Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Sekta binafsi ya ulinzi ilianzishwa mwaka 1980 ikiwa na kampuni mbili tu na ikiwa haina miongozo yoyote. • Kwa kuwa sasa sekta hii ina kampuni zaidi ya 850 nchini kote, je, Serikali italeta Sheria ya Sekta Binafsi ya Ulinzi ili pia kuanzisha mamlaka ya sekta binafsi ya ulinzi? • Je, Ofisi ya Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) ina mpango gani wa kushirikiana na Chama cha Sekta Binafsi ya Ulinzi ili kuimarisha ulinzi wa raia na mali zao?

Supplementary Question 1

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kuniruhusu niulize maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Waziri, mimi nasikitika sana Serikali haisemi kwamba mimi ndiye niliyeleta Muswada Binafsi wa Sekta ya Ulinzi Binafsi (Private Security Industry Bill) wa mwaka 2016.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa je, Serikali iko tayari kunilipia kunirudishia gharama hata nusu ya ghalama niliyoitumia katika utafiti huo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, na la pili, kwa kuwa mchakato wa kuipata sheria hii ya sekta ya ulinzi binafsi unakuwa mrefu sana, je, Serikali sasa iko tayari kutunga GN ambayo itatumika wakati huu wa mpito kwa sababu makampuni haya yalianzishwa bila GN wala sheria yoyote?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI):
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikianza na swali lake la kwanza, awali napenda kuchukua furusa hii kumshukuru sana Mheshimiwa Maige kwa mchango mkubwa sana ambao amekuwa akiutoa katika sekta binafsi ya ulunzi na hivyo kama Serikali tunathamini sana mchango wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya Mheshimiwa Maige kuwasilisha muswada wake binafsi hapa Bungeni majibu ya Serikali yalikuwa kwamba Serikali itafanya kazi hiyo, kwa maana ya kuleta muswada huo ili ujadiliwe mbele ya Bunge na sheria hii iweze kutungwa.
Kwa hiyo, nimuombe tu Mheshimiwa Maige kwamba ile kazi kubwa aliyoifanya aichukulie kama ni sehemu ya mchango wake kwa Taifa hili; na yeye kama akiwa mzalendo namba moja basi aone kama ni mchango wake katika kusaidia Serikali katika kukamilisha utungwaji wa sheria hii. Ninafahamu sana kwamba Mheshimiwa huyu ni mzalendo, itakuwa ni sehemu ya mchango wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili, la juu ya GN, katika majibu yangu ya msingi nimesma taratibu za utungwaji wa sheria zinaelekea kukamilika na hivyo namshauri Mheshimiwa Mbunge kwa sababu tumeshapitia kote huko, hatua hii ilibaki atupe nafasi Serikali kuwasilishwa muswada huu ili sheria hii itungwe na baadaye zitakuja hizo GN zingine kwa ajili ya ku-regulate maswala ya ulinzi katika sekta binafsi.

Name

Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Sekta binafsi ya ulinzi ilianzishwa mwaka 1980 ikiwa na kampuni mbili tu na ikiwa haina miongozo yoyote. • Kwa kuwa sasa sekta hii ina kampuni zaidi ya 850 nchini kote, je, Serikali italeta Sheria ya Sekta Binafsi ya Ulinzi ili pia kuanzisha mamlaka ya sekta binafsi ya ulinzi? • Je, Ofisi ya Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) ina mpango gani wa kushirikiana na Chama cha Sekta Binafsi ya Ulinzi ili kuimarisha ulinzi wa raia na mali zao?

Supplementary Question 2

MHE. RUTH. H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu Serikali ndiye msimamizi mkubwa wa usalama wa raia na mali zao, ningepa kufahamu ni kwa jinsi gani Serikali inasimamia kwa uhakika hizi sekta binafsi za ulinzi ili kuhakikisha wale wote walioajiriwa hawana historia ya uhalifu?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI):
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia taasisi zake mbalimbali imekuwa ikihakikisha kwamba kuanzia katika eneo la usajili wa makampuni haya ambayo pamoja na kwamba utaratibu wa usajili wake ni kupitia BRELA, lakini bado Jeshi la Polisi nalo lina nafasi ya kuweza kupitia na kuyatathimini maombi ambayo yanapekwa ili kujihakikishia. Kwa sababu kazi ambayo inakwenda kufanywa hapa na sekta ya ulinzi binafsi ni kazi ambayo vilevile ni ya kulisaidia Jeshi la Polisi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hii ni kwa sababu kwa mujibu wa viwango vya Umoja wa Mataifa askari mmoja anapaswa kulinda watu na 450, lakini sisi kwetu askari mmoja analinda kuanzia watu 1,150 mpaka 1,300. Kwa hiyo, ndiyo maaan kama Serikali tunatoa kipaumbele na ndiyo maana katika shughuli mbalimbali za sekta ya ulinzi binfsi tunahakikisha kwamba tunashirikiana nao katika kutoa elimu, lakini vilevile na kuzisimamia kuona kwamba zinayanya kazi ile iliyokusudiwa ili hatimaye isije ikaleta madhara makubwa kwa sababu na yenyewe pia ni sehemu ya ulinzi katika nchi yetu.

Name

Ester Alexander Mahawe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Sekta binafsi ya ulinzi ilianzishwa mwaka 1980 ikiwa na kampuni mbili tu na ikiwa haina miongozo yoyote. • Kwa kuwa sasa sekta hii ina kampuni zaidi ya 850 nchini kote, je, Serikali italeta Sheria ya Sekta Binafsi ya Ulinzi ili pia kuanzisha mamlaka ya sekta binafsi ya ulinzi? • Je, Ofisi ya Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) ina mpango gani wa kushirikiana na Chama cha Sekta Binafsi ya Ulinzi ili kuimarisha ulinzi wa raia na mali zao?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. MAHAWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Swali langu lilikuwa kuhusu ukosefu wa nyumba za polisi katika Mkoa wa Manyara ikiwemo Ofisi ya RPC. Ni lini sasa Serikali itaona kwamba kuna umuhimu wa Jeshi la Polisi kupatiwa nyumba ili waweze kufanya kazi yao kwa ufanisi.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI):
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tunatambua kwamba tunayo changamoto kubwa sana ya ukosefu wa nyumba za askari wetu, lakini katika mipango ya Wizara tumejiwekea utaratibu kwamba pindi pale bajeti itakaporuhusu tutahakikisha kwamba tunaifikia Mikoa yote ili kuwaondolea adha ya ukosefu wa nyumba watumishi wa Serikali hasa wa Jeshi la Polisi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuondolee hofu Mheshimiwa Mbunge bajeti ikikaa vizuri basi tutafikia katika maeneo yote katika kuondoa hadha hii.

Name

Bhagwanji Maganlal Meisuria

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chwaka

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Sekta binafsi ya ulinzi ilianzishwa mwaka 1980 ikiwa na kampuni mbili tu na ikiwa haina miongozo yoyote. • Kwa kuwa sasa sekta hii ina kampuni zaidi ya 850 nchini kote, je, Serikali italeta Sheria ya Sekta Binafsi ya Ulinzi ili pia kuanzisha mamlaka ya sekta binafsi ya ulinzi? • Je, Ofisi ya Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) ina mpango gani wa kushirikiana na Chama cha Sekta Binafsi ya Ulinzi ili kuimarisha ulinzi wa raia na mali zao?

Supplementary Question 4

MHE. BHAGWANJI MAGANLAL MEISURIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kinipa nasafi hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nazipongeza Serikali ya Zanzibar na Serikali ya Muungano kwa sababu katika Jimbo langu wamejenga kituo cha polisi Chwaka na Jozani. Lakini mimi naomba Serikali, wameniomba nizungumze Serikali ya Muungano pamoja na Zanzibar wapatiwe gari za doria, Chwaka na Jozani.
La kwanza kwa kuboresha wananchi wangu wapate hitaji lao, lakini lingine mimi mwenyewe binafsi nimetoa gari mbili hospitali za Chwaka na Kongoroni. Lakini hii gari ya polisi lazima tuhudumie tupate na mimi nimesaidia Jozani polisi walikuwa wanahitaji computer na nimewasaidia, lakini hii gari mnipatie zote mbili. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI):
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Bhagwanji hakuuliza swali, ilikuwa ni ombi la gari la doria na mimi tu kwa niaba ya Serikali tumepokea ombi lake na tutalifanyia kazi pindi pale nafasi itakaporuhusu basi tutaona namna ya kuweza kufanya.