Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA aliuliza:- Mkoa wa Tabora umepata usafiri wa uhakika wa ndege ya ATCL na kwa kuwa Tabora ina historia mbalimbali na kumbukumbu za mambo ya kale. Je, Serikali ipo tayari kuutangaza Mkoa wa Tabora kwa utalii?

Supplementary Question 1

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwanza namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ambayo yamekidhi lakini naomba niongeze kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Mkoa wa Tabora una historia nyingi sana ukizingatia pia na historia ya Baba wa Taifa, lakini wakati anajibu majibu yake Baba wa Taifa hakuwepo, hawakuongeza, kwa hiyo, niombe Wizara ya utalii iongeze kuitangaza historia ya Baba wa Taifa.
Lakini lingine kuna historia ya miembe ambayo ina umri wa miaka 100 nayo ipo kwenye njia ya watumwa. Kwa hiyo niombe niulize maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Kwa kuwa hivi sasa njia ya utmwa inatambulika, je, Serikali iko tayari kuikarabati ile njia kutoka Tabora hadi Kigoma - Ujiji ili iwarahisishie watalii kupita?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lingine, je, Serikali iko tayari kuwatuma wataalam kuhakikisha vivutio vyote ambavyo vipo katika Mkoa wa Tabora vinaorodheshwa? Ukilinganisha na mapato yaliyopatikana tangu 2013 mpaka 2017 ni milioni mbili, milioni mbili kuna nini? Kwa hiyo nasema kwa uchungu kwamba bado tunahitaji utangazaji wa utalii kwa Mkoa wa Tabora ni muhimu sana naomba izingatiwe, ahsante.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kukarabati hii njia ambayo inatoka Tabora hadi Kigoma hili tutalifanyia kazi, tutaangalia kadri upatikanaji wa fedha utakavyokuwepo katika bajeti zetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili, kuhusu kuorodhesha vituo, ni kweli kabisa Tabora ina historia ndefu sana ikiwa ni pamoja na hiyo aliyoisema ambapo Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliweza kusoma katika Mkoa ule na mambo mengine mengi na mimi mwenyewe nimefika katika yale maeneo, nimetembelea na nimeyaona. Kwa hiyo orodha tuliyonayo ni kubwa na tutaendelea kuifanyia kazi, kuiuhisha ili tuweze kuongeza mapato yatokanayo na utalii katika Mkoa huu wa Tabora.

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA aliuliza:- Mkoa wa Tabora umepata usafiri wa uhakika wa ndege ya ATCL na kwa kuwa Tabora ina historia mbalimbali na kumbukumbu za mambo ya kale. Je, Serikali ipo tayari kuutangaza Mkoa wa Tabora kwa utalii?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu ina vivutio vingi sana vya utalii ukiacha mbuga zetu na mlima na kadhalika, wazee wetu wa zamani, machifu wana vitu vyao ambavyo walikuwa wanatumia. Tuna ngoma zetu na vitu hivi vinaaza kupotea. Sasa Wizara hii ya Maliasili na Utalii ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba vivutio kama hivi, miji yetu kama Mji wa Kilwa vinahifadhiwa kwa ajili ya vizazi vinavyokuja?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nchi yetu na ina vitu vingi ambavyo ni vivutio vya utalii. Ni azma ya Wizara yetu kuhakikisha kwamba hivi vyote vinahifadhiwa ili viweze kutumika na vizazi vijavyo viweze kuvielewa na viweze kufaidika na matunda ya hivyo vitu vyote. Kwa hiyo ni azma ya Wizara yetu, itaendelea kulishughulikia, kuvilinda na kuvihifadhi.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. MWANNE I. MCHEMBA aliuliza:- Mkoa wa Tabora umepata usafiri wa uhakika wa ndege ya ATCL na kwa kuwa Tabora ina historia mbalimbali na kumbukumbu za mambo ya kale. Je, Serikali ipo tayari kuutangaza Mkoa wa Tabora kwa utalii?

Supplementary Question 3

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nukipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Mkoa wa Tabora una vivutio vingi vya utalii ukiwemo uwandaji. Ni lini Serikali itafanya uhakiki wa vitalu vya uwindaji vilivypo Tabora? Kwa sababu kuna taarifa kwamba vitalu vya uwaindaji vilivyopo vinasomeka ni vichache kuliko uhalisia wa vitalu vilivyopo?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kuna vitalu viko vingi katika nchi yetu na kazi yetu kubwa ambayo tunaifanya sasa hivi, tunapitia upya vitalu vyote ili tuweze kuvibaini na kuona vipi vinafaa na vipi havifai. Kwa hiyo badaa ya kukamilisha hilo zoezi ni wazi kabisa Mheshimiwa Mbunge atafahamu ni vitalu vingapi ambavyo vinapatikana katika Mkoa wa Tabora.