimiwa Waziri yamekuwa ni hayo hayo kwa muda mrefu, na maswali yalikuwa ni kwa nini sasa wanafunzi wote wanaomaliza kidato cha sita wasiende JKT kwa sababu lengo la JKT kama ulivyosema mwenyewe ni suala la uzalendo na maadili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kila leo wanasema wanaboresha, wanaongeza lakini sisi tunachotaka ni kwamba wote Watanzania vijana hawa tunataka wote wawe in uniform waweze kutekeleza suala zima la uzalendo na maadili ili nchi yetu maadili yasiendelee kuporomoka, sasa ni lini watahakikisha hilo linafanyika?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema jitihada zimefanyika na zimeonekana. Wakati tunarudisha tena utaratibu wa JKT baada ya kuwa tumeuacha kwa miaka mingi kuanzia mwaka 1994, idadi tuliyokuwa tunaweza kuchukua ilikuwa ndogo sana si zaidi ya vijana 5000; leo tunavyozungumza tayari tumefikia 20,000 na kambi mpya nimezitaja tunazozifungua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo si maneno tu ya kurudia hii ni mkakati uliopo. Kila mwaka tunaendelea kufungua kambi mpya tunaboresha za zamani na idadi imeendelea kuongezeka. Leo tunavyozungumza kama tunachukua vijana 20,000, bila shaka ndani ya miaka michache ijayo tutaweza kukidhi mahitaji ya vijana 60,000 au 80,000 ambao watakuwa wanahitimu.

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Hivi karibuni Serikali kupitia JKT imeanzisha tena mafunzo ya vijana wa kujitolea na wale wa mujibu wa sheria waliomaliza kidato cha sita au kutoka vyuo hapa nchini. • Je, ni kweli kuwa JKT wanachukua wanafunzi kwa mujibu wa sheria kutoka katika shule na vyuo vya Serikali tu? • Je, Serikali haioni kuwa vijana kutoka shule na vyuo binafsi wanahitaji pia mafunzo muhimu ya uzalendo na kujiendeleza kiuchumi? • Je, ni vijana wangapi kwa mujibu wa sheria kwa mwaka 2017/2018 wamechukuliwa na JKT katika shule na vyuo binafsi nchini?

Supplementary Question 3

MHE. MASOUD ABDALLA SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nina swali moja dogo la nyongeza. Kuna malalamiko kadhaa kwa vijana wale ambao walioajiriwa kwenye Shirika la Uzalishaji Mali la SUMA JKT, kiwango chao cha fedha ni kidogo sana na vijana hawa wanalinda katika maeneo kadhaa na maeneo muhimu kama vile benki. Ni mara kadhaa wamekuwa wakisema kwamba mtapandisha kiwango cha posho cha vijana hawa wa SUMA JKT Guard, ni kwa nini basi Serikali imekuwa ikisuasua kwa muda mrefu hawapandishi pesa hizi na ni vijana hwa wanafanya kazi kubwa?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Masoud kuhusu vijana wanaofanya kazi kwenye Shirika la SUMA Guard. Ni kweli malalamiko hayo na sisi tumeyapata, tumezungumza na Uongozi wa SUMA Guard ili waweze kuongeza viwango ambavyo wanawapatia vijana hawa. Hivi sasa tunavyozungumza ukiacha mshahara ile basic salary, kuna posho wanazopata za usafiri, za chakula na kadhalika; lakini bado tunakiri kwamba viwango wanavyopewa havikidhi haja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutaendelea kujitahidi kufanya kila linalowezekana ili maslahi kwa ujumla ya vijana hawa yaweze kuboreka. Kwa ujumla ni kwamba viwango vinavyofuatwa vinaendana na mashirika mengine ya ulinzi. Kwa hivyo ni vyema sisi kama Serikali tuone umuhimu wa kuboresha haya. Jambo hilo limechukuliwa na Uongozi wa SUMA JKT na ni mategemeo yetu kwamba wataweza kuwaboreshea viwango hivyo.