Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia vikundi vya wanawake waliopo katika Mkoa wa Rukwa katika suala la mikopo na kuwapatia elimu ya ujasiriamali?

Supplementary Question 1

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza kwa kuwa wanawake wengi wamehamasika sana kuanzisha VICOBA na wengine wameanzisha vikundi mbalimbali kwa lengo la kujikwamua kimaisha lakini wamekuwa wakiangaishwa sana kwa kupata hiyo asilimia 10; sasa ni lini Serikali itaweka mazingira mazuri ili hata kama hiyo asilimia 10 ipo lakini wawekewe mazingira mazuri ya kupata mikopo kwenye mabenki?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kwa kuwa asilimia 10 ya wanawake, walemavu na vijana inachelewa sana kuwafikia walengwa; sasa basi kwa nini Serikali isipunguze masharti ya kukopa kwenye mabenki ili wanawake waweze kukopa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kwamba ukilinganisha masharti yaliyopo katika upatikanaji wa hii asilimia tano ambayo imekusudiwa kwenda kwa wanawake na vijana masharti yake ni rahisi sana ukilinganisha na masharti ambayo yanatolewa na taasisi za fedha kama mabenki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nachoomba kumekuwa na dhana potofu kama vile fedha hizi zinatolewa kama vile ni pesa ambayo haitakiwi kurejeshwa, ni wajibu wetu kuhakikisha kwamba tunasimamia ili pesa hizi zinazotolewa ziweze kurejeshwa na wengine waweze kukopeshwa, vizuri tukawa na mfumo ambao ni rasmi ili kuhakikisha kila shilingi ambayo inatolewa inarudi ili wakinamama wengine waweze kukopeshwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili angependa masharti ya benki yakapunguzwa ili wakina mama waweze kuna access ya kwenda kukopa kwenye taasisi hizi za fedha. Hili ambalo lipo ndani yuwezo wetu kama ofisi ya Rais TAMISEMI ni kuhusiana na asilimia tano kama ambavyo swali lake la msingi lipo ni vizuri kwanza tuhakikishe kwamba fedha hizi ambazo zinakusanywa asilimia tano inatengwa na zile zinazotengwa zinakopwa ikionekana kwamba kuna gap ya uhitaji hapo ndio twende kwenye taasisi zingine za fedha.

NAIBU WAZIRI VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sambasamba na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, TAMISEMI ni kwamba katika mwezi huu wa tatu Mheshimiwa Rais alikaa na wadau mbalimbali wenye masuala ya kibiashara na viwanda katika moja ya jambo ambalo alizungumza ni kuwashauri watu wa mabenki kuweza kupunguza riba na kuweka masharti ambayo yatawasaidia zaidi wafanyabiashara. (Makofi)

Name

Magdalena Hamis Sakaya

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Kaliua

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia vikundi vya wanawake waliopo katika Mkoa wa Rukwa katika suala la mikopo na kuwapatia elimu ya ujasiriamali?

Supplementary Question 2

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi naomba nimuulize Mheshimiwa naibu Waziri swali moja la nyongeza.
Kwa kuwa mfuko huu wa kina mama na vijana unatakiwa uchangiwe na maeneo mawili kwa maana ya Serikali Kuu itoe fedha kwa ajili ya ule mfuko lakini pia Halmashauri zetu zitoe asilimia 10 kwa ajili ya ule mfuko. Kwa baadhi ya Halmashauri ikiwepo Kaliua tunajitahidi sana kutenga ile asilimia 10 lakini Serikali haitoi ile sehemu yake.
Je, Serikali haioni kwamba kutokutenga ni kuendelea kudumaza wanawake na vijana kutokupata mikopo kwa kiasi kinachotakiwa? Ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la msingi lilivyo ni juu ya Halmashauri kuhakikisha kwamba wanatenga asilimia 10 na yeye katika Halmashauri yake anasema wamekuwa wakitenga hii asilimia 10 kwa uzuri zaidi.
La kwanza ambalo naomba tuhamasishe na kuagiza Halmashauri zote ni kuhakikisha kwamba wanaiga mfano mzuri kama ambavyo Halmashauri ya Kaliua inafanya ili kwanza tuwe na uhakika katika hii asilimia 10 ambayo inatengwa, je, inawafikia akina mama na baada ya hapo tukiwa na uhakika na mfumo ambao ni rasmi unatumika Serikali haitasita kwa sababu lengo la Serikali ni kuhakikisha kwamba inawakomboa wanawake na vijana na ndio maana sheria ilipitishwa ili kuhakikisha kwamba tunawawezesha wanawake na vijana katika suala zima la uchumi.

Name

Kiteto Zawadi Koshuma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kusaidia vikundi vya wanawake waliopo katika Mkoa wa Rukwa katika suala la mikopo na kuwapatia elimu ya ujasiriamali?

Supplementary Question 3

MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana; kwa kuwa Halmashauri nyingi sana zinakabiliwa na changamoto ya kuwa na mapato madogo na hivyo kushindwa kabisa kutenga fedha hizi za asilimia 10, asilimia tano wka vijana na asilimia tano kwa akina mama kwa ukamilifu.
Je, Serikali inachukua hatua gani kwa Halmashauri ambazo hazitengi kabisa na hata tuliona katika bajeti ya mwaka jana kuna Halmashauri mbili zilikuwa zimetajwa kwamba hazijatenga kabisa fedha hizi za akinamama na watoto, lakini hatujaona Serikali ikiwachukulia hatua. Je, Serikali inachukua hatua gani kwa Halmashauri ambazo hazitengi kabisa fedha hizi za akina mama?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna excuse yoyote ambayo itasababisha Halmashauri isamehewe eti kwa sababu makusanyo yake ni kidogo. Kwa sababu hata kama ungekusanya shilingi moja, shilingi moja hiyo tunachotaka asilimia 10 ya shilingi moja si ya kwako. Wewe ni kama conduit tu unatakiwa pesa hiyo iende kwa wanawake na vijana.
Kwa hiyo, kama ambavyo tulisisitiza juzi katika jibu ambalo alijibu mwenzangu tutachukua hatua kali kwa Halmashauri yoyote na hasa Wakurugenzi wahakikishe kwamba asilimia 10 ya kutenga katika mapato ya ndani sio option, it’s a must! Na yeyote ambaye hatatekeleza hilo hatua kali zitachukuliwa dhidi yake.