Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA aliuliza:- Je, nini sera ya Serikali katika kubadilisha mandhari ya maeneo ambayo ni squatter au ya wazi kwa kuwekeza katika majengo ili kuwa na makazi ya kisasa kwa ajili ya wananchi kwa kutumia ardhi iliyopo katika eneo husika?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. MARY M. MWANJELWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili madogo ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Jiji la Mbeya halina master plan, general plan scheme na limekuwa katika data collection ya almost bilioni1.5. Swali langu ni kwamba je, Serikali haioni kwamba sasa ni wakati muafaka wa ku-push hili jambo lifike mwisho?
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, Mheshimiwa Naibu Waziri, Mheshimiwa Waziri walishatembelea katika Jiji la Mbeya na nilikuwa bega kwa bega, mguu kwa mguu na Mheshimiwa Naibu Waziri yeye mwenyewe amejionea ni jinsi gani Jiji la Mbeya limekuwa ni la squatter kwa muda mrefu sana, hususan katika maeneo ya Isanga, Ilemi, Nzovwe, Iyunga, Kalobe, Nonde, Mwakibete, Sinde, Soweto; yote haya na mengineyo mengi ni Squatter kwa muda mrefu sana. Swali langu kwa Serikali, haioni kuwa sasa ni wakati muafaka tena wa kusaidia up grading katika maeneo hayo? Nakushukuru.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI:Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Mwanjelwa kwa sababu mara nyingi katika Bunge hili kama tutakumbuka kila akileta swali la Makazi mara nyingi anapenda kutolea mfano wa Mbeya ambao unakuwa pengine haujawa na master plan mpaka dakika hii, lakini ni mji ambao unakuwa kwa kasi kubwa. Sasa hivi Wizara yangu inayo miji karibu 28 ambayo tayari michakato yake ya master plan inaendelea.
Mheshimiwa Spika, Jiji la Mbeya bado halijawa, mimi niwaombe sana watu wa Mbeya tuanze maandalizi ya kuwa na master plan kwa sababu mchakato mzima lazima uanzie kwenye eneo husika. Ni wazi kama wataanzisha kama ambavyo miji mingine imeanza kama Arusha, Dar es Salaam na Mwanza ambayo imeishaanza, sasa mimi niseme tu kwamba Jiji la Mbeya nalo sasa linatakiwa lianze mchakato huo kwa sababu ni suala ambalo litafanya libadilishe kabisa mandhari ya mji wenyewe.
Mheshimiwa Spika, kwa swali lake la pili, ni kweli nikiri kwamba nilikwenda Mbeya na tuliongozana naye, na maeneo anayoyataja ni kweli hayavutii kwa kasi ya namna ambavyo ilivyo. Mimi nimpongeze kwa sababu pia, amekuwa na kiu ya kutaka kuona mabadiliko yanakuwepo.
Mheshimiwa Mwanjelwa naomba nikuhakikishie kwamba kwenye maeneo ya Iyunga, Kalobe, Uyoe, Nonde, Mwakibete, Sinde, Isanga, Soweto na kadhalika, kweli nilijionea maeneo hayako katika hali nzuri.
Mheshimiwa Spika, sasa mimi niseme pale ambapo mtaanza master plan, basi tutawekeza pia katika maeneo hayo kuhakikisha kwamba yanabadilika ikiwa ni pamoja na kubadili mandhari kama ambavyo ulivyoomba kuweza kufanya ile pulling ya land kuweza kuleta pamoja na kuweza kujenga majengo ambayo pengine yatapendeza zaidi au kuweka mandhari ambazo zitafanya ule mji kweli uonekane kweli ni Jiji.