Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY aliuliza:- Madiwani ni wasimamizi wakuu wa rasilimali za halmashauri na wakati wa uchaguzi wa Madiwani, Wabunge na Rais ni mafiga matatu:- • Je, ni lini Serikali itawaongezea posho ya mwezi Madiwani hao? • Je, ni lini Serikali itawapa usafiri na msamaha wa kodi Madiwani katika vyombo vya usafiri?

Supplementary Question 1

MHE. KISWAGA B. DESTERY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali kwamba uchumi ukiwa nzuri tutaongeza, ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza. Kwa kuwa majibu yanaonesha kwamba kila baada ya miaka miwili Serikali ilikuwa ikiongeza posho za Waheshimiwa Madiwani mpaka 2015 na leo tuko 2017 tayari miaka miwili. Je, Serikali haioni kwamba kulingana na mazingira wanayofanyia kazi Waheshimiwa Madiwani pamoja na kupanda kwa maisha, sasa ni muda muafaka wa kuongeza posho angalau kidogo ili waweze kumudu maisha? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa mikopo hii wanayokopa kwenye mabenki ni kutokana na posho yao, Serikali haioni kwamba hizi fedha ni ndogo zaidi, hawawezi hata kupeleka kwenye usafiri. Je, Serikali kwa nini isiweke ruzuku kama inavyotoa kwa Waheshimiwa Wabunge nusu ili Waheshimiwa Madiwani waweze kumudu usafiri? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kwamba kwa wastani wa miaka miwili posho ya Madiwani inaongezeka; naomba nikiri kwamba Madiwani wetu wanafanya kazi kubwa sana. Mheshimiwa Kiswaga na Waheshimiwa Wabunge naomba niwaambie kwamba kwa bahati nzuri nilipata fursa ya kukaa na Madiwani katika vikao vya ALAT kule Musoma na hapa Dodoma na hii imekuwa ni concern yao kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili ni kweli na sasa hivi limewasilishwa katika mamlaka husika na kwamba sasa linafanyiwa kazi na linachambuliwa vizuri. Mambo yakikamilika vizuri basi watapata mrejesho kwamba Serikali imeamua vipi katika jambo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la ruzuku kwa vyombo vya usafiri nadhani ni wazo zuri naomba tulichukue, na Serikali itaangalia ni jinsi gani itafanya kwa sababu Madiwani wanafanya kazi kubwa, lakini siwezi kutoa commitment kutoka hapa kwamba nini kinafanyika kwa sasa.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY aliuliza:- Madiwani ni wasimamizi wakuu wa rasilimali za halmashauri na wakati wa uchaguzi wa Madiwani, Wabunge na Rais ni mafiga matatu:- • Je, ni lini Serikali itawaongezea posho ya mwezi Madiwani hao? • Je, ni lini Serikali itawapa usafiri na msamaha wa kodi Madiwani katika vyombo vya usafiri?

Supplementary Question 2

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri hapa amesema wataongeza kipato kwa Madiwani ikiwa mapato ya Serikali yataongezeka; lakini kwa mwaka sasa Serikali imekuwa ikitangaza kuongezeka kwa mapato, yaani makusanyo yamekuwa makubwa, ninachokitaka badala tu ya kuwalipa posho kwa nini sasa Madiwani wasilipwe mishahara kama tunavyolipwa sisi Wabunge ili wafanye kazi hiyo kwa moyo. Ahsante sana.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Menyekiti, Mheshimiwa Mwenyekiti, wazo la kulipwa mshahara na posho; kwa sababu kuna nafasi mbalimbali zimetengwa kwa utaratibu wake; kwa utaratibu Madiwani wanalipwa posho sawasawa na Wenyeviti wa Vijiji, kwamba kuna posho ile ya asilimia 10 kwa Wenyeviti wa Vijiji, lakini kuna posho maalum ya Madiwani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu wazo la mshahara, hili tuseme ni wazo tu ambalo Wabunge wanatoa kuona jinsi gani jambo hili linaboreshwa. Hata hivyo, mara nyingi Serikali inafanya tathmini katika maeneo mengi zaidi na hasa kuangalia wage bill ya Serikali itakuwaje baadaye endapo Madiwani wataingizwa katika eneo hilo kwa wakati mmoja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kwa hiyo nasema kwamba ni mawazo au chemchem ambayo inasaidia kuboresha ili unapofika wakati tuangalie jinsi ya kufanya; lakini kwa sasa hivi utaratibu tunaokwenda nao ni utaratibu wa posho kwa mujibu sheria.

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY aliuliza:- Madiwani ni wasimamizi wakuu wa rasilimali za halmashauri na wakati wa uchaguzi wa Madiwani, Wabunge na Rais ni mafiga matatu:- • Je, ni lini Serikali itawaongezea posho ya mwezi Madiwani hao? • Je, ni lini Serikali itawapa usafiri na msamaha wa kodi Madiwani katika vyombo vya usafiri?

Supplementary Question 3

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Huko nyuma Serikali ilikuwa ikitoa mafunzo kwa Madiwani ambapo mafunzo hayo yaliwajengea uwezo mkubwa ikiwa ni pamoja na kufahamu mipaka yao. Je, ni lini Serikali itarejesha mafunzo haya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba, kwa kipindi cha nyuma kulikuwa na mafunzo ya Madiwani ambayo yalikuwa yakitolewa ili kuwajengea uwezo waweze kufanya kazi yao vizuri kwa sababu wao ndio wanafanya maamuzi katika Mabaraza yetu ya Madiwani katika halmashauri zetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, hapa katikati mafunzo kidogo yalisimama. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba mchakato huu wa mafunzo umeanza katika maeneo mbalimbali na mafunzo haya yataweza kuwafikia Madiwani, lengo kubwa ni kujenga uwezo wao kwa kadri itakavyoonekana kwamba itafaa.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY aliuliza:- Madiwani ni wasimamizi wakuu wa rasilimali za halmashauri na wakati wa uchaguzi wa Madiwani, Wabunge na Rais ni mafiga matatu:- • Je, ni lini Serikali itawaongezea posho ya mwezi Madiwani hao? • Je, ni lini Serikali itawapa usafiri na msamaha wa kodi Madiwani katika vyombo vya usafiri?

Supplementary Question 4

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali moja dogo. Bahati nzuri mimi nimekuwa Diwani kwa miaka kumi na tano na Mwenyekiti wa Halmashauri. Kazi ya Udiwani zamani ilikuwa mikutano tu, unakuja kuitwa kwenye kikao unarudi nyumbani; lakini kwa kuwa sasa hivi Udiwani ni kusimamia miradi, ikianza kujengwa darasa mpaka jioni uko pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa Mheshimiwa Naibu Waziri atakubaliana nami kwamba mtekeleze yale maagizo au maelekezo ya Tume ya Lubeleje ya kushughulikia maslahi ya Madiwani, muwalipe Madiwani posho ya kutosha ili nao waweze kumudu maisha kwa sababu wanashinda kwenye miradi mpaka jioni?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la Mbunge wa siku nyingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiri wazi kwamba kuna Tume iliundwa ambayo Mheshimiwa Lubeleje ambaye ni Mbunge; ndiyo maana namwita Senior MP alikuwa ndiye Mwenyekiti wa Tume ile. Tume ile ilitoa mapendekezo mbalimbali na miongoni mwa mapendekezo hayo yaliyotolewa katika Tume ya Lubeleje ndiyo haya yaliyosababisha kufanya maboresho ya hata hivi viwango tunavyoviona hivi sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kikubwa zaidi na tukiri wazi kwamba Madiwani ndio wenye jukumu kubwa sana la kusimamia kazi za kule site. Ndiyo maana nimesema kwamba Serikali inalitazama hili kwa upana wa hali ya juu; kwamba nini tufanye. Kwa hiyo, hali itakapokuwa imeridhisha na maamuzi yakifanyika naamini kwamba posho ya Madiwani itaongezeka. Lengo ni kuwawezesha kufanya vizuri katika usimamizi wao wa kazi kwani wanafanya kazi kubwa na hakuna mtu anayebeza katika hili.

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY aliuliza:- Madiwani ni wasimamizi wakuu wa rasilimali za halmashauri na wakati wa uchaguzi wa Madiwani, Wabunge na Rais ni mafiga matatu:- • Je, ni lini Serikali itawaongezea posho ya mwezi Madiwani hao? • Je, ni lini Serikali itawapa usafiri na msamaha wa kodi Madiwani katika vyombo vya usafiri?

Supplementary Question 5

MHE. KANGI A.LUGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona. Waheshimiwa Wabunge hapa kila tukigusa maombi ya fedha kwenye miradi ya maji, barabara na afya tunaambiwa pale hali ya uchumi itakapokuwa nzuri. Leo pia tunagusa suala la posho za Madiwani tunaambiwa hali ya fedha itakapokuwa nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Taarifa ya Hali ya Uchumi ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwenye bajeti hii anasema hali ya uchumi ni nzuri na kwenye ukurasa wa tatu wa taarifa ya Benki, hii hapa ninayo, wanasema uchumi umekuwa kwa asilimia saba, ni kiwango kikubwa sana cha kimataifa. Sasa je, hii hali ya uchumi wanayotaka ni asilimia ngapi ndiyo hali ya uchumi itakayokuwa nzuri? Mimi nashindwa kuelewa.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapozungumza hali ya uchumi itakapokuwa nzuri; ni kweli tunakwenda vizuri, lakini malengo ya Serikali hii ya Awamu ya Tano ni kwenda mbali zaidi na ndiyo maana najua suala hili la posho si kwa Madiwani peke yake ni hata Walimu pamoja na watumishi wengine, kila mtu anataka angalau mshahara wake uweze kuongezeka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana tumesema kwamba acheni Serikali kwanza ijipange vizuri katika hili. Tunajua tuna vipaumbele vyetu vingi sana ambavyo ni lazima vyote tuvitekeleze. Ngoja tujipange vizuri, lakini kila kundi litaweza kufikiwa kwa kadri Mheshimiwa Rais alivyojipanga na Serikali yake ya Awamu ya Tano na hatimaye kila mtu ata-realize kwamba kweli hatukufanya makosa katika kupanga mipango muafaka kwa ajili ya nchi yetu.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY aliuliza:- Madiwani ni wasimamizi wakuu wa rasilimali za halmashauri na wakati wa uchaguzi wa Madiwani, Wabunge na Rais ni mafiga matatu:- • Je, ni lini Serikali itawaongezea posho ya mwezi Madiwani hao? • Je, ni lini Serikali itawapa usafiri na msamaha wa kodi Madiwani katika vyombo vya usafiri?

Supplementary Question 6

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Pamoja na posho za Madiwani, Wenyeviti ya Vijiji na Vitongoji kuwa ndogo, lakini bado halmashauri nyingi zimekuwa zinawakopa viongozi hawa posho hizi kiasi kwamba wana muda mrefu hawalipwi. Sasa Serikali iko tayari kutoa kauli yenye muda maalum kuhakikisha kwamba viongozi hawa wanalipwa madeni yao ya posho zao? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, juzi nilipokea concern kutoka Buchosa kwamba Madiwani wamekopwa takribani miezi minane, hili halikubaliki hata kidogo. Wakati mwingine utagundua kwamba ni uzembe tu wa usimamizi nzuri. Watu wanafanya collection lakini wakati mwingine katika suala la kuwalipa Madiwani wanaona kama ni hisani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nitoe maelekezo kwamba halmashauri mbalimbali tunafanya makusanyo, makusanyo yale yanakusanywa na Madiwani ndio wanaofanya maamuzi, lazima mwende mkalipe posho za Madiwani kwa kadri iwezekanavyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Madiwani wanafanya kazi kubwa lakini posho zao hazilipwi na wakati huo huo shughuli nyingine zinaendelea ambazo Madiwani hao ndio waliosimamia kupata fedha hizo, haitokubalika. Tutaenda kufuatilia halmashauri moja hadi nyingine. Naomba niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge kwamba tuta-cross check na halmashauri mbalimbali ambazo kwa makusudi kabisa wamekataa kuwalipa madiwani either kwa kiburi au kwa jambo lingine lolote.