Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE aliuliza:- Hospitali ya Mtakatifu Gaspar imekuwa Hospitali ya Rufaa tangu mwaka 2011 na inahudumia wananchi wa Mikoa ya Tabora, Singida na Mbeya. Wakati wa kampeni mwaka 2015, Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli aliahidi kuipatia vifaa tiba, dawa na watumishi wa kutosha ili kupunguza changamoto wanazokutana nazo wagonjwa:- Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais itatekelezwa ili kusaidia hospitali hiyo kutoa huduma za afya kwa ufanisi na kuokoa maisha ya wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa hospitali hii inahudumia wagonjwa wengi kutoka Mkoa wa Mbeya, Singida na Tabora lakini ina Madaktari Bingwa wachache; Madaktari Bingwa waliopo ni wanne tu. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha hospitali hii inakuwa na Madaktari Bingwa wa kutosha ili kutoa huduma bora kwa wakati wote?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa gharama za hospitali hii ya Mission pamoja na gharama nyingine za hospitali za binafsi ni kubwa sana ambapo wananchi wa kawaida hawawezi kumudu. Kwa mfano, mama anapoenda kujifungua anatakiwa kulipa Sh.150,000 kwa kawaida lakini anapojifungua kwa operesheni anatakiwa kulipa Sh.450,000. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Wilaya ya Itigi inapata Hospitali ya Wilaya? Mheshimiwa Spika, nakushukuru. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, kuhusiana na suala zima la kuwepo Madaktari Bingwa wa kutosha, ni nia ya Serikali kuhakikisha kwamba wanapatikana ili waweze kutoa huduma. Hivi karibuni Ofisi ya Rais, TAMISEMI imeweza kutoa tangazo kwa ajili ya Madaktari. Naamini katika wale ambao watakuwa wameomba na Madaktari Bingwa watapatikana kwa ajili ya kuwapeleka maeneo kama hayo.
Mheshimiwa Spika, naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira na swali hili limekuwa likiulizwa mara kwa mara na Wabunge wa Mkoa wa Singida, mnamo tarehe 7 mwezi huu swali hili liliulizwa na leo linaulizwa kwa mara ya pili. Kwa hiyo, inaonyesha jinsi ambavyo wanajali wananchi wao katika suala zima la afya.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na gharama za matibabu ambazo zinatolewa na hospitali hii na hospitali zingine binafsi, kama ambavyo nimejibu katika jibu langu la msingi tunatarajia mwongozo kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa sababu Serikali inawekeza pesa zake, kuwe na bei ambazo wananchi wanaweza kumudu.
Mheshimiwa Spika, amechomekea na swali lingine kuhusiana na ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Itigi, naomba nimhakikishie ni azma ya Serikali baada ya kuwa tumemaliza hizi hospitali 67, katika maeneo yote ambayo hakuna Hospitali za Wilaya Serikali itaenda kujenga.

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE aliuliza:- Hospitali ya Mtakatifu Gaspar imekuwa Hospitali ya Rufaa tangu mwaka 2011 na inahudumia wananchi wa Mikoa ya Tabora, Singida na Mbeya. Wakati wa kampeni mwaka 2015, Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli aliahidi kuipatia vifaa tiba, dawa na watumishi wa kutosha ili kupunguza changamoto wanazokutana nazo wagonjwa:- Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais itatekelezwa ili kusaidia hospitali hiyo kutoa huduma za afya kwa ufanisi na kuokoa maisha ya wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, nakubali kwamba Serikali inajitahidi sana kusaidia Hospitali ya Wilaya ya Urambo lakini bado tuna changamoto kubwa ambayo ni ukosefu wa theater, ni mradi wa ADB ambao ulijenga theater pale ikafikia lenta. Je, Serikali inawaliwaza vipi wapiga kura wangu wa Urambo kuhusu kumalizika kwa theatre ambayo ipo katika hatua ya lenta?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, nilipata nafasi ya kutembelea Urambo na naomba nimpongeze kwa dhati kabisa Mheshimiwa Sitta amekuwa ni mpiganaji kuhakikisha kwamba afya ya akinamama na watoto kwa ujumla inaboreshwa. Wakafanya kazi nzuri sana, wameanzisha na wodi maalum kwa wale watu ambao wangependa wawe kwenye grade A, ni jambo la kupongezwa na wengine ni vizuri tukaiga. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, nimeona ile theater ambayo inajengwa ikafikia usawa wa lenta, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Sitta Serikali itahakikisha kwamba kazi nzuri ambayo imefanyika haiachwi ikapotea, kwa kadri pesa itakavyopatikana tuna wajibu wa kuhakikisha kwamba tunamalizia ile theater ambayo ilikuwa imekusudiwa kwa ajili ya kutoa huduma kwa akinamama na watoto. (Makofi)

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE aliuliza:- Hospitali ya Mtakatifu Gaspar imekuwa Hospitali ya Rufaa tangu mwaka 2011 na inahudumia wananchi wa Mikoa ya Tabora, Singida na Mbeya. Wakati wa kampeni mwaka 2015, Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli aliahidi kuipatia vifaa tiba, dawa na watumishi wa kutosha ili kupunguza changamoto wanazokutana nazo wagonjwa:- Je, ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais itatekelezwa ili kusaidia hospitali hiyo kutoa huduma za afya kwa ufanisi na kuokoa maisha ya wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana na mimi kupata swali la nyongeza. Ni wiki mbili zimepita alikuja Katibu wa Hospitali ya Mwambani Bwana Kalindu na nikamwita Mheshimiwa Naibu Waziri tukakaa, tukaongelea habari ya Hospitali ya Mwambani pale Mkwajuni.
Mheshimiwa Spika, kama mnavyojua Songwe ni Wilaya mpya na hatuna Hospitali ya Wilaya lakini hii Hospitali ya Mwambani ndiyo inayotumika kama Hospitali ya Wilaya au Hospitali Teule, lakini watumishi mpaka sasa ni haba na hatupati dawa na hata mgao wa Serikali hauendi kama ambavyo inatakiwa ipewe Hospitali Teule. Ni nini Serikali inatamka juu ya jambo hili na Mheshimiwa Waziri anajua?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli Mheshimiwa Mulugo alikuja na tukakaa pamoja na Daktari ambaye alikuwa ametoka Hospitali ya Mwambani. Kimsingi Hospitali ya Mwambani kwa sababu ndiyo hospitali pekee iliyopo inatakiwa itumike kama DDH. Ni makosa tu ambayo yalifanyika na naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ndani ya muda mfupi tatizo litakuwa limeshatatuliwa na hospitali ile itatambuliwa kama DDH kwa sababu ndiyo hospitali ambayo ni tegemeo kwa wananchi wa Mwambani na Chunya kwa ujumla wake. (Makofi)