Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zainabu Nuhu Mwamwindi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINABU N. MWAMWINDI aliuliza:- Zahanati ya Kalenga iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa haikidhi mahitaji halisi ya wakazi wa vijiji vinavyoizunguka. Je, ni lini Serikali itaboresha zahanati hiyo kwa kujenga vyumba vya ziada na mahitaji mengine ya msingi?

Supplementary Question 1

MHE. ZAINABU N. MWAMWINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninaomba kuuliza swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba Zahanati ya Mangalali imefunguliwa Februari. Zahanati hii ipo katika Kata ya Ulanda na katika vijiji ambavyo bado vinaendelea kupata huduma kutoka kwenye Zahanati ya Kalenga ni Kijiji cha Makongati ambacho kutoka pale Zahanati ya Kalenga pana kilometa karibu 15, lakini pia Zahanati ya Kalenga ipo jirani kabisa na Makumbusho ya Chifu Mkwawa, lakini pia iko karibu kabisa na Barabara Kuu iendayo Hifadhi ya Taifa ya Ruaha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu, kwa kuwa mpango wa Serikali ni kila Kata kuwa na Kituo cha Afya, je, Serikali iko tayari kuunga mkono jitihada za wananchi wa Kalenga walio tayari kutoa eneo lao na sehemu ya nguvu kazi kwa ajili ya kupatiwa Kituo cha Afya? (Makofi). Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jibu langu la msingi nimeelezea jinsi ambavyo hakuna uwezekano wa kuongeza majengo katika Zahanati ya Kalenga kutokana na eneo lile kwamba lina makazi na tayari yameshapimwa kiasi kwamba uwezekano wa kutoa compensation Halmashauri haina uwezo huo.
Mhesimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza niungane na Mbunge kwa kumpongeza kwa jinsi ambavyo anapigania suala la kuhakikisha wananchi wanapata afya iliyo bora, lakini pia na Mbunge wa Jimbo Mheshimiwa Mgimwa kwa jitihada zake. Kwa taarifa nilizopata ni kwamba mpaka sasa hivi ameshachangia mabati 100 na mifuko 80 ya saruji ili kuhakikisha kwamba Kituo cha Afya kinajengwa Kalenga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba Vituo vya Afya vingi vinajengwa ili kupunguza msongamano ambao unajitokeza katika
Hospitali ya Mkoa wa Iringa kwani kutoka Kalenga kwenda Iringa ni kilometa 15 na pale kuna lami kiasi kwamba wananchi wana option ya kwenda hata kule, lakini lengo ni kuhakikisha kwamba wanapata huduma kwa urahisi zaidi.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. ZAINABU N. MWAMWINDI aliuliza:- Zahanati ya Kalenga iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa haikidhi mahitaji halisi ya wakazi wa vijiji vinavyoizunguka. Je, ni lini Serikali itaboresha zahanati hiyo kwa kujenga vyumba vya ziada na mahitaji mengine ya msingi?

Supplementary Question 2

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Lushoto lina Kituo cha Afya kimoja tu, lakini kwa juhudi za wananchi wamejitahidi kujenga Vituo vya Afya viwili, ambapo kituo cha kwanza kipo Ngwelo, Kituo cha pili kipo Gare. Je, nini kauli ya Serikali juu ya kumalizia vituo vile vya afya ili wananchi waweze kupata huduma wasiende mbali kufuata huduma za afya?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake Mheshimiwa Shekilindi anasema tayari wameshajenga Vituo vya Afya viwili, lakini kwa bahati mbaya hajafafanua vimejengwa to what extent? Kama vimekamilika au la! Maana kama vimekamilika, kinachotakiwa ni kuhakikisha kwamba huduma inapatikana kwa kupeleka Waganga pamoja na Wauguzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ni dhamira ya Serikali kuhakikisha kwamba Vituo vya Afya vyote vinakamilika na viweze kutoa huduma ambayo tunakusudia na hasa upasuaji wa dharura kwa akina mama na watoto. Kwa hiyo, naamini baada ya kujua status ya hivyo Vituo vya Afya ambavyo vimejengwa kwake, Serikali iko tayari kuhakikisha kwamba inachangia ili huduma hiyo ambayo tumeikusudia, iweze kutolewa.

Name

Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINABU N. MWAMWINDI aliuliza:- Zahanati ya Kalenga iliyopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Iringa haikidhi mahitaji halisi ya wakazi wa vijiji vinavyoizunguka. Je, ni lini Serikali itaboresha zahanati hiyo kwa kujenga vyumba vya ziada na mahitaji mengine ya msingi?

Supplementary Question 3

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pale Chalinze Wilayani Mdaula, kuna zahanati ambayo wananchi kwa nguvu zao wamekuwa wanaijenga tangu mwaka 2012. Wamejenga, wameweka plasta, wameweka madirisha, lakini bado wanasuasua kwa sababu uchumi siyo mzuri. Sasa swali langu kwa Serikali, ni lini sasa Serikali itaongeza nguvu ya Serikali kuwasaidia wananchi ile zahanati imalizike kusudi wananchi waweze kupata mahali pa kwenda kupata tiba? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Naibu Waziri wangu kwa ufafanuzi mzuri wa maswali yote ya awali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tunafahamu Mdaula na maeneo mengine kuna changamoto, wananchi wamefanya juhudi kubwa na ndiyo maana azma ya Serikali yetu ni kuhakikisha kwamba tunaunga mkono juhudi za wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hilo, sasa hivi tunafanya uwezeshaji wa kuangalia jinsi gani tutafanya kuhakikisha maboma yote yaliyojengwa katika Halmashauri zetu tunayakamilisha. Tutatumia takribani shilingi bilioni 69 ambapo jambo hili maeneo ya Mdaula pale, hasa Halmashauri ya Chalinze tutawaelekeza wahakikishe katika umaliziaji wa maboma hayo, ile Zahanati ya Mdaula iweze kutengewa fedha katika hizo fedha ambazo tutazitoa kuhakikisha kwamba wananchi wa eneo lile wanapata huduma za afya, kama azma ya Serikali ilivyokusudia.