Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:- Tatizo la wahamiaji haramu hasa kutoka Ethiopia limeshamiri sana katika nchi yetu kwa sasa:- (a) Je, ni wahamiaji haramu wangapi wamekamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria? (b) Kama wapo ambao wanaendelea na kifungo, je, ni hatua gani za kisheria ambazo zinachukuliwa baada ya kutolewa kifungoni?

Supplementary Question 1

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ambayo yametoa mwangaza kwa Watanzania, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa wahamiaji haramu wanapoingia nchini bila kutambuliwa kisheria baadhi yao huzaa watoto hapa nchini. Je, hawa watoto wanakuwa raia wa nchi gani? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa wale Watanzania ambao wanawakaribisha wahamiaji haramu hapa nchi na wanajua kisheria siyo utaratibu, je, Serikali inachukua hatua gani kwa raia hao? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Fakharia Shomar, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa suala la watoto wa wahamiaji haramu na wenyewe pia itakuwa ukaazi wao nchini ni kinyume na sheria za nchi yetu. Kama ambavyo tunafahamu kwa mujibu wa Sheria ya Uhamiaji mtu anaweza kuwa raia wa nchi ikiwa angalau mmoja wa wazazi wake wakati anazaliwa alikuwa raia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusiana na suala la raia ambao wamekuwa wakihifadhi wahamiaji haramu, kwanza tunataka kutoa wito kwa wananchi wenye tabia hizo kuacha mara moja kwani kufanya hivyo ni kinyumbe na sheria za nchi lakini vilevile adhabu yake ni kali sana. Moja katika jitihada ambazo tunazifanya kukomesha au kutokomeza kabisa hii biashara ya uhamiaji haramu ni kushughulika na mitandao ya wale ambao wanajihusisha na biashara hii ikiwemo wanaosafirisha, wanao-organize pamoja na wanaohifadhi. Kwa hiyo, wote hawa tukiwakamata tutawachukulia hatua za kali kabisa kwa mujibu wa sheria za nchi yetu.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:- Tatizo la wahamiaji haramu hasa kutoka Ethiopia limeshamiri sana katika nchi yetu kwa sasa:- (a) Je, ni wahamiaji haramu wangapi wamekamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria? (b) Kama wapo ambao wanaendelea na kifungo, je, ni hatua gani za kisheria ambazo zinachukuliwa baada ya kutolewa kifungoni?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa tatizo la wahamiaji haramu kutoka Ethiopia linaongezeka, je, Serikali haioni imefikia wakati wa kulizungumza suala hili kidiplomasia kati ya Tanzania na Ethiopia ili kuweka utaratibu maalum kuepuka kuwaweka magerezani ambapo huligharimu Taifa? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu sahihi aliyoyatoa tangu mwanzo na niwapongeze Waheshimiwa Wabunge kwa kulileta swali hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Ijumaa na Jumamosi tulikuwa na vikao vya Jumuiya ya Afrika Mashariki vinavyoshughulikia masuala ya kiusalama ya kisekta na kwenye maazimio tuliyoyapitisha ni pamoja jambo hili kuwa jambo la mipaka yote ya Jumuiya ya Afrika Mashariki tofauti na ilivyo sasa ambako nchi zingine zote za Jumuiya ya Afrika Mashariki ikiwepo Kenya wanapopitia zaidi kwao wao hili jambo halikuwa kama tatizo walikuwa wanapita tu kama mtembeaji mwingine yeyote aliyeko ndani ya nchi husika. Kwa hiyo, kwa sasa tumesema hili ni jambo ambalo tutalioanisha na mambo mengine ambayo yanazuiwa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ili hawa watu waweze kuanza kuzuiwa kwenye mipaka ya Kenya na Sudan Kusini tofauti na ilivyo sasa ambapo huwa wanapata kipingamizi wanapofika Tanzania na nchi zingine zote wanakuwa wameshapita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, tunalipokea na hilo jambo ambalo amelisemea la kuongea nanchi husika ambao wahamiaji hawa wanatoka ambapo ni Ethiopia, Eritrea pamoja na Somalia. Hiyo tutaifanya kwa kuanzia na Balozi zao zilizopo hapa ili jambo hilo liweze kuongewa pia katika nchi zao.

Name

Rev. Peter Simon Msigwa

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:- Tatizo la wahamiaji haramu hasa kutoka Ethiopia limeshamiri sana katika nchi yetu kwa sasa:- (a) Je, ni wahamiaji haramu wangapi wamekamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria? (b) Kama wapo ambao wanaendelea na kifungo, je, ni hatua gani za kisheria ambazo zinachukuliwa baada ya kutolewa kifungoni?

Supplementary Question 3

MHE. MCH. PETER S. MSIGWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru. Tatizo la wahamiaji haramu ni kubwa sana katika magereza nyingi za nchi hii na wengine wako under age. Tatizo kubwa ni pale ambapo hawa wahamiaji haramu kwa mfano Waethiopia wanakuwa wamemaliza vifungo vyao mfano mzuri ni Gereza la Lwanda, Mbeya Waethiopia 41 wamemaliza vifungo vyao zaidi ya miezi mitano, Serikali haina pesa za ku-process kuwarudisha nyumbani kwao wanaendelea kula chakula chetu. Ni lini Serikali itafanya mchakato wa makusudi wa kuwarudisha? Shahidi mzuri ni Mheshimiwa Sugu ambaye alikuwa katika gereza hilo.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mchungaji Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafanya jitihada nyingi sana kuhakikisha kwamba wahamiaji hawa wanarudi majumbani kwao baada ya kukamilisha kifungo chao. Si tu kwa kutumia rasilimali zetu chache tulizokuwa nazo, lakini pia kwa kutumia ushirikiano na uhusiano tuliyokuwanayo na Taasisi ya Uhamiaji ya Dunia (IOM).
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Mchungaji Msigwa atambue kwamba jitihada hizo tuendelee nazo kwa kasi. Hatupendelei wafungwa hawa waendelee kuishi magerezani kwani kufanya hivyo ni kuitia hasara Serikali. Sisi tutaendelea jitihada hizo kadri uwezo unavyoruhusu. Nadhani matukio kama haya ni machache sana nchini wengi tumekuwa tukiwarudisha.