Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO (k.n.y MHE. NJALU D. SILANGA) aliuliza:- Wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka 2015, Mheshimiwa Rais aliahidi kujenga nyumba za watumishi katika Makao Makuu ya Wilaya ya Itilima katika Kijiji cha Langabidili. Je, ni lini ahadi hiyo itaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 1

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza kabisa napenda kutoa pongezi kwa Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri. Nina maswali mawili tu madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba ujenzi unaendelea, lakini unaendelea kwa kasi ndogo sana.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba wanatoa fedha kwa wakati na kuhakikisha ujenzi huo unaendelea kwa haraka ili ukamilike, kwa sababu watumishi wanapata shida sana kusafiri kutoka Bariadi hadi Ligangabilili?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, Serikali ina mpango gani juu ya kuikaribisha National Housing (Shirika la Nyumba la Taifa) kwenye Mkoa wa Simiyu kuweza kujenga nyumba za National Housing katika mkoa nzima yaani katika wilaya zake zote tano ili kuweza kuwasaidia wafanyakazi kupata makazi mazuri ya kuweza kuishi? Ahsante sana.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NABU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwa ajenda ya kasi ndogo ya utendaji wa kazi naomba nichukue concern hiyo, tutafanya follow up kuangalia ni kinachoendea. Nilifika pale Itilima, ni kweli changamoto kubwa ilikuwa ni tatizo la fedha. Tukaja kufanya uhangaikaji katika ofisi yetu ndiyo maana tukapata zile fedha nyingine zikaenda kule, ili kuweza kuongeza speed ya ufanyaji wa kazi pale. Vilevile tutawasiliana na wenzetu wa Itilima ili kuangalia kuna kitu gani ambacho kinakwaza. Nia ni kuongeza speed ya utendaji wa kazi ili hatimaye wananchi na hasa watumishi wa Itilima waweze waweze kukaa katika mazingira rafiki.
Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la National Housing kuweza kukaribia katika Mkoa wa Simiyu kwa ajili ya kujenga nyumba; ni wazo nzuri, na niwashukuru sana wenzetu wa National Housing wamekuwa wakishiriki ujenzi wa nyumba katika maeneo mbalimbali. Hata hivyo ninaamini kwamba tutapata maelekezo vizuri juu ya nini cha kufanya kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, ambayo ni Wizara yenye dhamana katika eneo hilo, hasa katika Mkoa wa Simiyu.
Mheshimiwa Spika, mara nyingi sana wanaambiwa kwamba watenge maeneo maalum kwa ajili ya kuwakaribisha National Housing. Hata hivyo kuna maeneo mengine National Housing walijenga nyumba lakini matumizi ya zile nyumba imekuwa ni changamoto kubwa na sana katika Halmashauri zetu.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tuchukue kama ni challenge nyingine katika upande wetu vilevile, kwamba endapo National Housing wanakuja kuwekeza basi lazima nisiamasishe Halmashauri tuwe tayari kuhakikisha kwamba tunazitumia nyumba hizo, kwa sababu fedha hizi zisipotumika vizuri tutatengeneza gharama kubwa kwa Serikali yetu. Kwa hiyo, ni wazo zuri Mheshimiwa Nyongo na mimi kama TAMISEMI nitalichukua jambo hili, nitaongea na dada yangu Mheshimiwa Angelina, Naibu Waziri wa Ardhi tuangalie namna ya kufanya ili wananchi wa Simiyu waweze kufanya kazi kwa ajili ya kuwasaidia wananchi wa Simiyu.

NAIBU WAZIRI WA ARDHI:
Mheshimiwa Spika, Ahsante sana. Napenda kujibu swali la nyongeza na kumshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri alivyojibu majibu yake mazuri kuhusiana na suala la National Housing.
Kwa Mkoa wa Simiyu tayari National Housing wana maeneo waliyopewa katika Wilaya mbili, Wilaya ya Busega pamoja na Wilaya ya Bariadi. Tatizo lililoko katika wilaya zingine ni kwamba bado hawajawa tayari kutenga maeneo.
Mheshimia Spika, kwa maelekezo ambayo pia Mheshimiwa Rais alitoa kwamba National Housing ili waweze kujenga na waweze kutoa nyumba zao kwa bei nzuri lazima Halmashauri husika iwe imeshatenga eneo ambalo halina changamoto kwa maana kwamba litahitaji fidia, litahitaji miundombinu. Kwa hiyo, wao wafanye maandalizi tayari viwanja waweke National Housing watakwenda kujenga. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, la pili pia, kuna Wilaya zaidi ya 30 ambazo National Housing wamejenga na nyumba zile zinaharibika, ikiwemo Mkoa wa Rukwa, nyumba zimejengwa lakini watu hawajaingia wala hawajapanga. Kwa hiyo, wakati mwingine ku-pull up resources katika maeneo mengine inakuwa ni ngumu; na katikati hapa walisimama kwa ajili ya kuendeleza eneo la Iyumbu. Kwa hiyo halmashauri yoyote itakayokuwa tayari National Housing wataweza kuja, lakini tuwaombe pia mfanye maandalizi yale ya msingi ili National Housing waweze kushiriki.

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STANSLAUS H. NYONGO (k.n.y MHE. NJALU D. SILANGA) aliuliza:- Wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka 2015, Mheshimiwa Rais aliahidi kujenga nyumba za watumishi katika Makao Makuu ya Wilaya ya Itilima katika Kijiji cha Langabidili. Je, ni lini ahadi hiyo itaanza kutekelezwa?

Supplementary Question 2

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi nipate kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa watumishi wengi wa Serikali wamehamishiwa Mkoa wa Dodoma, je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha watumishi wote wa Serikali wanapata nyumba na waache kuhangaika hangaika mitaani kwa sababu nyumba za National Housing hazitoshi kwa watumishi wa Serikali waliohamishiwa Dodoma?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NABU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la mate wangu wa Bulombora dada yangu Mheshimiwa Maryam Msabaha kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kwanza ni kweli, ni nia njema Serikali. Tumesema kwamba Serikali ya Awamu ya tano si mlimila dole, kwamba inatekeleza kile ilichokiahidi; imesema tunaamia Dodoma na tumehamia sasa hivi Dodoma. Naomba niwahakikishie kwamba Serikali imeweka mipango vizuri kupitia nyumba za TBA, National Housing na CDA. Mkiangalia kule kama mnapita Iringa Road zimekarabatiwa, lengo lake kubwa ni kwamba kuweza kuwa-accommodate watumishi wote wa Serikali.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo tunashukuru sana kwa suala hili zuri, Serikali imeweka mpango vizuri. Niwaahakikishie watumishi wote kwamba msiwe na hofu mtakapokuja Dodoma, Serikali inapanga mipango mizuri, na ndiyo maana hata National Housing sasa wanajenga huu mji mpya pale. Hii yote ni kwa ajili ya kuhakikisha kwamba kwenye mchakato huu wa Mji Mkuu wa Serikali kuhamia Dodoma, Dodoma iweze ku-accommodate watumishi hawa wanaokuja hapa.