Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. HAMIDU H. BOBALI aliuliza:- Kumekuwa na Maswali yaliyokosa majibu stahiki kila mara kuhusu suala la mabaki ya mjusi (Dinosaur) yaliyopo Ujerumani, kila linapoulizwa au kuchangiwa hapa Bungeni:- (a) Je, ni nini kauli ya mwisho ya Serikali kuhusu faida ambayo wananchi wa Mkoa wa Lindi na Tanzania kwa ujumla watanufaika kutokana na mabaki hayo? (b) Je, kwa nini Serikali isishauriane na Serikali ya Ujerumani kuboresha barabara na huduma za maji katika Kijiji cha Manyangara katika Kitongoji cha Namapwiya, ambapo mabaki ya mjusi huyo yalichukuliwa?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Naomba nimuulize maswali mawili ya nyongeza Mheshimiwa Naibu Waziri:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa lugha yoyote ambayo tunaweza tukazungumza haiondoi ukweli kwamba dinosaurian huyu ni mali yetu sisi Watanzania, kwa hiyo, manufaa yoyote yanapaswa sisi tuanze kunufaika. Sasa kwa kuwa, Serikali imesema kwamba, Serikali ya Ujerumani imeji- commit katika masuala matatu aliyoyasema Mheshimiwa Waziri katika jibu lake la msingi, naomba jibu kwamba, ni lini utekelezaji wa haya utafanyika, ili tuweze kujua kwa sababu, wakati anajibu amesema kwamba, majibu yalikuwa yanatolewa wakati huo kwa wakati huo. Sasa sasa hivi nataka katika hizi commitment tatu ambazo Serikali ya Ujerumani wamezitoa, ni lini sasa utekelezaji utafanyika?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, hivi sasa tunapozungumza kumekuwa na tendency ya watalii kuwa wanakwenda, mwaka huu tumepokea watalii zaidi ya watano ama sita wamekwenda, lakini walikuwa wanapata kikwazo kikubwa cha barabara. Sasa Mheshimiwa Waziri haoni kwamba, kuna haja ya kujenga barabara hata kwa dharura ya kwenda kule, ili njia ikawa inapitika wakati tunasubiri hayo makubwa ambayo Serikali ya Ujerumani imeji- commit? Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Bobali kwa kuungana na Wabunge waliotangulia kabla yake, lakini pia na mawazo ya Wabunge wengine wote humu ndani ambao wana nia njema ya kuhakikisha kwamba, rasilimali na maliasili za nchi hii zinanufaisha Taifa hili. Hongera sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kuhusu swali lake kwamba, ni lini hatua hizi zinazozungumziwa zitachukuliwa. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hatua hizi ni za majadiliano ya pande mbili. Hivi ninavyozungumza Naibu Waziri wa Mambo ya Nje alikuwa asafiri wiki hii, kutokana na changamoto nyingine za Kiserikali safari hiyo imesogezwa mbele kwa wiki moja. Atakapokwenda, matokeo ya mazungumzo hayo pengine yatakuja sasa na mpango kazi na ratiba.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni vigumu kusema sasa hivi kwa upande mmoja bila kujua sasa kwa pamoja sisi sasa, Serikali ya Tanzania na Ujerumani, ratiba yetu ya utekelezaji wa haya ambayo yanaonekana kwamba tunakubaliana inaanza lini. Wakati huo utakapofika basi, utapata jawabu kwamba lini tunaanza na tunategemea kukamilisha lini programu tunayoizungumzia.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini katika swali lake la pili, anataka mpango wa muda mfupi, kwamba, kwa sasa hivi hatuwezi kufanya utaratibu pale, hivyo hivyo palivyo kwa sababu tu za kihistoria watu wanajua kwamba alitoka mjusi mkubwa pale wa vipimo na viwango tunavyovizungumzia watu wanataka kwenda kuona kwa mazingira hayahaya yaliyopo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu hili nafikiri nipate nafasi sasa ya kufika kwa uhalisia kabisa kwenye eneo hilo na kuona barabara hiyo inayozungumziwa, kwanza ni barabara ya aina gani. Barabara ya Mkoa, ni barabara ya Halmashauri au ni barabara ambayo jukumu lake linatakiwa kutekelezwa na nani Serikalini. Baada ya hatua hiyo tutaweza kujipanga vizuri zaidi kutekeleza, ili hayo mambo mazuri tunayokusudia yaweze kutekelezwa. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMIDU H. BOBALI aliuliza:- Kumekuwa na Maswali yaliyokosa majibu stahiki kila mara kuhusu suala la mabaki ya mjusi (Dinosaur) yaliyopo Ujerumani, kila linapoulizwa au kuchangiwa hapa Bungeni:- (a) Je, ni nini kauli ya mwisho ya Serikali kuhusu faida ambayo wananchi wa Mkoa wa Lindi na Tanzania kwa ujumla watanufaika kutokana na mabaki hayo? (b) Je, kwa nini Serikali isishauriane na Serikali ya Ujerumani kuboresha barabara na huduma za maji katika Kijiji cha Manyangara katika Kitongoji cha Namapwiya, ambapo mabaki ya mjusi huyo yalichukuliwa?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Ningependa Serikali ituambie kwa muktadha wake kabisa kwa sababu haya ambayo wameelezea kuyafanya it is a peanut! Ni madogo sana. Kujenga kituo cha Makumbusho, kuwafadhili watu kupata fani ya malikale ni hela ndogo sana! Mjusi huyu tangu apelekwe kule ni kiasi gani, kwa maana ya faida kutokana na utalii, umeiingizia Serikali ya Ujerumani? Kwa nini Serikali ya Tanzania tusiingie angalau mkataba tuwaambie angalau asilimia tano au 10 ya mapato watuletee kutokana na mjusi ambaye anaingiza fedha za utalii kule Ujerumani kuliko hizi peanut package ambazo wanatupa ambazo hazisaidii nchi yetu? (Makofi)

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshauri tu Dada yangu kwamba, masuala yanayohitaji utafiti na takwimu ni vizuri kusubiri utafiti na takwimu utoe matokeo badala ya kutoa kauli za jumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa labda niseme tu kwa kifupi kwamba, mjusi huyu au mijusi hawa waliotoka Tanzania kule Ujerumani na bahati nzuri wako baadhi ya Waheshimiwa Wabunge hapa wamefika pale mahali na mmojawapo ni Mheshimiwa Dkt. Kafumu ni kwamba, mijusi hawa wawili ni sehemu tu moja ya vivutio vingine vya malikale vilivyoko katika jumba la makumbusho kule Ujerumani ambalo ni kubwa na lina vitu vingi na kiasi ambacho hata kukokotoa kwamba, mijusi wawili wa Tanzania wanazalisha nini ndani ya jumba ambalo watu wanakuja kuangalia vitu vingi ambavyo Wajerumani hawa walivitoa katika nchi za Afrika walizotawala wakati huo katika maeneo mengi na wako wengi kwa kiasi hicho.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa mambo matatu ambayo yanafahamika tayari ni kwamba, viingilio katika makumbusho ya Elimu Viumbe huko Berlin ni Euro 3.5 hadi Euro nane, kwa jumba zima ambalo lina vivutio vingi ambapo wanafunzi, watafiti na wazee wanaingia bure, hilo la kwanza.
Pili, asilimia 95 ya Bajeti ya Makumbusho ya Elimu Viumbe Berlin kule, inatoka katika Serikali Kuu na Serikali ya Mji wa Berlin, maana yake ni kwamba, hiyo makumbusho haina hata uwezo wa kuweza kujiendesha yenyewe.
Tatu, Makumbusho ya Elimu Viumbe ya Berlin ina kumbi nyingi za maonesho, Ukumbi wa Dinosauria ukiwa ni mmoja tu, kwa hiyo, ni vigumu kujua kiasi halisi cha fedha kinachopatikana kutokana na kuingia na kuona masalia ya mijusi wa Tanzania. Vilevile kwenye makumbusho hii kuna nakala ya masalia ya mijusi kutoka nchi nyingine duniani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunapozungumzia suala la kuboresha eneo hili ambako mijusi wametoka, ili liweze kuwa eneo la utalii si sahihi kusema kwamba, kipato kitakachotoka pale kitakuwa peanut. Pia, pili, ukifundisha watu kwenye taaluma hiyo ya malikale ambayo itaendelea kufanya tafiti katika nchi nzima hii, athari yake ni kubwa. Kwa hiyo, kiufupi unaweza kusema tu kwamba, watu hawa sasa badala ya kutupa samaki wanataka kutupa boti, wanataka kutufundisha kuvua, ili tuweze kuvua wenyewe samaki tupate faida zaidi kuliko kupewa samaki wa siku moja tu. (Makofi

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. HAMIDU H. BOBALI aliuliza:- Kumekuwa na Maswali yaliyokosa majibu stahiki kila mara kuhusu suala la mabaki ya mjusi (Dinosaur) yaliyopo Ujerumani, kila linapoulizwa au kuchangiwa hapa Bungeni:- (a) Je, ni nini kauli ya mwisho ya Serikali kuhusu faida ambayo wananchi wa Mkoa wa Lindi na Tanzania kwa ujumla watanufaika kutokana na mabaki hayo? (b) Je, kwa nini Serikali isishauriane na Serikali ya Ujerumani kuboresha barabara na huduma za maji katika Kijiji cha Manyangara katika Kitongoji cha Namapwiya, ambapo mabaki ya mjusi huyo yalichukuliwa?

Supplementary Question 3

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na kwamba kwa kweli, Naibu Waziri nadhani hili swali la Mbunge wa Tarime amelinanihii. Pamoja na dinosaur Mikoa ya Lindi na Mtwara ina utajiri mkubwa wa utamaduni ambao unaweza kutumika kama sehemu ya utalii na kufaidisha watu wa Kusini. Je, ni lini Serikali au Wizara itaamua kuanza kuwekeza kenye utamaduni wa Kusini ili utumike kama utalii wa watu wa Kusini?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ni kweli Kusini ni sehemu ya maeneo yaliyoko nchi nzima, Tanzania nzima ambayo yana utajiri mkubwa wa kihistoria hasa Historia ya Utamaduni wa Mtanzania katika makabila yote tuliyonayo na kwamba, eneo hilo pia, ni kivutio cha kutosha kabisa chenye sifa ya kuweza kuwa maeneo ya shughuli za utalii.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nirudie tu kama ambavyo nimejibu swali kama hili mara nyingi nikiwa nimesimama hapa, mbele ya Bunge lako Tukufu. Ni kwamba, Halmashauri zote, ikiwemo ile ambayo Mheshimiwa Mbunge ni Mjumbe wa Baraza la Madiwani waharakishe kutekeleza Agizo la Serikali la kuorodhesha maeneo yote ambayo yako kwenye maeneo yao, Halmashauri zao, ambayo yana sifa hizo tunazozizungumzia, ili tulete Wizarani yaweze kupitiwa, yachambuliwe, ili kuweza kuwekwa katika viwango na kuweza kuona namna gani mahitaji yake yakoje, ili tuweze kuendelea katika kuvitangaza na badaye kuwavutia watalii kwa ajili ya shughuli za utalii.