Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nassor Suleiman Omar

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Ziwani

Primary Question

MHE. NASSOR SULEIMAN OMARY aliuliza:- Uhakiki wa vyeti feki umeathiri wafanyakazi wengi na wengine wamepoteza ajira zao:- Je, ni wafanyakazi wangapi wamepoteza ajira zao sekta ya elimu pekee?

Supplementary Question 1

MHE. NASSOR SULEIMAN OMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, Serikali ilitoa kauli kwa wale wote walioathirika na zoezi hili kimakosa; Je Serikali imeshawarejesha?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kuna wale ambao walioathirika kimakosa na wako karibu na kustaafu; je Serikali ina kauli gani?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba baada ya zoezi hili yalitokea manung’uniko na vilevile zilitokea rufaa mbalimbali za watumishi ambao walidhani kwamba wameonewa. Serikali ilifanya uchambuzi wa kina, wale ambao walionekana kwamba kulikuwa na makosa katika mchakato huo wamesharejeshwa kazini.
Mheshimiwa Naibu Spika, ameuliza swali lingine kwamba wale ambao walikuwa wanakaribia kustaafu Serikali imewaangalia namna gani? Ukweli ni kwamba kwa makosa ambayo walikuwa wameyafanya walitakiwa wapelekwe Mahakamani, lakini Serikali ilisema tuwasamehe mambo ya kuwapeleka mahakamani kwa makosa ya kughushi na wao wasilete madai mengine.

WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napenda kwanza kupongeza majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini napenda tu kuongezea kuhusiana na idadi ya waliokata rufaa na kurudishwa kazini, jumla ni watumishi 1,907. Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.(Makofi)

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NASSOR SULEIMAN OMARY aliuliza:- Uhakiki wa vyeti feki umeathiri wafanyakazi wengi na wengine wamepoteza ajira zao:- Je, ni wafanyakazi wangapi wamepoteza ajira zao sekta ya elimu pekee?

Supplementary Question 2

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Naibu Spika, zalio la vyeti feki ni Chama cha Mapinduzi na Serikali yake, Mheshimiwa Rais akiwa ni sehemu ya CCM kwa kipindi chote hicho.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunafahamu kwamba Walimu ama Watumishi wengi walianza na cheti cha mtu wakaenda wakasomea taaluma, wakafaulu taaluma zao, wakaenda kulitumikia Taifa hili kwa miaka mingi sana. Serikali ya watu ni Serikali yenye ubinadamu. Sasa nauliza, hivi ni kweli Serikali ya CCM inadhani ni sahihi kwa watu ambao wametumikia hili Taifa kwa miaka 20, wengine mpaka miaka 40 wengine miaka 30, waondoke hivi hivi bila hata kupata kifuta jasho, wanadhani ni sahihi?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, bahati nzuri dada yangu ama mdogo wangu naye ni Mwanasheria. You cannot benefit from your own wrong, suala hili lilikuwa ni jinai, huwezi ukanufaika hata kama uliweza ku-penetrate katika mfumo ikafikia hapo na ndiyo maana Mheshimiwa Rais aliweza kutoa amnesty na amnesty hii haikuweza kutoka bure.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Halima aweze kuelewa suala hili halijazalishwa tu hivi na Serikali ya CCM ni Criminal Offence na ilikuwa ni lazima kufanya hivyo. (Makofi)

Name

Juma Kombo Hamad

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. NASSOR SULEIMAN OMARY aliuliza:- Uhakiki wa vyeti feki umeathiri wafanyakazi wengi na wengine wamepoteza ajira zao:- Je, ni wafanyakazi wangapi wamepoteza ajira zao sekta ya elimu pekee?

Supplementary Question 3

MHE. JUMA KOMBO HAMAD: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Mheshimiwa Naibu Waziri katika jibu la msingi amesema kwamba jumla ya Walimu 3,655 walipoteza kazi baada ya uhakiki na kugundulika na vyeti feki. Nataka kujua tu katika mwaka 2016/2017 na 2017/2018 Serikali kama ilipoteza Walimu hawa; je, hadi sasa imeajiri Walimu wangapi?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya zoezi hilo kukamilika Serikali katika miaka hii miwili 2016/2017 na 2017/2018 imeajiri jumla ya Walimu 6,495. Kati ya hao Walimu wa shule za sekondari wa masomo ya sayansi na hisabati ni 3,728 na Walimu wa shule za msingi ni 2,767. Idadi hiyo ni zaidi ya walioachishwa kazi ni kwa sababu ya kuwa na vyeti vya kughushi.