Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza:- Mji wa Kibaha ni Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani na yapo maombi yaliyokwishapelekwa Serikalini kuomba Mji huo upewe hadhi ya kuwa Manispaa lakini hakuna majibu kwa ombi hilo hadi sasa:- Je, ni kwa nini mpaka sasa Serikali haijaupa hadhi Mji huo kuwa Manispaa?

Supplementary Question 1

MHE. SILVESTRY F. KOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu ya Serikali lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Ikumbukwe kuwa Mji huo wa Kibaha ndio Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani wenye Wilaya sita na yenye idadi ya watu zaidi ya 1,100,000, Mji huu wa Kibaha umekuwa unaongoza katika ujenzi wa viwanda ukiwa na viwanda vikubwa sita, vya kati 16, vidogo 78, vinavyoendelezwa kujengwa vitatu na ambavyo vipo katika taratibu za ujenzi kwenye makaratasi 20.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa tukipata kikwazo kikubwa hasa kwa wawekezaji hasa wanapotaka kuendeleza viwanda wanapobaini kwamba huu ni mji tu na wala hauna hadhi ya Manispaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu hiyo basi na tukizingatia kwamba Sera Kuu ya Serikali yetu ya Awamu ya Tano kwenda katika uchumi wa kati ni viwanda na inatekelezwa vizuri na kipekee na kwa kuongoza kwa mji wa kibaha, ni kwa nini sasa Serikali isitoe upendeleo wa pekee na kuupatia mji huu hadhi ya manispaa ili tuweze kwenda kwa kasi kulingana na sera ya Serikali?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wananchi wa Kibaha kwa utiifu na unyenyekevu kabisa wanaomba ombi lao hili lipewe uzito wa kipekee. Ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kwanza nimsifu Mheshimiwa Silvestry Koka, Mbunge wa Kibaha Mjini kwa jinsi anavyopangilia hoja zake kwa niaba ya wananchi wa Kibaha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa vigezo vilivyowekwa na mwongozo wa Serikali wa mwaka 2014 bado tunahimiza kwamba Halmashauri ya Mji wa Kibaha ifanye kila linalowezekana ili kuweza kutimiza vigezo hivi nilivyovitaja mwanzoni kwenye jibu la msingi ili waweze kufikia hadhi ya kupandishwa kuwa Manispaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo sisi kwa kweli tunaungana nao wakazi wa Kibaha. Ni mji wa muda mrefu na sisi tunashangaa kwa nini hawajaweza kuwavutia watu wengi waongezeke kwenye Mji. Hii idadi ya watu wote waliotaja inafanana na idadi ya wakazi wa Mkoa mzima wa Pwani. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka 2012, Mji wenyewe wa kibaha ambao ndio uko kwenye Halmashauri ya Mji wa Kibaha ulikuwa na wakazi 128,488, hizo ndizo taarifa tulizonazo. Kwa hiyo pamoja na kutilia uzito ombi lake bado tunahimiza kwamba Mji wa Kibaha wajitahidi kutimiza vigezo vilivyowekwa. Ahsante sana.

Name

Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza:- Mji wa Kibaha ni Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani na yapo maombi yaliyokwishapelekwa Serikalini kuomba Mji huo upewe hadhi ya kuwa Manispaa lakini hakuna majibu kwa ombi hilo hadi sasa:- Je, ni kwa nini mpaka sasa Serikali haijaupa hadhi Mji huo kuwa Manispaa?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii. Naomba kuuliza swali moja la nyongeza. Bagamoyo imepata hadhi ya Mamlaka ya Mji Mdogo mwaka 2005 na miaka 10 baadaye mwaka 2015 baada ya kujitathimini na kuona tumetimiza vigezo tumeomba kupandishwa hadhi kuwa Halmashauri ya Mji. Je, Serikali inatupa jibu gani kuhusu Bagamoyo kupandishwa kuwa Halmashauri ya Mji wa Bagamoyo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba tulipokea maombi ya Mji wa Bagamoyo kupandishwa hadhi kuwa Halmashauri ya Mji sawa sawa na ambavyo tumepokea maombi mengi ya aina hiyo. Kwa sababu kupandisha hadhi Mji kuwa Halmashauri ya Mji kunaweza kusababisha ongezeko la mahitaji mengi ya kiutawala, bado maombi hayo yako kwenye mchakato na tutayafikiria muda utakapofika na kuzingatia na uwezo wa Serikali.

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza:- Mji wa Kibaha ni Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani na yapo maombi yaliyokwishapelekwa Serikalini kuomba Mji huo upewe hadhi ya kuwa Manispaa lakini hakuna majibu kwa ombi hilo hadi sasa:- Je, ni kwa nini mpaka sasa Serikali haijaupa hadhi Mji huo kuwa Manispaa?

Supplementary Question 3

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja. Ningependa kujua Wilaya ya Nyangh’wale Makao yake Makuu ni Karumwa, lakini nikiuliza kila mara hapa kuhusu GN ya Makao Makuu ya Wilaya Nyangh’wale ambayo ni Karumwa, leo hili swali ni mara ya tano, kila nikiuliza naambiwa GN iko tayari lakini cha ajabu mpaka leo hatujakabidhiwa katika Halmashauri yetu ya Nyangh’wale. Je, GN hiyo tutakabidhiwa lini?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Naomba uniruhusu nitoke na Mheshimiwa Amar mara baada ya kipindi hiki twende kwenye Idara yetu ya Sheria ili tuweze kumpatia majibu sahihi.