Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:- Je, ni lini Mfumo wa EPICOR, LGMD na ule wa LAWSON iliyopo kwenye halmashauri itaanza kuwasiliana na si kuwa stand alone system kama ilivyo sasa?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali kwa hatua inayochukua katika kusimika mifumo mbalimbali katika Mamlaka za Serikali za Mitaa ili kurahisisha uendeshaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa. Pamoja na pongezi hizo, nampongeza vilevile Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, changamoto kubwa katika utumiaji wa mifumo hii ni upatikanaji wa wataalam wa TEHAMA katika Mamlaka za Serikali zetu za Mitaa. Je, Serikali ina mpango gani wa kuajiri wataalam wa kutosha wa TEHAMA hasa katika halmashauri mpya ambazo zimeanza hivi karibuni kama Nanyamba na Halmashauri ya Mji wa Newala?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ni kwamba kwenye Mfumo wa EPICOR kuna changamoto nyingine ambayo inapatikana hususan wakati wa kutayarisha final account katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kiasi kwamba wataalam hulazimika kutafuta taarifa nyingine nje ya mfumo. Je, Serikali ina mpango gani wa ku--repair changamoto hii ili tunapoandaa hesabu za mwisho kwa Mamlaka zetu za Serikali za Mitaa wataalam wategemee taarifa za kwenye system tu na si kuchukua nyingine kutoka nje?

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Nanyamba, Mwalimu Mstaafu, Mkurugenzi Mstaafu, RAS Mstaafu, mdogo wangu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la kuwaajiri wataalam wa TEHAMA, Wizara ya Utumishi na Utawala Bora tutakuwa tayari kuajiri watumishi hao kulingana na mahitaji. Katika zile nafasi 52,000 ambazo zilipitishwa na Bunge ambazo karibuni tutaanza kuajiri, zipo baadhi ya Halmashauri ambazo zimeweka maombi ya kuajiri wataalam hao. Sasa kila Halmashauri inawahitaji hawa kulingana na mahitaji yake yanahitilafiana.
Naomba nishauri, kwa hiyo, kama mdogo wangu Mheshimiwa Chikota, kule Nanyamba uliweka katika maombi, basi itakapofika kuajiri tutaajiri na kama hawakuwekwa tunashauri Nanyamba na Halmashauri nyingine zote katika bajeti inayokuja kutuwekea maombi hayo mkishirikiana na Wizara mama ya TAMISEMI.
Mheshimiwa Naibu Spika, Swali la pili la Mheshimiwa Chikota linahusu mfumo wa EPICOR ambao unasimamiwa na Wizara ya Fedha. Kwa sababu Kwa muuliza swali anapaswa kupata majibu sahihi ninaomba nimuombe Waziri mwenzangu wa Fedha ajibu suala la EPICOR kwa sababu linasimamiwa na Wizara yake, kwa ruhusa yako.

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Chikota kwa kweli kwa kujali umuhimu wa mifumo hii kuingiliana na kufanya kazi ipasavyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto ambayo anaisema ambayo sasa wataalam wanajikuta wakitegemea taarifa kutoka nje badala ya ndani ya mifumo kimsingi inatokana na madiliko ya teknolojia ambayo tunaenda nayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Chikota atakumbuka kwamba tulianza na platnum wakati ule, tukajikuta kwamba mifumo hii na ina hitilafu tukaamia kwenye EPICOR 7.0; lakini nayo kulikuwa na modules ambazo ni friendly kwa mtumiaji, lakini ikawa na changamoto nyingine tukahama tena tukaenda 7.35 tukaenda 9.05 na sasa tumefika EPICOR 10.20. Kwa hiyo, kwa kweli changamoto anayoisema ni ya kiteknolojia zaidi. Tunatarajia kwamba huu mfumo wa EPICOR 10.2 sasa to zero itajalibu kushughulikia hizi changamoto ambao zinajitokeza katika utumiaji.

Name

Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza:- Je, ni lini Mfumo wa EPICOR, LGMD na ule wa LAWSON iliyopo kwenye halmashauri itaanza kuwasiliana na si kuwa stand alone system kama ilivyo sasa?

Supplementary Question 2

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Kumekuwa na utaratibu wa kutengeneza mifumo yetu nyeti nje ya nchi jambo ambalo linaweza kuhatarisha usiri na usalama wa taarifa zetu.
Je, ni lini Serikali itaona umuhimu wa kutumia wataalam wetu wa ndani ili kuepuka matatizo ambayo yanaweza kujitokeza? Ahsante.

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeunda Wakala wa Serikali Mtandao. Serikali Mtandao iko pale kwa kusimamia mifumo yote inaayoanzishwa ndani ya Serikali na kwamba mifumo yote iliyopo sasa imeanzishwa kwa kuhusishwa Serikali Mtandao. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Kamati ya Bunge inayohusika na masuala ya Utawala na Serikali za Mitaa imependekeza na mimi nawaunga mkono kwamba Wakala wa Serikali Mtandao ibadilishwe iwe mamlaka ili iweze kusimamia mitandao yote na mifumo yote inayoanzishwa ndani ya Serikali.