Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Kumekuwa na sintofahamu ya matumizi ya ardhi pamoja na masharti maalum yanayotakiwa katika mapori yetu hususan kwa wawekezaji na wananchi wanaozunguka hifadhi na mapori tengefu. Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo hili?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUM DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri naomba kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa wananchi, wanaendelea kunyanyasika katika maeneo hayo, je, Serikali ina mpango gani wa kutoa muda maalum kwa kumaliza mgogoro huo wa kitaifa? Ahsante.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo tumekuwa tukitoa majibu kwa muda mrefu kwamba sasa hivi tunayapitia matatizo na changamoto zote zilizopo katika hifadhi zetu, ikiwa nia pamoja na maeneo yale yanayosimamiwa na jumuiya za wananchi, naamini kabisa kwamba baada ya muda mfupi na baada ya Serikali na wadau wengine kukaa kwa pamoja tutaleta ufumbuzi wa suala hili na haya matatizo yatapungua kwa kiwango kikubwa. (Makofi)

Name

Joyce John Mukya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Kumekuwa na sintofahamu ya matumizi ya ardhi pamoja na masharti maalum yanayotakiwa katika mapori yetu hususan kwa wawekezaji na wananchi wanaozunguka hifadhi na mapori tengefu. Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo hili?

Supplementary Question 2

MHE. JOYCE J. MUKYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru. Tatizo hili linafanana kabisa na tatizo la pori tengefu la Loliondo ambalo limedumu kwa kipindi cha miaka 25 sasa au zaidi, tokea nchi hii imepata uhuru ni awamu nne zimepita za uongozi na zote zikiongozwa na Serikali ya CCM. Kila awamu ilikuwa inapeleka uongozi wake kule kwa ajili ya kuongea na wananchi kwa ajili ya mgogoro huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata Waziri Mkuu Mheshimiwa Majaliwa ametoa agizo juzi kwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha aunde Kamati ya kwenda kushughulika na tatizo hili. Amepeleka ripoti na Mheshimiwa Dkt. Kigwangalla amepeleka ripoti lakini mpaka sasa hakuna ambacho kimefanyika;
Naomba kujua je, ripoti hizi, zinasema wananchi wale waendelee kuteseka au ni nini ambacho kiko chini ya carpet ambacho kinasababisha wananchi hawa wasipiwe suluhu, na haki yao kupitia mgogoro huo ambao umeikumba Serikali hii na nchi hii kwa muda mrefu kwa muda wa miaka 25 na zaidi? (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwa muda mrefu kumekuwa na tatizo na mgogoro huko Loliondo na mgogoro huu umedumu kwa miaka mingi. Hivi sasa Serikali kama ulivyosema mwenyewe imechukua hatua za kuunda kamati mbalimbali ikiwemo kamati ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambayo ilileta mapendekezo na mapendekezo hayo yamepitiwa na Serikali, Serikali imefanya uamuzi ambao tumeufikia ni kutaka kuwa na chombo maalumu kitakachosimamia lile pori la Loliondo.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi sasa Serikali inafanya mchakato wa kuanzisha hicho chombo au mamlaka ambayo itahusika na usimamizi wa pori hilo la Loliondo kwa usimamizi na ushirikiano wa wananchi wenyewe wa Loliondo. Hii ndiyo tunaamini kwamba itakuwa suluhu ya tatizo ambalo limedumu kwa muda mrefu katika lile eneo. Kwa hiyo, ni hivi karibuni tu tutaleta huo mwongozo na tutaleta hiyo mamlaka au tutaleta chombo hicho ambacho kitakwenda kusimamia tatizo hilo la Loliondo.

Name

Dr. Pudenciana Wilfred Kikwembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Kumekuwa na sintofahamu ya matumizi ya ardhi pamoja na masharti maalum yanayotakiwa katika mapori yetu hususan kwa wawekezaji na wananchi wanaozunguka hifadhi na mapori tengefu. Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo hili?

Supplementary Question 3

MHE.DKT. PUDENCIANA W. KIKWEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipatia nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Waziri ameongea kuhusu maeneo ya hifadhi ambayo yamekuwa yakihifadhiwa na Serikali lakini pia vyanzo vya maji. Kwa kuwa, wananchi wangu kwa kupitia Halmashauri ya Mpimbwe, Jimbo la Kavuu, wananchi wangu wa Kata ya Itobanilo; vijiji vya Senta Unyenye, Amani na Lunguya wamekuwa wakitumia maji ya Mto Kavuu ambao unapakana na mbuga ya Katavi na askari wa Katavi wamekuwa wakiwanyanyasa wananchi wakati vijiji hivyo hawana maji na tumekuwa na ujirani mwema wa kutumia.
Je, Serikali inasema nini kuhusu hawa watu wa National Park kupiga wananchi hovyo wakiwa wanaenda kutafuta huduma za msingi?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli wananchi wa kata hizo alizozitaja pamoja na hivyo vijiji vimekuwa vikitegemea sana maji ya eneo lile ambalo amelisema karibu na mbuga yetu ile ya Katavi.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Sheria zetu za Wanyamapori Sheria Na. 5 ya mwaka 2009 hairuhusu wananchi kuingia katika maeneo ya hifadhi bila kibali. Kwa hiyo, hivi sasa ambacho kinaweza kufanyika ili kunusuru matatizo hayo, kwa sababu tuna sera ile ya ujirani mwema nitaomba tukae na Mheshimiwa Mbunge, tukakae na wananchi wenyewe ili tuweze kuangalia ni namna gani tunawapelekea maji katika maeneo ya vijiji vinavyohusika badala ya kuingia kwenye hifadhi ambapo wanakuwa wanahatarisha maisha yao na pia hali wataharibu hifadhi kitu ambacho ni kinyume na sheria. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge tushirikiane katika kutatua tatizo hili.