Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

RUTH H. MOLLEL aliuliza:- Maboresho ya utendaji wa Serikali za Mitaa yalilenga kuimarisha na kujenga uwezo wa Serikali za Mitaa kujiendesha kwa kuwapatia rasilimali watu na fedha za kutosha kutekeleza Sera ya Ugatuaji wa Madaraka. Je, Serikali ina lengo gani kuimarisha Serikali za Mitaa ziweze kujiendesha?

Supplementary Question 1

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, ili hawa watumishi wa Serikali za Mitaa waweze kutoa huduma kwa ufanisi wanahitaji kupata mafunzo ya mara kwa mara ili kuboresha utendaji wao. Kwa kuwa kwa muda mrefu mafunzo yamesimamishwa, tunategemeaje hawa watumishi waweze kutoa huduma ipasavyo? Hilo swali la kwanza.
Mheshimiwa Spika, swali la pili, viongozi ambao wako karibu sana wananchi ni Watendaji wa Kata na Mitaa pamoja na Wenyeviti wa Vijiji na Wenyeviti wa Kata, ndio wapo karibu sana na wananchi na ndio ambao wanatoa huduma karibu kabisa na wananchi. Watendaji wanapata mshahara lakini Wenyeviti hawapati chochote. Je, Serikali ina mpango gani kwa ajili ya kuwamotisha Wenyeviti ili waweze kutoa huduma vizuri kwa wananchi? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Spika, katika maeneo ambayo yamejengewa uwezo kwa hali ya juu kabisa ni hili eneo la Serikali za Mitaa. Kuna programu nyingi sana za kisekta zimeendelea kutoa mafunzo mbalimbali kwa nyakatii mbalimbali. Kuna Programu kwa mfano ya Kuendeleza Sekta ya Kilimo, Programu ya Kuendeleza Sekta ya Maji, zote hizi zimekuwa na mafunzo mbalimbali kwa watendaji wa Serikali za mitaa kwa ajili ya kuimarisha uwezo wao, hasa hasa zile kada za fedha, ununuzi na wahandisi. Serikali inatoa commitment ya kuendelea kutoa mafunzo mara fedha zinapopatikana.
Mheshimiwa Spika, swali la pili kuhusu posho za Wenyeviti wa Serikali za Vijiji na Vitongoji. Mwongozo uliopo ni kwamba kila Halmashauri inatakiwa iboreshe makusanyo yake ya ndani, iongeze makusanyo yake ya ndani na mwongozo uliopo ni kwamba asilimia 20 ya mapato yake ya ndani yanatakiwa yatumike kwa ajili ya posho na agizo ambalo limetolewa na kusisitizwa na Serikali ni kwamba wale ambao wanachelewesha kulipa posho za wenyeviti wa vijiji na vitongoji sasa itabidi wachukuliwe hatua.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

RUTH H. MOLLEL aliuliza:- Maboresho ya utendaji wa Serikali za Mitaa yalilenga kuimarisha na kujenga uwezo wa Serikali za Mitaa kujiendesha kwa kuwapatia rasilimali watu na fedha za kutosha kutekeleza Sera ya Ugatuaji wa Madaraka. Je, Serikali ina lengo gani kuimarisha Serikali za Mitaa ziweze kujiendesha?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa lengo la Serikali kuchukua vyanzo vingi vya Halmashauri za Wilaya ilikuwa ni kusaidia ruzuku ya kutosha kwenye Halmashauri hizi. Lakini kwa kuwa ruzuku inayotolewa haitoshelezi kabisa kwa Halmashauri hizi kujiendesha.
Sasa swali langu, naishauri Serikali kwamba je, Serikali inaweza kurudisha baadhi ya vyanzo vya mapato kwa Halmashauri ili nazo ziweze kujiendesha badala ya kusubiri ruzuku na ruzuku yenyewe inachelewa sana?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu wangu katika swali la msingi nilipenda kujibu swali la Mheshimiwa Lubeleje ambapo mimi ninamuita greda la zamani makali ya yale yale. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kuna vyanzo mbalimbali vilichuliwa na Serilkali Kuu. Hata hivyo, kwa mamlaka tuliyopewa tutafanya namna ili kuhakikisha kwamba mapato, hata hayo ya vyanzo vilivyobaki yaweze kukusanywa vizuri.
Mheshimiwa Spika, ilikuwa kwamba hata miongoni mwa vyanzo tulivyokuwa navyo ukusanyaji ulikuwa na changamoto kubwa na ndiyo maana katika program zetu hivi sasa tunafanya namna ili tuweze kutumia mifomu ya electronic kwa ajili ya uongezaji wa mapato.
Mheshimiwa Spika, naomba niwahakikishieni kwamba sasa hivi Wizara ya Fedha imefanya commitment kwamba fedha zote zilizokusanywa zipelekwe na ndiyo maana mpaka leo hii ninavyozungumza katika quarter ya kwanza zaidi ya shilingi trilioni moja imechukuliwa katika Mamlaka ya Serikali za Mitaa katika OC na miradi ya maendeleo.
Kwa hiyo, ni imani yangu kwamba kutokana commitment ya Serikali katika ukusanyaji wa mapato jambo hili litakwenda vizuri; na hatimaye Mamlaka za Serikali za Mitaa zitaweza kutimiza wajibu wake kama inavyokusudiwa.