Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kasuku Samson Bilago

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. KASUKU S. BILAGO aliuliza:- Maeneo mengi ya Wilaya ya Kakonko yanaonyesha kuwepo kwa madini yenye thamani kama dhahabu na almasi. (a) Je, kuna tafiti zozote zilizofanyika kuhusu upatikanaji wa madini Wilaya ya Kakonko? (b) Kama zipo, je, ni madini gani yanapatikana na ni katika maeneo yapi?

Supplementary Question 1

MHE. KASUKU S. BILAGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, ulitaka kupanua goli. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri aliyotoa kwa swali hili, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, katika eneo hili ambalo lina chokaa linaloitwa Bumuli maarufu Ngongogwa liko katika Hifadhi ya Moyowosi - Kigosi. Wafanyabiashara wanaotaka kuchimba hiyo chokaa wamekuwa wakikwamishwa na shughuli zinazofanyika katika hifadhi na Mamlaka ya Hifadhi kuwazuia kufanya shughuli hiyo. Je, Serikali inaweza ikatoa utaratibu mahsusi watakaofuata wananchi wa Kaknoko ili waweze kuchimba chokaa hiyo ambayo ni grade two? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ipo dhahabu ambayo imepatikana sehemu za Nyamwilonge na Nyakayenze na maeneo ya Ruhuli inayoendelea kuchimbwa na wachimbaji wadogo wadogo kwa kutumia zana hafifu. Je, Serikali iko tayari kutoa ruzuku kwa wachimbaji wadogo wadogo katika maeneo hayo? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mheshimiwa Bilago lakini pia namshukuru kwa sababu anafuatilia sana maeneo ya wachimbaji katika maeneo yake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imechukua hatua nyingi sana, lakini kulingana na Sheria ya Madini na Sheria ya Hifadhi ya Mazingira, kifungu cha 95 cha Sheria ya Madini kinatoa utaratibu na utaratibu unaotumika hivi sasa kuchimba madini katika maeneo mengine kwanza kabisa mtu anaruhusiwa kupata leseni lakini akishapata leseni ya uchimbaji anawaona watu wa maliasili ili apate kibali cha maandishi na huo ndiyo utaratibu unaotumika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeshatoa leseni 70 katika maeneo karibu na Hifadhi ya Moyowosi na hizo leseni wananchi wanachimba na kuna vikundi viwili vya ushirika ambapo wanafanya kazi hiyo. Kwa hiyo, Mheshimiwa Bilago utaratibu upo lakini ni vizuri tukaa zaidi ili nikueleweshe ili wananchi wa Jimbo lako wanufaike zaidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la nyongeza la pili, maeneo ya Nyamwilonge na Nyakayenze pamoja na Makele na maeneo ya mbali, maeneo haya tumeshatoa leseni kwa sababu kuna uchimbaji mzuri wa dhahabu. Mwaka 2012 kuligunduliwa dhahabu na tukalitenga eneo hilo na hivi sasa kuna leseni 76 katika maeneo hayo. Nimuombe Mheshimiwa Bilago awahamasishe wananchi wa Jimbo lake ili eneo lililobaki tulilolitenga pia walitumie kwa manufaa ya maisha yao.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. KASUKU S. BILAGO aliuliza:- Maeneo mengi ya Wilaya ya Kakonko yanaonyesha kuwepo kwa madini yenye thamani kama dhahabu na almasi. (a) Je, kuna tafiti zozote zilizofanyika kuhusu upatikanaji wa madini Wilaya ya Kakonko? (b) Kama zipo, je, ni madini gani yanapatikana na ni katika maeneo yapi?

Supplementary Question 2

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa chanzo kikubwa cha migogoro kati ya wananchi na wawekezaji wanaoenda kuwekeza kwenye sekta hii ya uchimbaji wa madini ni utaratibu unaotumika wa kumalizana na wawekezaji kitaifa na kutowashirikisha vizuri wale wa Wilayani na pale kijijini penyewe ambapo utafiti au uchimbaji unakwenda kufanyika na mfano mzuri ni katika Jimbo langu la Mtama, Kata ya Namangale kuna utafiti unafanyika wa graphite na Kampuni ya Nachi Resources lakini mgogoro uliopo ni kwamba wananchi wa eneo lile hawaelewi kinachoendelea na hivyo kubaki na malalamiko mengi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ni lini Serikali itabadilisha huu utaratibu na kuwasaidia wananchi wangu wapate uelewa wa kinachoendelea ili waone ushiriki wao utakuwaje?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Nape tumekuwa tukishirikiana sana katika hili na wananchi wa Mtama nadhani ni mashahidi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii nisema utaratibu unaotumika ni kwamba mwekezaji yeyote anayepata leseni, hatua ya kwanza akishapata leseni ni kuonana na uongozi wa Halmashauri au uongozi unaohusika wa wilaya na kama hilo halifanyiki ni uvunjivu wa sheria na sisi tutalisimamia.
Lakini pia nichukue nafasi hii kusema kwamba tutapita katika maeneo ya kero, tumeshapanga utaratibu, kuanzia tarehe 02 Agosti, 2017 tunashughulikia matatizo hayo. Kwa hiyo, Mheshimiwa Nape hata kwake tutafika. Ahsante sana.

Name

Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. KASUKU S. BILAGO aliuliza:- Maeneo mengi ya Wilaya ya Kakonko yanaonyesha kuwepo kwa madini yenye thamani kama dhahabu na almasi. (a) Je, kuna tafiti zozote zilizofanyika kuhusu upatikanaji wa madini Wilaya ya Kakonko? (b) Kama zipo, je, ni madini gani yanapatikana na ni katika maeneo yapi?

Supplementary Question 3

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kata ya Isulamilomo, Jimbo la Nsimbo katika Mkoa wa Katavi kuna mwekezaji yuko pale, hana leseni na kuna vijana zaidi ya 4,000 hawana leseni, lakini mwekezaji huyu sijui anapata nguvu gani ya kuwazuia hawa wachimbaji wadogo wadogo zaidi ya 4,000 kuchimba lakini zaidi wanapigwa na wananyanyaswa kwenye huu mgodi mpya ulioko katika Jimbo la Nsimbo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nini tamko la Serikali sasa ili tujue nani ni halali kuchimba katika mgodi huu?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninamshukuru kwa kutupa taarifa, lakini atusaidie zaidi mwekezaji huyu ni nani, utatusaidia sana Mheshimiwa Mbunge. Hebu tupatie huyo ni nani halafu tukafanyie kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jibu la msingi ni kwamba maeneo yote ambayo wawekezaji wameyashikilia bila kuyafanyia kazi Serikali sasa inayatwaa kwa mujibu wa sheria ili iwagawie wananchi. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge tutakaa pamoja tuone kero hiyo tuitatue kwa mujibu wa sheria, ikiwezekana kabisa tutachukua hatua za kisheria. (Makofi)