Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kukipatia Kituo cha Chanika gari la patrol?

Supplementary Question 1

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba niwashukuru sana Jeshi la Polisi la Zimamoto. Juzi walipata ajali ya moto katika Kata ya Zingiziwa na ukaunguza maduka zaidi ya 15 lakini kwa mara ya kwanza Zimamoto waliwahi mapema wakasaidia kuzima moto ule pamoja na kwamba mdhara yalikuwa makubwa lakini walisaidia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hiki kituo kimejengwa kwa nguvu za wananchi pamoja na wadau mbalimbali na Naibu Waziri anafahamu kwamba hii sehemu ndiyo mpakani mwa Mkuranga, unaenda Mkuranga, Kisarawe, mapori ya Dondwe na kama alivyosema vingine vyote ni Police Post. Kwa hiyo, naomba hii hoja ya kutafuta gari, kabla ya kuleta hili swali hapa Bungeni nimewasiliana na mapolisi, wanapata shida na eneo ni kubwa, Ukonga sasa ina watu zaidi ya 900,000. Kwa hiyo, kwa kweli tunahitaji gari kwani hilo gari lililopo linafanya kazi ya OCS na ikitokea dharura wanakuwa stranded wanakimbiza watu na pikipiki jambo ambalo ni hatari. Eneo hili Benki ya CRDB imefungwa kwa sababu ya kiusalama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ningeomba hii hoja ya kutafuta gari ipewe uzito, gari liende pale liwe stagnant kwamba kuna gari ambalo viongozi wanalitumia na gari la doria kwa maana ya ku-control Ukonga yote. Kwa hiyo, ningeomba hilo lizingatiwe. Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza…
Haya la pili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Kata ya Kivule tunalo eneo tayari la kituo cha polisi, kama ambavyo Chanika wamejenga wananchi tumechangia, ningeomba commitment ya Waziri au Jeshi la Polisi, ni lini tutaenda kufanya harambee eneo lile kwa sababu tayari wananchi wameweka msingi eneo hili. Bunge lililopita Waziri aliahidi hajaja, kwa hiyo, leo naomba kauli yake.
Lini twende Kivule, tuchangishe fedha tujenge kituo kingine ili tupunguze uhalifu katika eneo lile? Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya ya Mheshimiwa Waitara, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimepokea pongezi zake kwa niaba ya Jeshi la Zimamoto kuhusiana na kazi nzuri ambayo inaendelea kufanywa. Hii inathibitisha juu ya kuimarika kwa huduma za vyombo hivi vilivyo chini ya Wizara ya Mambo ya Nchi ikiwemo Jeshi la Zimamoto katika kutekeleza majukumu yake na kuwapatia huduma wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na swali lake la kwanza, kama ambavyo nimejibu katika swali langu la msingi kwamba tutaangalia uwezekano huo. Kama unavyofahamu kwamba tuna changamoto za magari maeneo mengi nchini, kwa hiyo, tutaangalia vile vigezo na kulingana na idadi ya magari ambayo tutapokea ndipo tutaamua eneo hili linapaswa lipelekewe gari sasa hivi ama baadaye. Hata hivyo, tunatambua umuhimu wa kupeleka gari katika eneo hilo na maeneo mengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ni kuhusu lini tutafanya harambee. Kwanza nimpongeze Mbunge kwa jinsi ambavyo ameweza kuhamasisha kuhusiana na hili suala la harambee, mimi nimwambie tuko tayari hata sasa hivi. Kwa hiyo, baada tu ya Bunge hili Tukufu tukae tuweze kupanga ratiba ya kuweza kufanya hiyo kazi. Tunathamini sana jitihada za Wabunge na wadau mbalimbali katika kusaidia kukabiliana na changamoto za vituo vya polisi nchini na hili jambo tutaliunga mkono.

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kukipatia Kituo cha Chanika gari la patrol?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipatia nafasi. Kwa kuwa tatizo kwenye swali la msingi la 323 la usafiri wa patrol kwa vituo vya polisi lipo karibu nchi nzima. Je, Serikali sasa inajipangaje kwenda kutatua tatizo hili la usafiri wa patrol katika vituo vya polisi hasa katika Jimbo langu la Kavuu?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Kikwembe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama ambavyo nimesema mwanzo kwamba tuna mpango wa kuweza kuona jinsi gani tutapunguza changamoto ya vitendea kazi ikiwemo magari katika kutoa huduma za Jeshi la Polisi. Nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba ndiyo maana sasa hivi tupo katika jitihada za kuweza kukamilisha na kurekebisha mapungufu ambayo yalijitokeza ili tuweze kusambaza magari hayo ambayo yanategemewa kusaidia kupunguza changamoto hiyo ikiwemo katika Jimbo lake, kulingana na vigezo ambavyo nimevieleza katika swali langu la msingi.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWITA M. WAITARA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kukipatia Kituo cha Chanika gari la patrol?

Supplementary Question 3

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mkoa wa Arusha jiografia yake ni pana sana na mkoa huu upo mpakani, hivyo unahitaji uangalizi mkubwa kiusalama, lakini magari mengi ya polisi ni mabovu. Je, ni lini Serikali inafikiria kutuletea magari ya polisi mapya ndani ya Mkoa wa Arusha? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Catherine Magige, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Arusha, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ya magari iliyopo katika Mkoa wa Arusha nayo tunaitambua. Katika mkakati wetu siyo tu kupeleka magari mapya lakini tunajitahidi kuangalia uwezekano wa kuyafanyia matengenezo yale magari ambayo yanaweza yakarekebishika. Kazi hiyo imewezwa kufanywa katika baadhi ya mikoa na Arusha tutaangalia uwezekano wa kuweza kukarabati magari hayo lakini wakati huohuo magari yatakapokuwa yamepatikana tutaweza kuyasambaza katika mikoa yote nchini ikiwemo Mkoa wa Arusha.