Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:- Wilaya ya Mkalama ni mpya na haina vitendea kazi kama vile magari katika katika Idara ya Afya na huduma za dharura zinapatikana makao makuu huku tarafa zikiwa zimetawanyika hivyo wananchi hasa wajawazito na watoto wamekuwa wakipoteza maisha kabla ya kufika hospitali kwa kukosa usafiri. Je, ni lini Serikali itatoa gari la wagonjwa (ambulance) tatu kwa kila tarafa ikiwemo Makao Makuu ili kunusuru vifo hivyo?

Supplementary Question 1

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwanza naomba niweke rekodi sawasawa. Cha kwanza, Wilaya ya Mkalama haina Hospitali ya Wilaya, pili mapato ya ndani ni kidogo ukilinganisha na mahitaji ya Wilaya mpya zote Tanzania na tatu ni kwamba gari lililopo lilirithiwa kutoka Wilaya ya Iramba na uzoefu unaonyesha mgawanyo wa mali unapofanyika Wilaya mpya zinapata yale magari mabovu mabovu, hilo gari lipo tu kwenye vitabu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, ni lini Serikali itatoa magari mapya na ya uhakika kwa Wilaya zote mpya Tanzania ikiwepo Mkalama? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Serikali pamoja na kujenga Kituo cha Afya ina mpango gani wa kunusuru vifo hasa vya akina mama na watoto katika mazingira ya kutokuwepo na gari la wagonjwa? Mheshimiwa Naibu Waziri ameshafika Mkalama na Naibu Waziri wa Afya naye alishafika Mkalama na kuona jiografia ile, hapa nilipo wananchi wangu wanalia kila siku msiba.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mheshimiwa Mbunge Jimbo lake limegawanyika kutokana na lile Jimbo alilokuwa Mheshimiwa Mwigulu Mchemba. Tulivyofika pale miongoni mwa changamoto kubwa sana katika Jimbo lake, kwanza kweli hawana Hospitali ya Wilaya lakini ndiyo maana jambo kubwa tulilolifanya kutokana na shida kubwa iliyopatikana pale, Mheshimiwa Mbunge alinipeleka pale na tukaweza kuangalia kwa pamoja tukaweka katika mpango wao wa sasa kuhakikisha kwamba tunakikarabati kile Kituo cha Afya ili waweze kuwa na theater kabisa ya upasuaji wa watoto na Mungu akijalia tutapeleka mradi wa takribani shilingi milioni 700.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali la lini gari la wagonjwa litapatikana, naomba nisitoe commitment ni lini litapatikana. Kama nilivyosema awali katika majibu yangu ya msingi kwamba jambo kubwa hili tuanzie katika needs assement ya Halmashauri yetu. Naomba niseme kwamba Serikali imesikia kilio cha Mheshimiwa Allan na tutaangalia uwezekano wowote utakaowezekana, tukipata fursa tutatoa kipaumbele kwa Jimbo la Mkalama kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma ya kutosha.
Mheshimiwa Mweyekiti, hata hivyo, niseme kwamba kama Serikali kwa umoja wake inajua kwamba wananchi wa Mkalama wana shida kubwa sana, tutajadiliana kwa pamoja kwa mawazo mapana zaidi. Kwa sababu licha ya kutokuwa na vituo vya afya…
Hata miundombinu ya barabara kuwasaidia wagonjwa kufika hospitalini ni shida tutalifanyia kazi.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:- Wilaya ya Mkalama ni mpya na haina vitendea kazi kama vile magari katika katika Idara ya Afya na huduma za dharura zinapatikana makao makuu huku tarafa zikiwa zimetawanyika hivyo wananchi hasa wajawazito na watoto wamekuwa wakipoteza maisha kabla ya kufika hospitali kwa kukosa usafiri. Je, ni lini Serikali itatoa gari la wagonjwa (ambulance) tatu kwa kila tarafa ikiwemo Makao Makuu ili kunusuru vifo hivyo?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwa kuwa Ukerewe inaundwa na visiwa na kwa kuwa yanapotokea matatizo ya dharura kiafya inakuwa kazi ngumu sana kuwawahisha wagonjwa kupata huduma ya ziada.
Je, sasa Serikali haioni umuhimu wa kutoa ambulance boat kuweza kusaidia kuokoa maisha ya wananchi wa Ukerewe?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshiniwa Mwenyekiti, najua kwamba tulipeleka ambulance kule ya kawaida katika kipindi cha kati, lakini na mahitaji ya kwamba watu wa Ukerewe wapate ambulance boat, naomba Serikali tuchukue kwa mawazo yenu mapana. Kama Mbunge anavyofahamu tuliongea naye private kwamba tutafika Ukerewe baada ya Bunge hili, tukifika kule tutajadiliana kwa mapana na pamoja nini tutawasaidia wananchi wa Ukerewe. Pia jambo hili tutaangalia jinsi gani tuliweke katika kipaumbele kama Serikali kwa kuweka mawazo ya pamoja kwa upana wake.

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:- Wilaya ya Mkalama ni mpya na haina vitendea kazi kama vile magari katika katika Idara ya Afya na huduma za dharura zinapatikana makao makuu huku tarafa zikiwa zimetawanyika hivyo wananchi hasa wajawazito na watoto wamekuwa wakipoteza maisha kabla ya kufika hospitali kwa kukosa usafiri. Je, ni lini Serikali itatoa gari la wagonjwa (ambulance) tatu kwa kila tarafa ikiwemo Makao Makuu ili kunusuru vifo hivyo?

Supplementary Question 3

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Chemba ni kati ya Wilaya mpya katika Mkoa wetu wa Dodoma. Ukitoka Kondoa kwenda Chemba ni zaidi ya kilomita 50 na ukitoka Dodoma Mjini kwenda Chemba ni zaidi ya kilomita 100 lakini Kituo cha Afya kilichopo pale hakikidhi mahitaji na Kituo cha Bahi ambacho kinahesabika kama Hospitali ya Wilaya bado kina upungufu makubwa. Je, lini Serikali itaungana na wananchi wa Chemba kuhakikisha kwamba Makao Makuu ya Wilaya inapata hospitali ya Wilaya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini ni kwamba mpango wa Serikali wa mwaka huu imetengwa shilingi milioni 23 ambayo ni kwa ajili ya kuhakikisha tunafanya maandalizi ya awali lakini tumeshaingiza katika mpango mwingine na vilevile wenzetu wa Chemba wako katika mchakato wa kushirikisha National Health Insurance Fund katika jambo hilo. Kwa hiyo, naomba tuseme kwamba mipango hii yote itaenda kwa pamoja kusaidia Chemba iweze kupata kituo cha afya. Hata hivyo, ndiyo maana tunaamua kufanya ukarabati mkubwa katika Kituo kimoja cha Afya cha Chemba na Bahi tupunguze referral system ili kusaidia wananchi kupata huduma za upasuaji wakiwa katika maeneo yao.