Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI aliuliza:- Wilaya ya Namtumbo haina huduma stahiki za Hospitali ya Wilaya wala Vituo vya Afya licha ya kuwepo kwa Sera ya kila Wilaya iwe na Hospitali ya Wilaya na kila Kata iwe na Kituo cha Afya. (a) Je, sera hiyo kwa Wilaya ya Namtumbo itatekelezwa lini? (b) Makadirio yaliyofanywa na TBA kwa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Namtumbo ni shilingi bilioni19. Je, Serikali ipo tayari kutenga na kutoa kiasi hicho katika bajeti ya mwaka 2018/2019? (c) Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa vitendea kazi na wataalam katika Vituo vya Afya vitano vilivyopo Namtumbo ili viweze kutoa huduma bora za afya?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI: Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijauliza swali la nyongeza, naomba kuchukua fursa hii kukushukuru sana wewe kwa ushiriki wako mkubwa kutafuta fedha za kujenga Hospitali ya Wilaya ya Namtumbo kupitia Selous Marathon na hivi karibuni tutakuwa na chakula cha jioni kule Dar es Salaam, nakushukuru sana. Wananchi wa Namtumbo wataenzi sana kazi hiyo unayoifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, nina maswali madogo mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, hivi Serikali hususani Wizara ya Fedha kwa kushirikiana na TAMISEMI haioni umuhimu wa kuongeza bajeti ya kuendeleza ujenzi wa jengo la upasuaji kutoka milioni 100 zilizotajwa kwa mwaka ujao wa fedha hadi walau bilioni moja ili kweli ujenzi ufanyike?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kwa kuwa aliyekuwa Naibu Waziri wa Afya Mheshimiwa Dkt. Hamisi Kigwangalla alishafika Lusewa, Makao Makuu ya Mji Mdogo wa Sasawala na kujionea umbali ulivyo kutoka pale Lusewa hadi maeneo ambayo yanaweza yakapatikana huduma za upasuaji na hivyo akajionea kabisa hatari ambayo akina mama wajawazito wanaipata.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivi Waziri wa TAMISEMI atatusaidiaje kuteleleza ahadi ambayo Naibu Waziri huyo aliitoa ya kuhakikisha Kituo hiki cha Afya cha Lusewa kinakamilika na kuanza kutoa huduma ndani ya mwezi mmoja wakati akijua kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo haina fedha kabisa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Ngonyani kwa kazi kubwa anayofanya ya kuwalilia wananchi wake. Bahati nzuri mimi nimeweza kufika kule Namtumbo na Naibu Waziri wakati huo sasa hivi Waziri wa Maliasili, ni kweli changamoto ni kubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nichukue hoja ya Mheshimiwa Mbunge kwa ujumla wake na ndiyo maana kutokana na changamoto ya eneo hili ukiachia kile Kituo cha Afya cha Namtumbo tulichopeleka takribani shilingi milioni 400 mwezi Desemba na kazi tume-target mpaka tarehe 30 Aprili, zote ziwe zimekamilika lakini tumeanza juhudi tena kubwa zingine kuhakikisha tunaongeza vituo vya upasuaji katika Kituo cha Afya cha Msindo na Mkongo ambapo tunaenda kuweka thearter maalum kwa ajili ya upasuaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali tumesikia kilio chake, tutafanya kila liwezekanalo na timu yangu hapa chini ya Naibu Mawaziri wangu kuhakikisha kwamba mambo haya yanaenda kwa kasi na ndiyo maana kutokana na jiografia ya Wilaya ile jinsi ilivyo leo hii tuna zoezi tena la vituo vya afya viwili. Ahsante.

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI aliuliza:- Wilaya ya Namtumbo haina huduma stahiki za Hospitali ya Wilaya wala Vituo vya Afya licha ya kuwepo kwa Sera ya kila Wilaya iwe na Hospitali ya Wilaya na kila Kata iwe na Kituo cha Afya. (a) Je, sera hiyo kwa Wilaya ya Namtumbo itatekelezwa lini? (b) Makadirio yaliyofanywa na TBA kwa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Namtumbo ni shilingi bilioni19. Je, Serikali ipo tayari kutenga na kutoa kiasi hicho katika bajeti ya mwaka 2018/2019? (c) Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa vitendea kazi na wataalam katika Vituo vya Afya vitano vilivyopo Namtumbo ili viweze kutoa huduma bora za afya?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza awali ya yote sina budi kushukuru kwamba hali ya ulinzi Kibiti inazidi kuimarika. Kwa hiyo, tuna kila sababu ya kumshukuru Rais wetu, kipenzi chetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Afya cha Kibiti sasa kinazidiwa, je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka fedha ili kuwa Hospitali ya Wilaya ya Kibiti? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni ukweli usiopingika kwamba hospitali inazidiwa na tafsiri yake nini ambacho kinatakiwa kufanyika? Ni kwamba tuna kila sababu ya kuhakikisha kwamba tunajenga vituo vya afya vingi ili Hospitali ya Wilaya hiyo iwe na sehemu ya kupumulia.
Mheshimiwa Naibu Spika, rai yangu Mheshimiwa Mbunge awahimize wananchi wake waonyeshe nia ya kuanza ujenzi na Serikali itapeleka mkono pale ambapo tayari wananchi washaanza ujenzi.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI aliuliza:- Wilaya ya Namtumbo haina huduma stahiki za Hospitali ya Wilaya wala Vituo vya Afya licha ya kuwepo kwa Sera ya kila Wilaya iwe na Hospitali ya Wilaya na kila Kata iwe na Kituo cha Afya. (a) Je, sera hiyo kwa Wilaya ya Namtumbo itatekelezwa lini? (b) Makadirio yaliyofanywa na TBA kwa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Namtumbo ni shilingi bilioni19. Je, Serikali ipo tayari kutenga na kutoa kiasi hicho katika bajeti ya mwaka 2018/2019? (c) Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa vitendea kazi na wataalam katika Vituo vya Afya vitano vilivyopo Namtumbo ili viweze kutoa huduma bora za afya?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na mimi napenda niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Jimbo la Bunda Mjini na Halmashauri ya Mji ya Bunda Mjini wanataka Hospitali ya Manyamanyama iwe Hospitali ya Wilaya na tayari vikao vya Halmashauri vilishakaa. Tatizo hawana jengo la mortuary na tayari kupitia wadau wameshaanza ujenzi. Je, Serikali haioni kwamba inapaswa kuisaidia Halmashauri ya Mji wa Bunda na hasa ukizingatia Halmashauri ile ni changa kumaliza jengo lile ili sasa ile dhamira ya Hospitali ya Manyamanyama kuwa hospitali ya Wilaya ifanikiwe?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, nilipata manufaa na faida ya kwenda kutembelea Halmashauri ya Bunda nikiwa na ziara ya Mheshimiwa Waziri Mkuu na kwa bahati mbaya Mheshimiwa Mbunge hakuwepo, angekuwepo tungeenda Manyamanyama tukapata fursa ya kujua nini hasa ambacho kinatakiwa kifanywe ili tuweze kushirikiana. Naomba kwa wakati mwingine tuungane tuone namna nzuri ya kuweza kusaidia ili wananchi waweze kupata huduma.

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. ENG. EDWIN A. NGONYANI aliuliza:- Wilaya ya Namtumbo haina huduma stahiki za Hospitali ya Wilaya wala Vituo vya Afya licha ya kuwepo kwa Sera ya kila Wilaya iwe na Hospitali ya Wilaya na kila Kata iwe na Kituo cha Afya. (a) Je, sera hiyo kwa Wilaya ya Namtumbo itatekelezwa lini? (b) Makadirio yaliyofanywa na TBA kwa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Namtumbo ni shilingi bilioni19. Je, Serikali ipo tayari kutenga na kutoa kiasi hicho katika bajeti ya mwaka 2018/2019? (c) Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa vitendea kazi na wataalam katika Vituo vya Afya vitano vilivyopo Namtumbo ili viweze kutoa huduma bora za afya?

Supplementary Question 4

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Mkoa wa Morogoro wenye Wilaya saba na Halmashauri tisa ina Hospitali za Wilaya mbili tu ambazo ni Ulanga na Kilosa. Kwa kuwa katika bajeti ya mwaka huu, Serikali imetenga shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Wilaya ya Morogoro hususani katika Halmashauri ya Morogoro Vijijini katika Kata ya Mvuha.
Je, ni lini Serikali italeta hizi shilingi milioni 500 ili tuanze ujenzi wa Hospitali ya Wilaya katika Halmashauri ya Mvuha?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Naibu Waziri, napenda kujibu swali hili la Mheshimiwa Omary Mgumba, ni kweli na mimi nilipata fursa ya kufika Mvuha nikiwa na Mbunge mwenyewe jiografia na hali ya pale tunatakiwa tufanye kila liwezekanalo kuhakikisha tunaimarisha huduma ya afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wengine wote ni jukumu la Serikali kuhakikisha kwamba tunaboresha sekta ya afya ndiyo maana leo hii tunaboresha vituo vya afya 212 kwa awamu ya kwanza kihistoria.
Mheshimiwa Mgumba naomba nikuambie, nilifika pale na tumebaini changamoto na Serikali hii ya Chama cha Mapinduzi itafanya kila liwezekenalo kuwasaidia wananchi wa Morogoro Vijijini na wananchi wengine katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, rai yangu moja kubwa ni kwamba tunafanya ujenzi wa vituo vya afya 212 then vituo vya afya vingine 70 vipya vitakuja, niwaombe Waheshimiwa Wabunge tushirikiane kusimamia matumizi mazuri ya fedha, lengo kubwa ni kwamba ikifika tarehe 30 Aprili, tuwe tume- launch vituo vya afya visivyopungua 212 katika historia ya nchi yetu hii.