Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. MARY P. CHATANDA aliuliza:- Mhimili wa Mahakama kama ilivyo mihimili mingine unahitaji kuwa na eneo la uhakika la kufanyia kazi na vitendea kazi vya uhakika:- (a) Je, ni lini Wilaya ya Korogwe itajengewa Mahakama ya Wilaya?

Supplementary Question 1

MHE. MARY P.CHATANDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pia nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri kwa kutukumbuka Korogwe, Kilindi na Mkinga kwamba mwaka huu wa fedha watatupatia fedha kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama. Swali la nyongeza, kwa kuwa vile vile Mahakama hizi zimekuwa na upungufu mkubwa wa wafanyakazi hususan Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo. Je, Serikali ina mpango gani sasa wa kutupelekea Mahakimu Mahakama za Mwanzo Korogwe Mjini na Vijijini? Ahsante sana.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU:
Mheshimiwa Spika, kabla sijamjibu swali lake napenda nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Korogwe kwa hatua madhubuti ambayo wameianza ya ujenzi wa Mahakama ya Mwanzo ya Mnyuzi na hivi sasa najua wanasubiri tu ramani kuanza ujenzi huo.
Mheshimiwa Spika, kuhusu lini tutawapelekea watumishi kwa maana ya kada ya Mahakimu, nimwondoe tu hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba pale ambapo tutakuwa tuna uwezo wa kibajeti wa kuweza kufanya kazi hiyo tutafanya, kwa sababu tumeanza na ukarabati wa miundombinu, basi jambo hili likikamilika pia tutaona namna ya kuweza kuongezea watumishi katika Mahakama za Korogwe ili nao waweze kupata huduma hii ya Kimahakama. (Makofi)

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. MARY P. CHATANDA aliuliza:- Mhimili wa Mahakama kama ilivyo mihimili mingine unahitaji kuwa na eneo la uhakika la kufanyia kazi na vitendea kazi vya uhakika:- (a) Je, ni lini Wilaya ya Korogwe itajengewa Mahakama ya Wilaya?

Supplementary Question 2

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Wilaya ya Karatu ilikuwa na Mahakama za Mwanzo nne lakini hivi sasa imebaki Mahakama moja tu iliyoko Karatu Mjini ndio inayofanya kazi, Mahakama zingine za Mwanzo zimesimama kutokana na upungufu wa Mahakimu wa ngazi hiyo. Je, ni lini Serikali itapeleka Mahakimu wa Ngazi ya Mahakama za Mwanzo ili huduma hiyo muhimu ipatikane kwenye ngazi za Tarafa kule chini? Ahsante. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU:
Mheshimiwa Spika, tumepokea ombi lake na natumaini mwaka wa fedha unaokuja tutayafanyia kazi maombi yake ili na wakazi wa Karatu waweze kupata fursa ya kupata watumishi wa kuwahudumia katika Idara hii ya Mahakama.

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. MARY P. CHATANDA aliuliza:- Mhimili wa Mahakama kama ilivyo mihimili mingine unahitaji kuwa na eneo la uhakika la kufanyia kazi na vitendea kazi vya uhakika:- (a) Je, ni lini Wilaya ya Korogwe itajengewa Mahakama ya Wilaya?

Supplementary Question 3

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Spika, asante sana, Wilaya ya Ulanga pamoja na kuwa na Mbunge kijana machachari lakini haina Mahakama ya Wilaya. Je, wananchi wa Ulanga wanaisikiliza Serikali yao ya hapa kazi tu inawaambia nini kuhusiana na jengo la Mahakama ya Wilaya? (Kicheko/Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU:
Mheshimiwa Spika, ukiangalia katika miaka ya hivi karibuni Serikali imeendelea kujenga Mahakama tofauti na miaka iliyopita na kwa mwaka huu wa fedha unaokuja 2017/2018, tumetengewa kiasi cha shilingi billioni 46 kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama. Nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge na kwamba ninacho kitabu hapa kinachoelezea Mahakama zitakazojengwa, kwa hiyo nimwombe tu afike katika Ofisi yetu aangalie, ni orodha ndefu sana ya Mahakama na naamini kabisa eneo lake la Jimbo la Kilombelo lilitakiwa pia liwe limezingatiwa ili nao waweze kupata huduma hii.