Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Kufuatia utoaji wa elimu ya msingi bure, shule za msingi na sekondari ndani ya Halmashauri ya Mji wa Tarime zimekuwa na upungufu mkubwa wa madarasa na madawati hadi kufikia walimu kulazimika kufundishia chini ya mti na wanafunzi walio madarasani wanakaa kwenye sakafu kwa idadi kubwa kinyume na matakwa ya Sera ya Elimu. Je, ni nini mpango wa Serikali wa kuhakikisha shule hizo ndani ya Halmashauri ya Mji wa Tarime zinaondokana na changamoto za miundombinu ya kufundishia na kujifunzia ili kutoa elimu bora?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kufuatia majibu ya Mheshimiwa Waziri, ni dhahiri kabisa imeonyesha ni jinsi gani miundombinu ya kujifunzia na kujifunza katika Halmashauri ya Mji wa Tarime hairidhishi na inapelekea matokeo mabaya kwa ufaulu wa wanafunzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa wananchi wa Tarime wameitikia sana wakishirikiana na wadau mbalimbali ikiwepo mimi mwenyewe Mbunge. Tumejenga madarasa mengi lakini mengi yamekaa bila kuezekwa na kwa kuwa kuna Shule ya Msingi Mtulu ambayo imejengwa na wananchi kwa kujitolea madarasa sita pamoja na ofisi lakini Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji amezuia ile shule wananchi wasiendelee kujenga kwa kile anachokiita kwamba ni mgogoro wa ardhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa sasa kupitia Wizara hii ambayo ipo chini ya Ofisi ya Rais na Rais ana mamlaka ya kubadilisha matumizi ya ardhi, wawatie moyo wananchi wale waliojenga yale madarasa ili sasa waweze kuamuru ile shule iendelezwe ili kupunguza adha ya upungufu wa madarasa katika Halmashauri ya Mji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika Halmashauri ya Mji kuna shule moja ambayo inatumiwa na shule tatu, Shule za Msingi Azimio, Mapinduzi na Sabasaba. Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI kipindi hicho akiwa Naibu Waziri alitembelea sisi kama Halmashauri ya Mji tunataka ile shule ijengwe ghorofa ili sasa walimu wasikae kwenye mti kama Ofisi, wanafunzi wasifundishiwe nje chini ya mti, wanafunzi wasirundikane 120 kwenye darasa moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa nini sasa Serikali isiweze kutumia ile asilimia tano ambayo walisema Waziri anaweza akapeleka kwenye matumizi mbalimbali kama tulivyoona ilivyoenda Chato kwenye uwanja wa ndege. Kwa nini msijenge ghorofa katika shule ile kwenye zile asilimia tano ambazo ni zaidi ya shilingi trilioni 1.7 ili sasa kupunguza adha ya ukosefu wa madarasa katika Mji wa Tarime? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, wanasema ukisikia upande mmoja, hakika upande ambao haujasikilizwa utakuwa lazima umekosa. Itakuwa ni vizuri tukajiridhisha sababu ambazo zimesababisha Mkurugenzi azuie uendelezaji wa hiyo shule ili tunapokuja kutoa taarifa iwe ni taarifa ambayo iko balanced. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie mbunge, miongoni mwa maeneo ambayo nitatembelea ni pamoja na kwenda kutazama uhalisia wa hiki ambacho nakisema kwa sababu lengo ni kuhakikisha kwamba tunapunguza msongamano wa vijana wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwaase Waheshimiwa Wabunge na viongozi kwa ujumla, kwamba katika Wilaya ya Tarime, vijana ambao wanamaliza kuanzia darasa la kwanza mpaka darasa la saba wapo 25,000 lakini vijana ambao wanajiandaa kuingia darasa la kwanza wapo 13,000; kwa hiyo, unaweza ukaona sisi kama taifa kuna mambo ambayo lazima tu-address namna ya population growth inavyokwenda, tukiacha tukatizama hivi tukidhani kwamba Serikali peke yake inaweza hakika haiwezekani. Ni vizuri tukashirikishana pande zote ili kutatua matatizo haya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, juu ya swali lake la pili juu ya ujenzi wa ghorofa, ghorofa jambo zuri na ningependa na mimi nijiridhishe halafu tuone na uwezo wetu maana unapotengeneza chakula lazima ujue na unga upo kiasi gani kwa sisi tunaokula ugali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, na juu ya asilimia tano nitaomba niwasiliane na Mheshimiwa Mbunge tuone hiyo asilimia tano na tutayamaliza ili tatizo hili liweze kutatuliwa lakini siamini kwamba asilimia tano inajenga ghorofa. (Makofi)

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Kufuatia utoaji wa elimu ya msingi bure, shule za msingi na sekondari ndani ya Halmashauri ya Mji wa Tarime zimekuwa na upungufu mkubwa wa madarasa na madawati hadi kufikia walimu kulazimika kufundishia chini ya mti na wanafunzi walio madarasani wanakaa kwenye sakafu kwa idadi kubwa kinyume na matakwa ya Sera ya Elimu. Je, ni nini mpango wa Serikali wa kuhakikisha shule hizo ndani ya Halmashauri ya Mji wa Tarime zinaondokana na changamoto za miundombinu ya kufundishia na kujifunzia ili kutoa elimu bora?

Supplementary Question 2

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii kuwapongeza wananchi wa Tanzania, wanajenga sana zahanati, madarasana mifereji.
Je, Serikali haiwezi kuwa na mpango Maalum kwamba wananchi wakijenga kiasi fulani Serikali nayo inakuwa na kiasi fulani inachukua kumalizia kwa sababu watanzania wanajenga mno? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge ni kama amerudia yale ambayo nilikuwa nawaasa Waheshimiwa Wabunge, kwamba hakika kwa kushirikishana wananchi pamoja na Serikali kwa pamoja tunafika na ndiyo maana nikatoa mfano nilivyokuwa nimeenda Moshi Vijijini, Kituo cha Afya ya Kiaseni nimekuta wananchi wamejitoa na Serikali nayo ikapeleka nguvu, hakika tukishirikishana tutaweza kutoka. (Makofi)

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza:- Kufuatia utoaji wa elimu ya msingi bure, shule za msingi na sekondari ndani ya Halmashauri ya Mji wa Tarime zimekuwa na upungufu mkubwa wa madarasa na madawati hadi kufikia walimu kulazimika kufundishia chini ya mti na wanafunzi walio madarasani wanakaa kwenye sakafu kwa idadi kubwa kinyume na matakwa ya Sera ya Elimu. Je, ni nini mpango wa Serikali wa kuhakikisha shule hizo ndani ya Halmashauri ya Mji wa Tarime zinaondokana na changamoto za miundombinu ya kufundishia na kujifunzia ili kutoa elimu bora?

Supplementary Question 3

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote nampongza Mheshimiwa Rais kwa utaratibu wa kutoa elimu bure kwani wanufaika wakubwa ni watoto wenye ulemavu ambao siku za nyuma hawakuweza kupata nafasi hiyo. Hata hivyo, pamoja na jitihada hizo, changamoto ndio bado zipo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende katika suala zima la madawati, madawati ni kweli kabisa yametolewa lakini hayakuzingatia uhitaji hasa kwa watoto wenye ulemavu ambao wengine bado wanalazimika kukaa chini kutokana na hali zao haziwawezeshi kukaa katika madawati hayo.
Je, Serikali ina mpango gani ili basi kuzingatia mahitaji ya watoto hao wenye ulemavu ili waweze kufurahia maisha na kusoma vizuri ili waweze kutimiza ndoto za? Ahsante. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni nia thabiti ya Serikali kuhakikisha kwamba makundi yote yanazingatiwa katika kutengeneza miundombinu, na ndiyo maana katika hizi siku za karibuni nilivyopata fursa ya kutembelea Mkoa wa Arusha, nikafika Kituo cha Afya Muriet, pale unakuta miundombinu kwa ajili ya walemavu nayo imewekwa. Naomba niwatake Wakurugenzi wote wa Halmashauri, jambo lolote kuhusiana na miundombinu inapotengenezwa sasa hivi lazima tuhakikishe hitaji la watu maalum.