Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:- Sehemu kubwa ya Misitu ya Hifadhi ndani ya Wilaya ya Same ni Msitu wa Shengena ambao ni chanzo cha Mito mikubwa ya Nakombo, Hingilili, Yongoma na Saseni ambayo maji yake yanatumiwa na wakazi wa Majimbo ya Same Mashariki, Mlalo na Korogwe Vijijini:- • Je, ni lini Serikali itaanzisha doria kulinda Msitu wa Shengena kuzuia uharibifu unaoendelea ikiwemo uchomaji moto ambao pia unaathiri maisha ya watu? • Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanzisha utaratibu wa uvunaji wa miti iliyokomaa katika Msitu wa Shengena na kuweka mkakati wa kuotesha miti mingine ili msitu uwe endelevu? • Je, Serikali inasema nini juu ya athari za kimazingira zinazotokana na uchimbaji wa madini ya Bauxite unaoendelea katika Msitu wa Shengena?

Supplementary Question 1

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nina maswali mawili ya nyongeza. Kwanza, kwa kuwa kutokana na majibu ya Mheshimiwa Waziri, uvunaji wa miti hata baada ya kukomaa unakatazwa; na kwa kuwa Jimbo la Same Mashariki hakuna hata vitalu vya miti. Je, ni namna gani Serikali itahakikisha kwamba kunaanzishwa vitalu ili wananchi waweze kupata miche ya kuweza kupanda kwenye maeneo yao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa wananchi wa Jimbo la Same Mashariki wengi walihamasishwa na walipanda miti mingi na wengi walichukua mikopo ili wapande miti kwa biashara, lakini inapofika wakati wa uvunaji wanahangaishwa sana na Halmashauri hata pale Wizara ilipotoa maagizo kwamba waruhusiwe kuuza miti yao. Je, Mheshimiwa Waziri anatoa tamko gani hasa kwa Halmashauri ya Same ili wajue kwamba Wizara ina msimamo gani juu ya suala la wananchi waliopanda miti yao waweze kuivuna na kuiuza kibiashara? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kaboyoka katika swali lake la kwanza, anataka kujua ni namna gani Serikali itawawezesha wananchi wa kule Same Mashariki kuwa na vitalu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye swali lililotangulia, katika mkakati wa upandaji miti Kitaifa, kila Halmashauri ya Wilaya imepangiwa kupanda miti kwa wastani wa miti milioni mbili kila mwaka. Nasema ni wastani, kwa sababu itazingatia ukubwa wa Halmashauri, idadi ya watu, hali ya hewa ya Halmashauri inayohusika, kuona maeneo rafiki ambayo miti inaweza kupandwa. Kwa hiyo, ziko Halmashauri nyingine zitapanda miti zaidi ya hiyo, Halmashauri nyingine zinaweza zikapanda miti pungufu ya hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, uwepo wa vitalu vya miti ni suala ambalo litafanyika baada ya kazi ya mkakati huu kuwa imefikia katika Halmashauri hiyo na kwa hiyo, mtaweza kupata ushauri kutoka Wizarani chini ya mkakati huo nilioutaja ili muweze kuoneshwa ni maeneo yapi, ya ukubwa gani muweze kuwa na vitalu vya kuweza kupanda miti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali la pili la Mheshimiwa Kaboyoka, anataka tamko kuhusiana na miti ambayo inakatwa kwenye maeneo ambayo ni ya miti ya kupandwa ukilinganisha na hatua za udhibiti kwa mujibu wa sheria ambayo inazuia ukataji miti hovyo ambayo inaendana na uharibifu wa mazingira.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda tu nimshauri Mheshimiwa Mbunge kwamba ni jukumu la Serikali sasa kuweza ku-balance na tunaposimamia ukataji wa miti kwa ajili ya matumizi mbalimbali ikiwemo mkaa na matumizi mengine, hatutakataza matumizi ya miti halali ambayo imepandwa kwa njia halali, isipokuwa usimamizi wake unaendana na upataji wa vibali mahususi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Taasisi chini ya Wizara zilizoko katika Halmashauri hiyo zitaweza kutoa utaratibu ambao chini ya utaratibu huo miti halali iliyopandwa kwa madhumuni hayo ikiwa imekidhi vigezo vya kisayansi kama vile kukomaa na mambo mengine, utaratibu huo hauwezi kuzuiliwa.
Mheshimiwa Mbunge, ufafanuzi zaidi kuhusiana na suala hili unaweza ukapatikana wakati wowote ule baada ya session hii.

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:- Sehemu kubwa ya Misitu ya Hifadhi ndani ya Wilaya ya Same ni Msitu wa Shengena ambao ni chanzo cha Mito mikubwa ya Nakombo, Hingilili, Yongoma na Saseni ambayo maji yake yanatumiwa na wakazi wa Majimbo ya Same Mashariki, Mlalo na Korogwe Vijijini:- • Je, ni lini Serikali itaanzisha doria kulinda Msitu wa Shengena kuzuia uharibifu unaoendelea ikiwemo uchomaji moto ambao pia unaathiri maisha ya watu? • Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanzisha utaratibu wa uvunaji wa miti iliyokomaa katika Msitu wa Shengena na kuweka mkakati wa kuotesha miti mingine ili msitu uwe endelevu? • Je, Serikali inasema nini juu ya athari za kimazingira zinazotokana na uchimbaji wa madini ya Bauxite unaoendelea katika Msitu wa Shengena?

Supplementary Question 2

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, ni dhahiri mbinu zote za ulinzi zinazotumika pamoja na ulinzi shirikishi bado hazijasaidia kutatua tatizo la uharibifu wa misitu na hususan misitu ya asili kwenye nchi yetu. Je, Serikali inafikiria nini sasa kuhusu mbinu mbadala ya kuhakikisha kwamba misitu yetu inahifadhiwa na kuendelezwa kwa ajili ya kizazi kijacho?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza siyo jambo jema sana kuthibitisha hapa kwamba jitihada zote zile za kisheria na zile za kupitia ushirikishaji wa wananchi zimeshindikana kuweza kuzuia tatizo hili la uharibifu wa mazingira. Napenda kuungana na Mheshimiwa Mbunge kuona kwamba jitihada hizo bado zipo na zinatakiwa kuendelea. Tunatakiwa tu kuboresha namna ambayo tumekuwa tukifanya hapo nyuma, maisha bado yanaendelea ili tuweze kuhakikisha kwamba uhifadhi wa mazingira unaendelea kuwepo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tutaongeza idadi ya Wataalam ili waweze kusimamia vizuri zaidi, lakini pia tutaweza kusimamia misitu ili tuweze kupunguza uharibifu wa mazingira.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:- Sehemu kubwa ya Misitu ya Hifadhi ndani ya Wilaya ya Same ni Msitu wa Shengena ambao ni chanzo cha Mito mikubwa ya Nakombo, Hingilili, Yongoma na Saseni ambayo maji yake yanatumiwa na wakazi wa Majimbo ya Same Mashariki, Mlalo na Korogwe Vijijini:- • Je, ni lini Serikali itaanzisha doria kulinda Msitu wa Shengena kuzuia uharibifu unaoendelea ikiwemo uchomaji moto ambao pia unaathiri maisha ya watu? • Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanzisha utaratibu wa uvunaji wa miti iliyokomaa katika Msitu wa Shengena na kuweka mkakati wa kuotesha miti mingine ili msitu uwe endelevu? • Je, Serikali inasema nini juu ya athari za kimazingira zinazotokana na uchimbaji wa madini ya Bauxite unaoendelea katika Msitu wa Shengena?

Supplementary Question 3

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa uwepo wa Msitu wa Shengena, Msitu wa Shangai na Msitu wa Bombo ndiyo unaosaidia uwepo wa Hifadhi ya Mkomazi; lakini katika Msitu huo wa Bombo kuna uvamizi mkubwa unaofanywa na wananchi. Je, ni lini sasa Serikali itaweka mipaka (beacons) kutenga eneo hili la Msitu wa Bombo ambao ni msitu maalum wa kuvuta mvua? (Makofi)

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni kweli kabisa msitu wa Bombo ni msitu muhimu sana kwa ajili ya Hifadhi ya Mkomazi, lakini pia kwa ajili ya ikolojia nzima ya eneo la Mkomazi. Sasa lini Serikali itaweka beacons?
Mheshimiwa Mwenyekiti, zoezi la uwekaji wa beacons linaendelea nchi nzima na nataka nimhakikishie kwamba kama bado hatujafika Mkomazi, nitakwenda kuangalia ratiba na kuona lini tunafika huko ili niweze kumpa tarehe kabisa, lini tunaweka katika hifadhi hiyo. Kwa hiyo, tuonane baada ya hapa, tuweze kuona ni lini beacons zinawekwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, huo ni mpango wa Serikali ambao unaendelea sasa hivi kuweka beacons au kuweka alama za mipaka katika hifadhi zote nchini.

Name

Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:- Sehemu kubwa ya Misitu ya Hifadhi ndani ya Wilaya ya Same ni Msitu wa Shengena ambao ni chanzo cha Mito mikubwa ya Nakombo, Hingilili, Yongoma na Saseni ambayo maji yake yanatumiwa na wakazi wa Majimbo ya Same Mashariki, Mlalo na Korogwe Vijijini:- • Je, ni lini Serikali itaanzisha doria kulinda Msitu wa Shengena kuzuia uharibifu unaoendelea ikiwemo uchomaji moto ambao pia unaathiri maisha ya watu? • Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanzisha utaratibu wa uvunaji wa miti iliyokomaa katika Msitu wa Shengena na kuweka mkakati wa kuotesha miti mingine ili msitu uwe endelevu? • Je, Serikali inasema nini juu ya athari za kimazingira zinazotokana na uchimbaji wa madini ya Bauxite unaoendelea katika Msitu wa Shengena?

Supplementary Question 4

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru nami kuweza kupata muda wa kuuliza swali moja la nyongeza. Mamlaka ya Wanyamapori maeneo ya Ngwala, Itiziro na kule Guwa wamevamia vijiji hivyo na hivyo wamewasambaza wananchi, wamewanyang’anya mashamba, wamenyang’anya mbao na mali zao nyingine; na Mheshimiwa Naibu Waziri nilikwambia. Sasa nataka Mheshimiwa Naibu Waziri anithibitishie humu ndani mbele ya Bunge kwamba ni lini tutaongozana mimi na yeye twende tuka-solve mgogoro huo kwa ajili ya wanyamapori maeneo ya Ngwala?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kifupi kama ulivyoelekeza, ni kwamba kwanza mpaka unahusisha pande mbili na ni vigumu sana upande mmoja kusema mwingine amemwingilia mwingine kwenye mpaka wake. Nafikiri njia sahihi, wote wawili wanaweza wakawa mahali pamoja halafu kila mmoja akaangalia vigezo nani ameingia kwa mwingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na swali lake, lini tutaweza kwenda; nilimwambia kabla na narudia tena kusisitiza, tukimaliza Bunge hili la Bajeti mimi na yeye tutapanga ratiba ambayo itakuwa ni rafiki, twende kwenye maeneo hayo, halafu tutaangalie namna gani tunaweza kutatua tatizo hilo.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza:- Sehemu kubwa ya Misitu ya Hifadhi ndani ya Wilaya ya Same ni Msitu wa Shengena ambao ni chanzo cha Mito mikubwa ya Nakombo, Hingilili, Yongoma na Saseni ambayo maji yake yanatumiwa na wakazi wa Majimbo ya Same Mashariki, Mlalo na Korogwe Vijijini:- • Je, ni lini Serikali itaanzisha doria kulinda Msitu wa Shengena kuzuia uharibifu unaoendelea ikiwemo uchomaji moto ambao pia unaathiri maisha ya watu? • Je, Serikali haioni umuhimu wa kuanzisha utaratibu wa uvunaji wa miti iliyokomaa katika Msitu wa Shengena na kuweka mkakati wa kuotesha miti mingine ili msitu uwe endelevu? • Je, Serikali inasema nini juu ya athari za kimazingira zinazotokana na uchimbaji wa madini ya Bauxite unaoendelea katika Msitu wa Shengena?

Supplementary Question 5

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Jimbo la Mbulu Mjini mipaka yake kwa asilimia 50 inazungukwa na misitu ya asili na maji wanayotumia viumbe wakiwemo binadamu yanatoka katika misitu hiyo. Hivi sasa maji hayo yameanza kupungua ndani ya misitu. Je, ni lini Serikali itapeleka wataalam watakaofanya utafiti katika misitu inayozunguka Jimbo la Mbulu Mjini ili iweze kufanyia kazi taarifa yake ya utafiti kwa ajili ya kushauri jamii inayozunguka misitu hiyo? (Makofi)

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nataka kusema tu Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba ameshafika Ofisini kwangu siyo mara moja na suala hili tumelizungumza, tumeliweka wazi, tumesema kwamba nina maslahi kwa wananchi wa Jimbo lile. Kwa hiyo, ni lini tunaenda? Jibu ni lile lile ambalo nilisema kabla; nimemwambia Ofisini na narudia tena hapa kwamba mara baada ya Bunge hili la bajeti, nina ziara ndefu sana, ratiba hiyo inahusisha pia Jimbo lake. (Makofi)