Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Mji wa Ruangwa Mkoani Lindi una madini mengi lakini wachimbaji walio wengi wa madini hayo ni wachimbaji wadogo wadogo ambao hawana zana za kisasa za kuchimba madini. Je, Serikali haioni haja ya kuwasaidia kwa kuwapa mikopo ili waweze kununua zana za kisasa za uchimbaji?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa majibu haya ambayo ameyatoa Mheshimiwa Naibu Waziri wa Madini na Nishati, majibu ya jumla ambayo yanaelekeza katika maeneo yote ya uchimbaji wa madini, ningependa kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba katika Mkoa wetu wa Lindi tunayo madini mbalimbali lakini katika eneo hili la Wilaya ya Ruangwa tuna madini ya green gannet, green tomalin, dhahabu, safaya na graphite pamoja na madini mengine, lakini maeneo haya wachimbaji waliopo ni wachimbaji wadogo wadogo ambao wanatumia zana ambazo si bora, zana hafifu.
Ningependa kujua tunayo Sera na Sheria Mpya ya Madini ya kuwatengea maeneo wachimbaji hao wadogo wadogo, sera hii imewanufaisha vipi na Sheria mpya ya Madini wachimbaji wadogo wadogo wa maeneo hayo ya Wilaya ya Ruangwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili la nyongeza ningependa kumuomba Mheshimiwa Waziri, yupo tayari sasa kuja katika Mkoa wetu wa Lindi maeneo ya Ruangwa kuja kuona maeneo ya machimbo haya ya madini na kuona changamaoto mbalimbali zinazowakumba wachimbaji hao wadogo wadogo na kuona namna gani Wizara yake inaweza kuwasaidia? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote sio tu nipo tayari kwenda Lindi isipokuwa nipo tayari kufuatana na Mheshimiwa Hamida twende pamoja mpaka Lindi. Kwa hiyo kwa ruhusa ya Kiti chako nipo tayari na ukitupa ruhusa hata kabla ya Bunge kumalizika nipo tayari Mheshimiwa Mbunge kwenda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimpongeze Mheshimiwa Hamida Abdallah anavyoshughulikia masuala haya, tangu ameingia katika Bunge hili tumeshashirikiana naye sana na katika juhudi zake amefanikisha kutenga maeneo mawili muhimu sana katika Mkoa wa Lindi, eneo mojawapo ni Kitowelo pamoja na eneo la Maguja Nachingwea, kwa hiyo, Mheshimiwa hongera sana kwa kazi zako.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa Mkoa wa Lindi una madini mengi sana, baadhi ya madini yanayopatikana katika Mkoa wa Lindi kama alivyoyataja Mheshimiwa Mbunge ni pamoja green tomaline, safaya pamoja na madini load garden, lakini kuna dhahabu, kuna chumvi kuna madini mengi yanayoitwa ruby ambayo ni madini ya mfano sana katika nchi yetu. Kwa mkoa wa Lindi una utajiri wa madini mengi tu pamoja na chumvi. Nichukue nafasi hii kuwahamsisha sana Waheshimiwa Wabunge wa Mkoa wa Lindi na maeneo mengine ili kuhamasishe wachimbaji wadogo wakachimbe madini hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sera na sheria kweli kabisa zinataja kuwatengea maeneo wananchi nchi nzima. Katika Mkoa wa Lindi tumeshatenga maeneo yafuatayo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumetenga eneo la hekta 300 Kilwa Masoko kwa ajili ya uchimbaji wa madini ya chumvi, tumetenga maeneo ya hekta 525 eneo la Kitowelo katika Wilaya ya Liwale na eneo la kilometa 7.2 katika eneo la Maguja Wilaya ya Nachingwea na tunakwenda sasa kutenga eneo lingine la hekta 825 katika eneo linaitwa Hoteli Tatu. Hivyo, Mheshimiwa Mbunge tunaendelea kutenga maeneo kama na sera ya madini inavyoelekeza.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Mji wa Ruangwa Mkoani Lindi una madini mengi lakini wachimbaji walio wengi wa madini hayo ni wachimbaji wadogo wadogo ambao hawana zana za kisasa za kuchimba madini. Je, Serikali haioni haja ya kuwasaidia kwa kuwapa mikopo ili waweze kununua zana za kisasa za uchimbaji?

Supplementary Question 2

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kwa kuuliza swali la nyongeza, linalohusiana na masuala ya madini kama ambavyo Mheshimiwa Hamida ameuliza hapo mwanzoni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo lililopo Ruangwa linafanana kabisa na tatizo lililopo Jimbo la Ndanda katika kijiji cha Chiwata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kijiji cha Chiwata sasa hivi kuna uwekezaji unaendelea kwa ajili ya madini ya graphite, lakini uwekezaji huu umekuwa ukufanyika kwa siri kubwa sana kiasi kwamba wananchi wa Chiwata hawafahamu nini kinaendelea na hawako tayari kuendelea kukaa kimya, wamenituma nimuulize Waziri.
Je, Serikali ipo tayari sasa kuleta mkataba ambao utatumika kwa ajili ya uchimbaji wa madini katika kijiji cha Chiwata ili kuondoa sintofahamu ambayo inaweza ikajitokeza miaka ya baadaye ya kuhitaji kufanya review na ku-cancel mikataba ile? Ninaomba commitment ya Serikali ni lini iko tayari kuleta mkataba ule ujadiliwe na Bunge ili ukatumike kwa ajili ya manufaa ya wananchi wa Jimbo la Ndanda? Ahsante.(Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Mheshimiwa Mwambe nampongeza sana, tumekuwa tukishirikiana naye sana kwenye masuala ya wachimbaji wadogo mbali na masuala yake ya masuala ya nishati kwenye eneo lake. Kuhusiana na eneo analolitaja yuko mwekezaji ambaye sasa anajiandaa na kukamilisha utafiti, atakapokamilisha utafiti ndio aanze shughuli za uchimbaji, kwa hiyo hata hatua ya kuingia mkataba bado.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo nikuombe sana Mheshimiwa tukae, tujue kitu gani kinahitajika na itakapofikia wakati wa kuingia mikataba tukushirikishe, sasa ni lini mkataba tutauleta nadhani bado sana kuzungumza jambo hilo akamilishe utafiti, akishaanza uchimbaji akaingia mikataba tutajadiliana, kama kutakuwa na haja ya kuuleta basi tutaona ni utaratibu gani utumike ili Mheshimiwa Mbunge kuweza kuuona mkataba huo.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Mji wa Ruangwa Mkoani Lindi una madini mengi lakini wachimbaji walio wengi wa madini hayo ni wachimbaji wadogo wadogo ambao hawana zana za kisasa za kuchimba madini. Je, Serikali haioni haja ya kuwasaidia kwa kuwapa mikopo ili waweze kununua zana za kisasa za uchimbaji?

Supplementary Question 3

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE: Ahsante Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuniona. Tatizo lililopo Ruangwa halina tofauti na tatizo lililopo Manyoni Magharibi, kwa kuwa sasa kuna Sera ya Madini inayotaka kuwapatia wachimbaji wadogo wadogo wa madini ruzuku.
Je, ni lini sasa Serikali itatoa ruzuku kwa wajasiriamali wachimbaji wa gypsum wa Wilaya ya Itigi ili kuongeza uzalishaji na hata kuanzisha viwanda? (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nikupongeze Mheshimiwa Matembe, Mkoa wa Singida na hasa katika maeneo ya Itigi kuna maeneo mengi sana ambayo kuna madini ya dhahabu na katika maeneo hao kwa mwaka jana tumepatia ruzuku wachimbaji wadogo 32, lakini tunaendelea pia kufanya hivyo.
Mheshimiwa Mbunge kushirikishe tu, tutakapofikia hatua sasa ya kugawa ruzuku nyingine awamu ya tatu ambayo ipo kwenye maandalizi tutakushirikisha na tunatarajia kuanzia mwakani taratibu zikikamilika tutaanza kukamilisha utaratibu mwingine wa kuwapatia ruzuku pamoja na mikopo. (Makofi)

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Mji wa Ruangwa Mkoani Lindi una madini mengi lakini wachimbaji walio wengi wa madini hayo ni wachimbaji wadogo wadogo ambao hawana zana za kisasa za kuchimba madini. Je, Serikali haioni haja ya kuwasaidia kwa kuwapa mikopo ili waweze kununua zana za kisasa za uchimbaji?

Supplementary Question 4

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Ahsante Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Kama ambavyo Naibu Waziri ameitambua Kitowelo kwamba atatenga kwa ajili ya wachimbaji wadogo.
Vilevile eneo hilo liko ndani ya kijiji cha Lilombe, lakini tangu uchimbaji huu mdogo umeanza kijiji kile cha Lilombe hakijawahi kunufaika kwa lolote na Halmashauri nzima ya Liwale haijawahi kunufaika kwa lolote, kwa sababu vibali vya uchimbaji vinatoka Kanda, halafu wale wakitoka kwenye Kanda wanaingia moja kwa moja vijijini wanaanza uchimbaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, nini kauli ya Serikali juu ya manufaa wanayoyapata vile vijiji ambavyo tayari machimbo hayo yapo? (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nakiri jambo ambalo anazungumza na tumezungumza naye kama miezi miwili iliyopita, nikaomba sana nimuagize Mheshimiwa Mkurugenzi wake na Watendaji wa Vijiji ili watumie fursa hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wachimbaji wote nchi nzima, wadogo na wakubwa wanatakiwa kutoa ushuru wa Halmashauri husika, wanatakiwa kuchangia maendeleo ya vijiji ambayo shughuli za uchimbaji zinafanyika. Kwa hiyo, nimuombe sana Mheshimiwa Mbunge ikiwezekana nitakafanya ziara huko tutaita mkutano chini ya Mkurugenzi wako, Watendaji wote wa Serikali ambao shughuli za migodi zinafanyika ili sasa Serikali za Vijiji vianze kunufaika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu ni kwamba kila kijiji ambapo kuna mgodi wa aina yoyote mkubwa na mdogo lazima wachimbaji hao washiriki katika shughuli za maendeleo.