Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Morogoro umekamilika lakini haina umeme wala maji:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme na maji katika hospitali hiyo ili ianze kutumika na kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya Morogoro?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, pia nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Sasa naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa ni sera na mpango wa Serikali kila wilaya kuwa na hospitali, je, ni lini ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Vijijini utaanza licha ya jitihada nyingi za Serikali?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni lini ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Mvomero utakamilika?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) : Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba ni sera ya Serikali kujenga hospitali moja kila wilaya na napenda nimhakikishie Mheshimiwa Dokta Ishengoma na Waheshimiwa Wabunge wote kwamba Serikali itaendelea kuwezesha ujenzi wa hospitali moja kila wilaya kwa awamu. Katika Mkoa wa Morogoro tumeanza na Manispaa ya Morogoro na tutaendelea na wilaya nyingine kwa awamu zinazofuata. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri wangu, katika sehemu ya pili ya swali lake Mheshimiwa Dokta Ishengoma kuhusu Hospitali ya Mvomero na bahati nzuri tulikuwa pale Mvomero tukabaini baadhi ya upungufu. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imeshatenga fedha ya kumalizia jengo lile baada ya kuona upungufu ule na imani yangu ni kwamba kabla ya mwezi Januari hospitali ile itakuwa imekamilika ili wananchi wa Mvomero waweze kupata huduma vizuri. (Makofi)

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Morogoro umekamilika lakini haina umeme wala maji:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme na maji katika hospitali hiyo ili ianze kutumika na kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya Morogoro?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Majimbo ya Longido na Ngorongoro ni majimbo ambayo yapo kwenye mazingira magumu sana na upatikanaji wa huduma za afya si wa uhakika. Wilaya ya Ngorongoro haina hospitali ya wilaya, Wilaya ya Longido imetengwa kwenye bajeti lakini utekelezaji bado. Je, ni lini Serikali itaweka mkazo kwenye majimbo haya ambayo kwa kweli yana mazingira magumu ya kijiografia?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama alivyosema mwenyewe kwamba Majimbo ya Longido na Ngorongoro yapo katika mazingira magumu na Wilaya ya Longido hakuna hospitali na Wilaya ya Ngorongoro tayari iko katika bajeti. Naomba ushirikiano wake mara fedha ambazo zipo kwenye bajeti zitakapopelekwa, ashiriki kikamilifu katika kusimamia ili matumizi ya fedha zile yawe mazuri kama ambavyo ilikusudiwa. Mwaka ujao wa fedha tushirikiane naye kuhakikisha kwamba Longido nao tunawawekea bajeti. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Morogoro umekamilika lakini haina umeme wala maji:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme na maji katika hospitali hiyo ili ianze kutumika na kupunguza msongamano wa wagonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya Morogoro?

Supplementary Question 3

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Tabora Manispaa tuna tatizo kubwa la msongamano wa wagonjwa katika Hospitali Teule ya Kitete na kwa kuzingatia hilo, Tabora Halmashauri kwa kushirikiana na Madiwani pamoja na wananchi wengine tumetenga eneo kwa ajili ya kujengwa Hospitali ya Wilaya ambayo mpaka sasa hivi ujenzi wake unasuasua kwa sababu ya ukosefu wa fedha. Je, Serikali inajipanga vipi katika kusaidia uwezeshaji wa kuweza kujenga hospitali hiyo ya wilaya?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba nimshukuru Mheshimiwa Mwakasaka pamoja na Waheshimiwa Madiwani katika Manispaa ya Tabora kwa kutenga eneo la kujenga Hospitali mpya kwenye Manispaa ya Tabora ambayo itakuwa Hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa msingi huohuo, kwa kuzingatia kwamba Hospitali ya Kitete ni kweli imezidiwa na mzigo maana yake ndiyo hospitali pekee ya rufaa ya mkoa, Serikali inaahidi na namwomba ushirikiano wake, wakati tutakapokuwa tunaweka kwenye bajeti tushirikiane ili tuweze kupitisha kwa pamoja. Ahsante sana.