Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatatua au kumaliza kabisa tatizo la baadhi ya wakazi wanaoitwa Wahamiaji katika Vijiji vya Nyabuzume, Tiring’ati, Nyaburundi na Bigegu ambao kwa miaka mingi wamekuwa wakisumbuliwa na hoja hiyo bila kupewa ufumbuzi?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Waziri, lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Katika nchi yetu raia wengi hawana vyeti vya kuzaliwa. Katika Mkoa wa Mara lipo kabila la jamii ya Waluo kwa maana ya Wajaluo. Kwa kuwa wao ni wengi, wengi wao wanaishi Kenya na inaonekana kwamba, zipo hisia tu kila Mjaluo anayeonekana Tanzania hapa anakuwa kama mhamiaji. Ni lini sasa hawa Wajaluo ambao ni raia wa Tanzania wanaoishi mpakani na hasa kwenye vijiji nilivyovitaja, ni lini watapewa haki yao ya msingi kama raia kuliko kusumbuliwa kila siku kuonekana kama wahamiaji wakati wao ni wa karibu hapa wanaishi maeneo ya Rorya?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; hivi mtu akiwa mlowezi, ni lini ulowezi wake unakoma? (Kicheko)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru sana babu yangu, Mheshimiwa Getere, kwa maswali mawili mazuri sana. Moja, hili alilosema la Wajaluo, si Wajaluo tu watu ambao wana makabila yanayoingiliana na nchi za jirani kupata misukosuko ya aina hiyo, yapo matatizo haya Mikoa yote ya pembezoni.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nimwambie tu kuhusu lini hilo litakwisha ni kwamba, Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani, kupitia Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa wako katika hatua za mwisho za kufanya utambuzi na badaye kuwapatia vitambulisho wananchi wote wa Tanzania. Kwa hiyo, pale watakapokuwa wameshapata vitambulisho hapatakuwepo na mtu tena kuhisiwa hisiwa kwa ajili ya makabila kuwa yana mwingiliano katika nchi za jirani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu walowezi na lenyewe liko karibu sana na hili nililolisema. Kuna taratibu za walowezi, watu waliolowea hapa kupewa uraia wao. Kwa hiyo, kwa wale ambao watakidhi vigezo na wakapewa uraia watapewa vitambulisho na hilo litakuwa limekoma la kuwa walowezi na watakuwa Raia wa Tanzania. (Makofi)

Name

Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatatua au kumaliza kabisa tatizo la baadhi ya wakazi wanaoitwa Wahamiaji katika Vijiji vya Nyabuzume, Tiring’ati, Nyaburundi na Bigegu ambao kwa miaka mingi wamekuwa wakisumbuliwa na hoja hiyo bila kupewa ufumbuzi?

Supplementary Question 2

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Naibu Spika, swali la Bunda la Mheshimiwa Getere, halina tofauti sana katika Jimbo langu la Serengeti katika Vijiji vya Rwamchanga, Masinki, Ring One na maeneo mengine, ambapo kuna jamii ya Wakisii, Wanandi, ambao wamekuwepo kabla ya uhuru. Je, ni lini Serikali itawafanya kuwa raia wa Tanzania? Maana tumeona maeneo mengine wakimbizi…

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimjibu babu yangu Mbunge wa Serengeti kwamba, kwa wale wote ambao wameshakaa tangu enzi ya uhuru na wako Tanzania na wangependa kuwa raia wa Tanzania, pana taratibu. Wafike kwenye Ofisi za Uhamiaji watapewa taratibu za kuhalalisha uraia wao kwa sababu, uraia hatuwapi tu kwa kutamka, lazima wapite kwenye taratibu zile ili kuweza kuweka kumbukumbu sawa kwamba, wameshakuwa raia.