Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RUTH H. MOLLEL aliuliza:- Serikali yoyote duniani inaendeshwa na rasilimali watu wenye weledi, ari na uzalendo. Ili Watumishi hawa wafanye kazi kwa moyo wanahitaji kuthaminiwa, kutambuliwa mchango wao na kupewa stahili zao bila bughudha:- Je, Serikali imebuni mkakati gani wa kuwapa motisha na ari Watumishi wa Umma ili wafanye kazi kwa kujituma badala ya vitisho?

Supplementary Question 1

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, ahsante. Namshukuru Waziri kwa majibu yake lakini ninayo maswali mawili ya nyongeza. Tangu Serikali ya Awamu ya Tano ingie madarakani annual increment zimesimama na hata kwa bajeti hii ya mwaka huu, ya Waziri wa Fedha aliyoitoa juzi hakuna mahali popote tunaona kuna increment yoyote kwa ajili ya Watumishi wa Umma. Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba mishahara ya watumshi inaboreshwa ili waweze kupambana na hali ya uchumi na hali ya maisha ambayo imepanda?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, vile vile tangu Awamu ya Tano imeingia madarakani training ilikuwa imesimamishwa na training ni sehemu moja ya kuwapa watumishi motisha na kuwawezesha kupata weledi. Je, Serikali itaanza lini kutekeleza mpango wa mafunzo ambao upo na haujatekelezwa? (Makofi)

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, kuhusiana na suala la annual increment nadhani kama atakuwa alifuatilia vizuri hotuba ya Mheshimiwa Rais wakati wa Mei Mosi ilielezwa kabisa bayana kwa Vyama vya Wafanyakazi annual increment mwaka huu itakuwepo.
Mheshimiwa Spika, pia ukiangalia katika bajeti ya mshahara maana yake yeye amesema kwamba hajaiona, obviously kwenye bajeti ya mshahara huwezi kusema sasa hapa hii ndio itakuwa nyongeza ya mwaka. Bajeti ya mwaka jana ilikuwa ni trioni 6.6, bajeti ya mwaka huu ni nadhani trioni 7.25.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, asubiri aone katika mwaka wa fedha utakapoanza endapo annual increment hiyo itakuwepo au la! Nadhani tusichanganye na kima cha chini cha mshahara, nadhani atakuwa ameelewa kwa sababu yeye amekaa Utumishi anafahamu, lakini nimtoe hofu nimweleze tu kwamba Mheshimiwa Rais alishaahidi kupitia siku ya Mei Mosi kwamba nyongeza ya mwaka itakuwepo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na kupandisha Watumishi mishahara Serikali imekuwa ikifanya hivyo kila mara hali ya kiuchumi inapoimarika na tumekuwa tukijitahidi na tutakuwa tukifanya hivyo kila mara kwa mujibu wa takwimu, lakini vilevile kwa kuangalia mfumuko wa bei pamoja na takwimu nyinginezo zinazotolewa na shirika letu la NBS.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na mafunzo; mafunzo hayajawahi kusitishwa, mafunzo yanaendelea na hata kama mkiangalia katika bajeti mbalimbali za Mawizara zilizopitishwa, kupitia kwa waajiri wao na Maafisa Masuuli wamekuwa wakitenga bajeti zao. Niendelee kusisitiza kupitia Bunge lako Tukufu waajiri waendelee kuweka mipango yao ya mafunzo ya kila mwaka, wajitahidi kufuatilia mipango hiyo lakini zaidi waweze kutenga fedha kwa ajili ya kuendeleza na kutoa weledi kwa ajili ya watumishi wao.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RUTH H. MOLLEL aliuliza:- Serikali yoyote duniani inaendeshwa na rasilimali watu wenye weledi, ari na uzalendo. Ili Watumishi hawa wafanye kazi kwa moyo wanahitaji kuthaminiwa, kutambuliwa mchango wao na kupewa stahili zao bila bughudha:- Je, Serikali imebuni mkakati gani wa kuwapa motisha na ari Watumishi wa Umma ili wafanye kazi kwa kujituma badala ya vitisho?

Supplementary Question 2

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali. Kwanza niipongeze Serikali hii ya Awamu ya Tano kwa kazi nzuri ambayo imekuwa ikiifanya katika nchi hii. Hivi karibuni kulikuwepo na zoezi la uhakiki wa vyeti feki na katika uhakiki huo kuligundulika kwamba kuna vyeti feki katika taasisi nyingi na kusababisha sasa kuwepo na upungufu mkubwa sana katika taasisi mbalimbali na hasa katika hospitali zetu na Halmashauri zetu. Sasa napenda kujua je, ni lini sasa zoezi la kuziba zile nafasi ambazo wale wenye vyeti feki wameondolewa zitaweza kuzibwa ili kusaidia wale wafanyakazi waliopo wasifanye kazi kwenye mazingira magumu sana? (Makofi)

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze kwa namna ambavyo amekuwa akifuatilia ustawi wa watumishi lakini pia kwa namna ambavyo anafuatilia upungufu huu uliojitokeza wa watumishi kutokana na zoezi lililoendeshwa la wenye vyeti feki.
Mheshimiwa Spika, nipende tu kusema kwamba, tumekuwa tukieleza humu ndani tayari kibali kimeshatolewa cha ajira 15,000. Tulikuwa tunafanya mashauriano na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, wameshatuletea orodha maana yake ilikuwa ni lazima tujue katika kila kituo ni nafasi ipi ambayo iko wazi.
Mheshimiwa Spika, nipende tu kusema kwamba katika maeneo ambayo yameathirika sana ni sekta ya elimu pamoja na sekta ya afya kwa zaidi ya asilimia 70 na zaidi kidogo. Pia kwa sekta ya afya tu peke yake zaidi ya watumishi 3,360 wamekumbwa katika zoezi hili. Nimweleze tu kwamba tayari tumeshaanza mchakato huo na muda si mrefu nafasi hizo zitazibwa.