Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:- Ni muda mrefu tangu transfomer katika Kijiji cha Itengelo, Kata ya Saja imefungwa lakini umeme haujawashwa. Je, ni lini Serikali itawasha umeme katika kijiji hicho?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuweza kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Waziri katika Jimbo la Njombe Mjini kuna vijiji ambavyo vimepitiwa na mradi wa Makambako - Songea na mradi huu haujaingia kwenye vitongoji, haujaingia kwenye zahanati, shule ikiwemo shule ya sekondari ya Anne Makinda; na kwa kuwa mradi huu ni wa muda mrefu sana na vijiji vinaendelea kupanuka.
Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika vijiji hivi vilivyopitiwa na mradi wa Makambako - Songea?
Swali langu la pili, Jimbo la Lupembe lina vijiji 45, kati ya vijiji 45, vijiji 34 havina umeme ikiwemo Kijiji cha Ninga na kwa kuwa wananchi wa Kijiji cha Ninga wameamua kuunga mkono sera ya viwanda kwa kununua mashine ya kusaga yenye uwezo wa kusaga sembe zaidi ya tani 12 kwa siku, kwa nia ya kuanzisha kiwanda.
Je, Serikali itapeleka lini umeme katika vijiji hivi hususani Kijiji cha Ninga ili ndoto yao ya kiwanda chao kiweze kufanya kazi? (Makofi)

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru kwa kunipa fursa ya kujibu maswali mawili ya nyongeza.
Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge Neema pamoja na Wabunge wa Viti Maalum kwa namna ambavyo wanauliza maswali katika sekta yetu ya nishati.
Swali lake la kwanza amerejea kwamba mradi unaoendelea wa ujenzi wa msongo wa KV 220 Makambo - Songea; kwanza awali ya yote nimshukuru Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa kutuwekea jiwe la msingi katika mradi huu. Mradi huu unaendelea vizuri mpaka sasa umefikia asilimia 70, na utaunganisha vijiji 120 katika Mikoa ya Njombe na Ruvuma.
Mheshimiwa Naibu Spika, Katika maeneo ambayo ameyataja Mheshimiwa Mbunge Neema na naomba nimtaarifu mpaka sasa Vijiji vitano katika Mkoa wa Njombe vimeshawasha umeme kupitia mradi huu na kwamba katika maeneo ambayo ameyataja hayajafikiwa na mradi huu, nataka nimwambie tu pia Serikali inaendelea kutekeleza mradi wa densification na kwa mkoa wa Njombe peke yake mpaka sasa hivi vijiji 12 vimeshaunganishwa.
Kwa hiyo nataka nimwambie maeneo ambayo yatakakuwa mradi huo haukuyafikia yatafikiwa na miradi ambayo inaendelea REA Awamu ya Tatu pamoja na densification ambavyo kama nilivyosema na kama ambavyo Serikali imekuwa ikitoa maelekezo, taasisi za umma ikiwemo shule ya sekondari na hapa amerejea sekondari ya Mama Anne Makinda viunganishwe katika miradi hii inayoendelea. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili amekitaja Kijiji cha Ninga, nataka nimthibitishie Mheshimiwa Mbunge kama alivyosema Jimbo la Lupembe lina vijiji 34 kati ya vijiji hivyo, vijiji 24 vipo katika mradi wa REA Awamu ya Tatu pamoja na kijiji ambacho amekitaja, na naomba niwapongeze vijiji vyote ambavyo vinatekeleza sera ya viwanda na kwa kuwa Serikali yetu ya Awamu ya Tano imedhamiria kutekeleza mapinduzi ya viwanda, nishati ya umeme itafika katika Kijiji cha Ninga pamoja na vijiji vingine kwa Awamu ya Tatu ambayo inaendelea. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:- Ni muda mrefu tangu transfomer katika Kijiji cha Itengelo, Kata ya Saja imefungwa lakini umeme haujawashwa. Je, ni lini Serikali itawasha umeme katika kijiji hicho?

Supplementary Question 2

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa uzinduzi wa REA Awamu ya Tatu kimkoa wa Geita ulifanyika kwenye Wilaya ya Nyangh’wale, Kijiji cha Nijundu, mwenzi wa sita mwaka jana, lakini cha ajabu mpaka leo hii hata kijiji kimoja kati ya vijiji 35 vya Wilaya ya Nyangh’wale havijapelekewa nguzo.
Je, ni lini sasa Serikali itaanza kupeleka nguzo hizo katika hivyo vijiji ambavyo tumepewa vijiji 35?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Amar kwa swali lake zuri, katika Mkoa wa Geita mkandarasi wake ni JV White Service Limited ambaye ameshaanza kazi, na kwa kuwa ameeleza kwamba mpaka sasa katika Wilaya yake, nataka niseme wakandarasi hawa walipoteuliwa unakuta Mkoa mmoja una mkandarasi mmoja, na Mkoa huo unaweza ukawa na Wilaya mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa maelekezo ya hivi karibuni katika Mkoa wa Geita mkandarasi alikuwa ameshaagiza nguzo takribani 3,000 na tulimpa maelekezo aende kila Wilaya. Kwa hiyo, kama mkandarasi mpaka sasa hivi hajafika katika Wilaya ya Nyang’wale naomba nimuelekeze na nimpe agizo kwamba kama vile tulivyotoa maelekezo tulivyokutana kikao cha tarehe 13 Januari, wakandarasi wote wafanye miradi Wilaya zote, wasijielekeze katika Wilaya moja.
Kwa hiyo, ninamuagiza mkandarasi JV White wa Mkoa wa Geita aelekee kwenye Wilaya zote na afanye kazi ya kuunganisha kupeleka hii miundombinu ya umeme kama ambavyo tulikubaliana katika Kikao cha tarehe 13 Januari, 2018.

Name

Lucy Simon Magereli

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:- Ni muda mrefu tangu transfomer katika Kijiji cha Itengelo, Kata ya Saja imefungwa lakini umeme haujawashwa. Je, ni lini Serikali itawasha umeme katika kijiji hicho?

Supplementary Question 3

MHE. LUCY S. MAGERELI: Nakushukuru sana Mheshimiwa Naibu Spika, kwa fursa niulize swali la nyongeza.
Changamoto ya umeme kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Kigamboni bado ni kubwa sana pamoja na kwamba mwaka jana wakati wa bajeti, wakati Waziri akijibu swali la Mheshimiwa Dkt. Ndungulile, alieleza bayana ya kwamba tatizo la msongo mdogo wa umeme eneo la Kigamboni litakuwa limekwisha mwaka jana mwezi Agosti, lakini hadi tunapozungumza leo bado changamoto ya umeme mdogo Kigamboni ni kubwa, lakini ukiachilia hilo umeme huo unakatika mara 15 kwa siku.
Je, Serikali ina maelezo gani kuhusu suala hili na kuchelewa kwa kutekelezwa kwa mradi huu wa kufunga transfoma kubwa yenye msongo wa kutosha kutupa huduma ya umeme eneo la Kigamboni?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Lucy kwa swali lake zuri na ni muhimu sana. Kupitia Bunge lako Tukufu, napenda nitoe taarifa ya Serikali kuhusiana na utekelezaji wa miradi ya umeme muhimu sana kwa wananchi wa maeneo ya Kigamboni.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa wananchi wa Kigamboni hivi sasa hawana umeme wa uhakika, lakini hatua madhubuti tunayofanya ni kujenga substation itakayowapelekea umeme sasa wananchi wa Kigamboni wote, mradi huu utakamilika mwezi tarehe 25 Mei tutakuwa tumeshawapelekea wananchi wa Kigamboni.
Mheshimiwa Naibu Spika, hatua ya haraka tunachofanya hivi sasa tunakamilisha utekelezaji wa mradi wa kabambe katika Jiji la Dar es Salaam kwa eneo la Mbagala. Mradi tunategemea kuuwasha kati ya tarehe 20 mwezi huu kuanzia tarehe 12 tutakuwa tumeshawasha na tarehe 20. Mradi huu utahudumia wananchi wa Mbagala, Kurasini, Kigamboni pamoja na maeneo mengine ya Dar es Salaam.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimpe taarifa Mheshimiwa Mbunge, kazi hiyo inafanyika na wananchi wa Kigamboni watarajie kwamba umeme utapatikana kufikia mwisho wa mwezi huu. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:- Ni muda mrefu tangu transfomer katika Kijiji cha Itengelo, Kata ya Saja imefungwa lakini umeme haujawashwa. Je, ni lini Serikali itawasha umeme katika kijiji hicho?

Supplementary Question 4

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, shida iliyoko huko Njombe inafanana sana na iliyoko huko Kigoma. Mkoa wa Kigoma tuna mkandarasi ambaye ana mgogoro, sasa mgogoro huu umeendelea kati ya REA na Wizara ya Ujenzi. Tungependa kujua kwa Wilaya za Kigoma, Buhigwe, Uvinza na Kasulu, mgogoro kati ya mkandarasi na Wizara unamalizika lini ili mradi wa REA Awamu ya Tatu uweze kuanza? Nakushukuru.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mara nyingine tena ninapenda kumshukuru sana Mheshimiwa Nsanzugwanko anavyofatilia masuala ya umeme katika Mkoa wa Kigoma kwa ujumla wake.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa kwa upande wa Mkoa wa Kigoma, Mkandarasi kwa ajili ya kutekeleza mradi wa REA Awamu ya Tatu mchakato umekuwa ukiendelea, lakini nitumie nafasi hii kusema kuwa, kweli wakandarasi walishtakiana, shitaka linaendelea mahakamani na kwa taratibu za Kisheria, jambo linapokuwa mahakamani huwezi kuliingilia kwa sababu ni muhimili mwingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, ninatoa taarifa tu kwamba Serikali imeshaanza kuwapelekea umeme wananchi wa Kigoma, wiki iliyopita tulizindua mradi wa utekelezaji wa umeme vijijini katika Wilaya ya Kibondo na tayari mkandarasi ameshawasha Kijiji cha Mabamba. Lakini katika Jimbo la Kakonko pia tumeshazindua, mkandarasi ameshawasha umeme katika Kijiji cha Katale na ataendelea Nyamtukuza. Niwape taarifa wananchi wa Kigoma kwamba mara baada ya taratibu za kimahakama kukamilika vijiji vyote 120 vilivyobaki vitapelekewa umeme.

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. NEEMA W. MGAYA aliuliza:- Ni muda mrefu tangu transfomer katika Kijiji cha Itengelo, Kata ya Saja imefungwa lakini umeme haujawashwa. Je, ni lini Serikali itawasha umeme katika kijiji hicho?

Supplementary Question 5

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Naibu Spika nakushukuru.
Kumekuwa na tabia ya umeme kukatika katika Mkoa wa Lindi hususan maeneo ya Mchinga, Mvuleni na Kilolambwani kadri mvua inaponyesha, lakini siku mvua haikunyesha umeme huwa haukatiki.
Nataka kujua, kuna changamoto gani kwamba siku za mvua lazima umeme ukatike hata kama hatuoni nguzo iliyodondoka?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali moja zuri sana la Mheshimiwa Mbunge wa Lindi. Ni kweli, kwanza kabisa nitumie nafasi hii kuipongeza sana Serikali yetu, kulikuwa na matatizo makubwa sana ya umeme katika Mkoa wa Mtwara na Lindi miaka na miezi michache iliyopita. Lakini tangu mwezi Desemba, Serikali yetu imetenga fedha na imelipa fedha na tumekarabati mitambo yote iliyokuwa haifanyi kazi katika Jimbo la Mheshimiwa Mbunge na Mikoa ya Mtwara na Lindi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kadhalika ni kweli mvua na umeme ni vitu viwili tofauti sana, mara zote kunapokuwa na mvua hasa ya muungurumo wa radi huwa inaingilia sana miundombinu ya umeme, hata inapokuwa mvua ya upepo mara nyingi nguzo zetu zinaanguka.
Mheshimiwa Naibu Spika, ingawa amesema mara zote kunapokuwa hakuna mvua umeme hauna shida, ili kuondokana na tatizo hilo sasa hivi tunaanza utaratibu wa kuleta nguzo za zege ambazo zitakuwa imara, wakati wa mvua zitakuwa hazidondoki. Kwa hiyo, tatizo hilo litakwisha mara moja, siyo kwa Lindi tu ni kwa nchi nzima.