Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y MHE. YOSEPHER F. KOMBA) aliuliza:- Ni dhamira ya Serikali kutekeleza mpango wa elimu bure kuanzia chekechea hadi kidato cha nne, lakini mpango huu una changamoto ambazo zisipotatuliwa zitasababisha kushuka kwa ubora wa elimu. (a) Je, ni nini tamko la Serikali juu ya wanafunzi wanaoanza kidato cha kwanza kwa kigezo cha kutofaulu kwa kiwango cha kianzia alama 100 na kuendelea? (b) Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha ujenzi wa maabara unakamilika kwa wakati?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Sera ya Elimu Bure imewasaidia baadhi ya wazazi wasio na uwezo kuandikisha watoto shuleni, lakini wakati huo huo bado kuna michango kadhaa inayoendelea kwa baadhi ya shule na michango hii imerudisha nyuma morali ya wazazi kuchangia kwa juhudi katika maendeleo mbalimbali ya shule.
Je, Serikali ipo tayari sasa kutoa elimu kwa wananchi kwamba sera ni elimu bila ada na siyo elimu bure ili kuwafanya wananchi waweze kuchangia kwa nguvu kama ilivyokuwa zamani? (Makofi)
Swali la pili, shule za Sekondari za Keni, Shimbi na Bustani katika Halmashauri ya Wilaya ya Rombo ni shule ambazo zimejengwa kwa mtindo wa ghorofa kwa sababu ya uhaba wa ardhi katika Wilaya ya Rombo na sasa zina muda karibu wa zaidi ya miaka 10 wananchi wameshindwa kuzikamilisha.
Je, Serikali ipo tayari katika bajeti ijayo katika bajeti
ijayo kuzipokea hizi shule na kuzikamilisha ili kuweza kuunga mkono nguvu za wananchi katika jitihada zao za kufanya maendeleo mengine kama kumalizia maabara?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS – TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubalina na Mheshimiwa Selasini kwamba kuna michango ambayo inaruhusiwa. Lakini michango ile ina utaratibu kwamba ili kusudi mchango uweze kukubalika kisheria ni lazima Kamati ya Shule au bodi ya shule iwe imeujadili na kupeleka kwa wadau ambao ni wazazi, wakipitisha wanaomba kibali kwa Mkuu wa Mkoa, wakipata kibali basi hapo wanaweza wakaendelea na kuchangishana. Huo ni utaratibu ambao ni mzuri, namshauri Mheshimiwa Mbunge autumie. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa swali lake
la pili, sisi Ofisi ya Rais, TAMISEMI pamoja na Wizara ya Elimu tupo tayari kukaa na Mheshimiwa Mbunge ili tuweze kujadili namna ambavyo tunaweza tukaboresha utaratibu wa kuzikamilisha hizi shule ambazo anazizungumzia. (Makofi)

Name

Upendo Furaha Peneza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y MHE. YOSEPHER F. KOMBA) aliuliza:- Ni dhamira ya Serikali kutekeleza mpango wa elimu bure kuanzia chekechea hadi kidato cha nne, lakini mpango huu una changamoto ambazo zisipotatuliwa zitasababisha kushuka kwa ubora wa elimu. (a) Je, ni nini tamko la Serikali juu ya wanafunzi wanaoanza kidato cha kwanza kwa kigezo cha kutofaulu kwa kiwango cha kianzia alama 100 na kuendelea? (b) Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha ujenzi wa maabara unakamilika kwa wakati?

Supplementary Question 2

MHE. UPENDO F. PENEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona.
Katika suala la elimu bure, moja ya changamoto ni pamoja na utoro unaowakabili hasa watoto wa kike. Sasa ningependa kujua Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba Serikali sasa ina mpango gani kuhakikisha ya kwamba watoto wa kike wanaoingia shuleni wanabaki shuleni kwa kumaliza, kwa Serikali kuweka pesa za ruzuku kwa ajili ya sanitary pads (vifaa vya hedhi) kuziongeza katika capitation fund ili kuweza kupunguza suala la utoro mashuleni. Sasa Serikali ina mkakati gani katika bajeti ijayo kuongeza pesa hizo ili watoto wetu waweze kupata pedi hizo bure mashuleni? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA
NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika makubaliano ya Jumuiya ya East Africa nadhani ni miongoni mwa jambo ambalo lilikuwa likijadiliwa sana hasa tatizo kubwa la watoto wasichana wanapokosa hivi vifaa kwa ajili ya kujikimu wakiwa shuleni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tulichukue hili kwa sababu ni jambo la msingi basi tukifika kwenye mchakato wa bajeti sisi sote tushirikiane kwa pamoja tuangalie nini tufanye ili mradi kuhakikisha kwamba tuweze kusaidia vijana wetu watulie masomoni na wapate elimu vizuri. Kwa hiyo, tunalichukua kama mchango mzuri katika mchakato tutakuja tutaijadili. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y MHE. YOSEPHER F. KOMBA) aliuliza:- Ni dhamira ya Serikali kutekeleza mpango wa elimu bure kuanzia chekechea hadi kidato cha nne, lakini mpango huu una changamoto ambazo zisipotatuliwa zitasababisha kushuka kwa ubora wa elimu. (a) Je, ni nini tamko la Serikali juu ya wanafunzi wanaoanza kidato cha kwanza kwa kigezo cha kutofaulu kwa kiwango cha kianzia alama 100 na kuendelea? (b) Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha ujenzi wa maabara unakamilika kwa wakati?

Supplementary Question 3

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, naomba niulize swali dogo la nyongeza.
Hivi karibuni Naibu Waziri wa Elimu ametoa kauli akisema watoto wakitaka kuolewa wawe na cheti cha kumaliza form four, wakati huo huo Serikali ilisema wale wanafunzi ambao wanapata ujauzito wakiwa shuleni wasiendelee.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ningependa nipate
kauli ya Serikali katika mkanganyiko huu, nini hasa ni kauli ya Serikali sahihi. Vipi wanafunzi ambao wanapata mimba wakiwa shuleni na hawaendelei kwa mfumo wa shule, lakini na kauli ya Waziri ya kusema anayetaka kuolewa awe na cheti cha form four? Ahsante. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS – TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (TAMISEMI) -MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa majibu sahihi kwa Mheshimiwa Waitara pamoja na Watanzania wote waliopata mkanganyiko kuhusu kauli hiyo ni kwamba, nilisema Sera Mpya ya Elimu ya mwaka 2014 huko tunakoelekea inabadilisha mfumo wa sasa wa elimu kwenda kwenye mfumo mpya ambao utahitaji mtoto aanze chekechea mwaka mmoja, asome shule ya msingi miaka sita, shule ya sekondari miaka minne na hii itakuwa ni lazima kwa yeyote atakayeanza darasa la kwanza hadi amalize form four. Kwa hiyo, nikasema kwamba tutakapofika wakati huo, kithibitisho muhimu kwamba huyu mtoto sasa amemaliza form four ni school leaving certificate, wakati huo siyo leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ndugu yangu Mheshimiwa Waitara huo ni ufafanuzi sahihi kabisa wa sera mpya. Sasa hivi tunaandaa utaratibu na maandalizi ikiwepo pamoja na miundombinu ili tuweze hatimae kuitekeleza hiyo sera muda utakapofika. Kwa hiyo, usiwe na mkanganyiko ndugu yangu Waitara. (Makofi)

Name

Dr. Haji Hussein Mponda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y MHE. YOSEPHER F. KOMBA) aliuliza:- Ni dhamira ya Serikali kutekeleza mpango wa elimu bure kuanzia chekechea hadi kidato cha nne, lakini mpango huu una changamoto ambazo zisipotatuliwa zitasababisha kushuka kwa ubora wa elimu. (a) Je, ni nini tamko la Serikali juu ya wanafunzi wanaoanza kidato cha kwanza kwa kigezo cha kutofaulu kwa kiwango cha kianzia alama 100 na kuendelea? (b) Je, ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha ujenzi wa maabara unakamilika kwa wakati?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. HADJI H. MPONDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jibu la msingi Waziri amezungumzia kwamba baadhi ya Halmashauri tayari wameshamaliza ujenzi wa maabara katika shule za sekondari na mojawapo ya Halmashauri hii ni Halmashauri ya Malinyi tumeshamaliza karibu asilimia 90 ya maabara ya masomo ya sayansi katika shule za sekondari na baadhi ya majengo haya sasa hivi yanaanza kuharibiwa na wadudu wau ndege aina ya popo.
Je, ni lini Serikali watakamilisha utaratibu wa kupeleka vifaa ili maabara hizo zianze kutumika rasmi.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwamba tuliweza kununua vifaa kwa ajili ya maabara zaidi ya 1,000, tumeweza kuvisambaza. Ninafahamu Mheshimiwa Dkt. Mponda hata tulivyofika kule kwako Malinyi tuliona kweli ulitoa concern hiyo.
Kwa hiyo, tutafanya kila liwezekanalo kuona jinsi ya upelekaji wa vifaa. Hata hivyo, katika ile shule ambayo ulisema ina changamoto kubwa, kabla ya mwezi wa pili nadhani tutafanya kazi kubwa kuhakikisha kwamba shule ile tunaiboresha, wananchi wa Malinyi ambao wana changamoto kubwa sana waweze kupata elimu vizuri.(Makofi)