Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA S. MOLLEL aliuliza:- Je, ni kwa kiwango gani Serikali imetekeleza agizo la Bunge la kukusanya kodi katika huduma za mahoteli kwenye Hifadhi za Taifa kwa njia ya Concession Fee Fixed Rate?

Supplementary Question 1

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniopa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza na vilevile naishukuru Serikali kwa majibu mazuri, lakini pia nimpongeze Waziri kwa kushughulikia mgogoro wa Loliondo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza, tunafahamu awali kulikuwa na tatizo baadhi ya watu na zikiwemo baadhi ya hoteli zilikaidi kukusanya makusanyo haya. Nilitaka tu kujua pamoja na majibu haya mazuri, ni hatua zipi zimechukuliwa kwa wale ambao walikaidi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni hatua zipi zilichukuliwa kwa hoteli ambazo zilikiuka ukusanyaji huu wa kodi hii yaani concession fees?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza Mheshimiwa Amina Mollel kwa kazi nzuri ambayo amekuwa akiifanya, hasa katika kuwatetea watu wenye ulemavu. Amekuwa akifanya kazi hiyo vizuri sana. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli wakati tunaanza utekelezaji wa tozo hii baadhi ya hoteli zilikuwa bado hazijapata elimu ya kutosha kwa nini tozo hi imeanzishwa. Kutokana na jitihada ambazo Serikali ilichukua kuwaelimisha wamiliki wa hoteli zote hizo kwa nini tumeanzisha tozo hiyo na kwa nini ni muhimu kulipa na kwa nini tumeachana na mtindo wa zamani, basi hoteli zote hivi sasa zimeelimika na zote zinatekeleza. kwa sababu, zote zina-comply na utaratibu huu mpya basi hakuna hatua ambazo zimechukuliwa. Kwa wale ambao watakaidi ndiyo hapo tutachukua hatua lakini kwa hivi sasa zote zinatekeleza.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA S. MOLLEL aliuliza:- Je, ni kwa kiwango gani Serikali imetekeleza agizo la Bunge la kukusanya kodi katika huduma za mahoteli kwenye Hifadhi za Taifa kwa njia ya Concession Fee Fixed Rate?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, inasikitisha sana Watanzania wamekuwa wakilipa Concession Fee sawa na wageni. Je, ni kwa nini Serikali isione umuhimu wa kuwa-charge Concession Fee Watanzania tofauti na wageni?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue nafasi hii kumjibu Mheshimiwa Catherine Magige, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Concession Fees inalipwa katika hoteli za kitalii na ni kwa wageni wanaotoka sana sana nje ya nchi, kwa wenyeji hawatozwi. Katika hilo, zile hoteli ambazo zinamilikiwa na Shirika la Hifadhi ya Taifa hazitozwi hiyo Concession Fee. Kwa hiyo, hii ni specifically kwa zile hoteli za kitalii.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA S. MOLLEL aliuliza:- Je, ni kwa kiwango gani Serikali imetekeleza agizo la Bunge la kukusanya kodi katika huduma za mahoteli kwenye Hifadhi za Taifa kwa njia ya Concession Fee Fixed Rate?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, asante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sekta ya utalii inachangia takribani 17% ya pato la Taifa na wamiliki wa hoteli hizi za kitalii wamekuwa wakitozwa kodi nyingi au tozo nyingi sana takribani 46 na wamekuwa na malalamiko ya muda mrefu. Je, ni kwa nini Serikali isifikirie utaratibu mwingine wa kuwarahisishia hao wawekezaji kwenye hoteli za kitalii ulipaji wa tozo hizo?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Paresso, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kumekuwa na kodi na tozo nyingi ambazo zimekuwepo katika baadhi ya hoteli, lakini jitihada zilizochukuliwa na Serikali ya Awamu ya Tano ni kuhakikisha hizi kodi zote zinahuishwa zinabaki chache. Mwaka jana, kama mtakumbuka, kuna baadhi ya kodi ziliondolewa na mwaka huu hivi sasa kuna kazi inaendelea kwa ajili ya kuhuisha kuangalia hizi kodi ziunganishwe kwa pamoja ili kurahisisha walipaji hao kusudi wasiwe na kodi za hapa na pale. Kwa hiyo, jitihada hizo zinafanyika na Mheshimiwa awe na subira, pale tutakaposoma bajeti yetu atasikia ni hatua gani ambazo tunakusudia kuzichukua.