Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jaku Hashim Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. JAKU HASHIM AYOUB aliuliza:- Kuna mjenzi aliyejenga Vituo vya Polisi kupitia Kampuni iitwayo Al Batna Building Co. Ltd. Vituo alivyojenga ni Kituo cha Polisi Mkokotoni - Unguja na Kituo cha Polisi cha Madungu kilichoko Chakechake Pemba kwa gharama ya shilingi 223,440,000. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa deni hilo tangu 2012 hadi leo hii? (b) Je, Serikali inayo taarifa kwamba mwenye kampuni hiyo aliyejenga vituo hivyo amepata maradhi makubwa huku akihangaika kufuatilia haki yake hiyo bila mafanikio? (c) Je, ni lini Serikali itamtembelea na kumpa pole kwa maradhi hayo mabaya yaliyompata?

Supplementary Question 1

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa umakini wake, ufuatiliaji wake na utendaji wake na hasa kwa wapiga kura wake vilevile Jimboni kwake ingawa majukumu ni mengi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza kwa kukiri na hii ni mara ya pili kukiri, katika wakati wa bajeti na leo hii. Nafikira baada ya kupitisha bajeti yake ataniambia labda kesho au kesho kutwa tufuatane. Naomba kumwuliza maswali mawili madogo sana ya nyongeza.
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, zabuni zinafunguliwa na Serikali, iweje leo hii uhakiki ufanyike wakati mradi umeshafanyika na kukamilika karibu miaka mitano? That is (a).
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa mhusika amemaliza kazi, kwa nini Serikali isimlipe fedha yake na uhakiki huo ufanyike kwa watendaji waliosimamia tender hizo ili kuwawajibisha? Hii ni sawa sawa na kumchukua kuku aliyechinjwa kisha akaliwa, ushahidi huwezi kuupata. (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Jaku kwa kufuatilia masuala yanayohusu wananchi wake. Hili siyo jambo moja ambalo Mheshimiwa Jaku amefanya hivyo, nawaomba na Wabunge wengine tuige mwenendo wake. Panapotokea jambo linalohusu wapiga kura wake, Mheshimiwa Jaku huwa anafuatilia Ofisini, Wizarani na hapa Bungeni. Nampongeza sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba suala la uhakiki ni utaratibu ambao tulijiwekea Serikalini kwa ajili ya; moja, kuwa na uhakika wa madeni ambayo yanatakiwa kulipwa; pili, kuweka kumbukumbu sawa ili kuondokana na ulipaji wa madeni mara mbili. Hii ina faida pia hata kwa anayedai kuweza kuhakikisha kwamba haki yake haipotei. Kwa maana hiyo, kwa sababu ni utaratibu ambao una-cut across kwa wazabuni wote kwa madeni yote ya Serikali na suppliers wengine wote, ni lazima na sisi kama Wizara, ni lazima tufuate taratibu hizo kwa wazabuni wote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa taratibu hizo zilishafanyika kama nilivyokwambia, sasa hivi ni suala tu la upatikanaji wa fedha. Sehemu kubwa ilikuwa ni kukubalika kwa deni hilo, kukubalika kwa kazi ambavyo hivyo vyote vimeshafanyika na tunampongeza kwamba amefanya kazi nzuri.

Name

Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. JAKU HASHIM AYOUB aliuliza:- Kuna mjenzi aliyejenga Vituo vya Polisi kupitia Kampuni iitwayo Al Batna Building Co. Ltd. Vituo alivyojenga ni Kituo cha Polisi Mkokotoni - Unguja na Kituo cha Polisi cha Madungu kilichoko Chakechake Pemba kwa gharama ya shilingi 223,440,000. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa deni hilo tangu 2012 hadi leo hii? (b) Je, Serikali inayo taarifa kwamba mwenye kampuni hiyo aliyejenga vituo hivyo amepata maradhi makubwa huku akihangaika kufuatilia haki yake hiyo bila mafanikio? (c) Je, ni lini Serikali itamtembelea na kumpa pole kwa maradhi hayo mabaya yaliyompata?

Supplementary Question 2

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kumekuwa na upungufu wa vituo vya polisi nchini. Pamoja na changamoto hizo, lakini polisi hao wamekuwa na changamoto za kukosa magari na mafuta kwa ajili ya kulinda wananchi wetu kwenye maeneo yetu. Vilevile hivi karibuni polisi wamekuwa wakilalamika kwamba magari hayana mafuta, kwa hiyo, wanashindwa kufanya doria kuzunguka kwenye maeneo korofi kwa ajili ya kuwalinda wananchi wa Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nini mkakati wa Serikali wa kuhakikisha sasa polisi hao wanapatiwa mafuta, lakini pia kuongezewa magari kwa ajili ya usalama wa Watanzania? Ahsante.

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia jambo la sskari wetu. Niwahakikishie tu Waheshimiwa Wabunge kwamba katika bajeti hii tuliyopitisha, fedha zilizotengwa kwa ajili ya mafuta, doria pamoja na shughuli nyingine imeongezeka tofauti na iliyokuwa inatoka katika Awamu ya Kwanza ya mwaka wa fedha uliopita. Kwa maana hiyo, tutakuwa tumepunguza kwa kiwango kikubwa ukosefu wa mafuta katika shughuli zetu hizo za doria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2016 tulipokea magari 77 kwa ajili ya askari wetu na kati ya mwezi huu mpaka mwezi wa saba tunatarajia kupokea magari mengine zaidi ya 200 na tutayagawa katika maeneo ambayo yana uhitaji mkubwa wa magari kwa ajili ya shughuli za doria ikiwemo Mikoa kama ya Kagera, Kigoma, Katavi pamoja na maeneo mengine ambayo yanahitaji doria na yanahitaji magari yawepo katika maeneo yale ikiwemo kwa ndugu yangu Mheshimiwa Nsanzugwanko na Mheshimiwa Bilago.

Name

Emmanuel Adamson Mwakasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. JAKU HASHIM AYOUB aliuliza:- Kuna mjenzi aliyejenga Vituo vya Polisi kupitia Kampuni iitwayo Al Batna Building Co. Ltd. Vituo alivyojenga ni Kituo cha Polisi Mkokotoni - Unguja na Kituo cha Polisi cha Madungu kilichoko Chakechake Pemba kwa gharama ya shilingi 223,440,000. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa deni hilo tangu 2012 hadi leo hii? (b) Je, Serikali inayo taarifa kwamba mwenye kampuni hiyo aliyejenga vituo hivyo amepata maradhi makubwa huku akihangaika kufuatilia haki yake hiyo bila mafanikio? (c) Je, ni lini Serikali itamtembelea na kumpa pole kwa maradhi hayo mabaya yaliyompata?

Supplementary Question 3

MHE. EMANUEL A. MWAKASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Tatizo la kutolipa wakandarasi au wazabuni katika sehemu mbalimbali za nchi hasa wale ambao wanatoa huduma kwenye vituo vya polisi limekuwa ni kubwa kwa muda mrefu. Kwa mfano, mkoani Tabora kuna wazabuni wengi ambao wanaidai polisi malimbikizo ya muda mrefu ya huduma wanazotoa na hasa utengenezaji wa magari.
Kwa mfano Tabora yapo malalamiko ya muda mrefu ya mzabuni ambaye anatengeneza magari ya polisi hajalipwa sasa hivi ni zaidi ya miaka mitatu, anadai zaidi ya shilingi milioni 222. Sijui Mheshimiwa Waziri anazo taarifa hizi na kama hana, atasaidiaje mkandarasi huyu ambaye ndiye anatengeneza magari ya polisi pale Tabora Mjini alipwe fedha zake?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninazo taarifa anazozisemea Mheshimiwa Mbunge. Nakumbuka nilivyotembelea Mkoa wa Tabora nililetewa jambo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimejibu kwenye swali la msingi, ni utaratibu wa Serikali tulioweka wa kuhakiki kwanza madeni yote. Baada ya kuwa tumeshafanya uhakiki, yale madeni ambayo yamehakikiwa ndiyo yanalipwa kukiwa na kumbukumbu sawa za kazi iliyofanyika na fedha zinazodaiwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maana hiyo, kwa jambo hili ulilolileta Mheshimiwa Mbunge, mhakikishie mtoa huduma huyo kwamba baada ya uhakiki huo ambao ulishafanyika nitawaelekeza watu wangu waweke kipaumbele katika kulipa madeni hayo ili kutokuwakwamisha wazabuni wetu kuweza kuendelea na shughuli zao na kutoa huduma hizo ambazo wametoa hata huko kwetu.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. JAKU HASHIM AYOUB aliuliza:- Kuna mjenzi aliyejenga Vituo vya Polisi kupitia Kampuni iitwayo Al Batna Building Co. Ltd. Vituo alivyojenga ni Kituo cha Polisi Mkokotoni - Unguja na Kituo cha Polisi cha Madungu kilichoko Chakechake Pemba kwa gharama ya shilingi 223,440,000. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kulipa deni hilo tangu 2012 hadi leo hii? (b) Je, Serikali inayo taarifa kwamba mwenye kampuni hiyo aliyejenga vituo hivyo amepata maradhi makubwa huku akihangaika kufuatilia haki yake hiyo bila mafanikio? (c) Je, ni lini Serikali itamtembelea na kumpa pole kwa maradhi hayo mabaya yaliyompata?

Supplementary Question 4

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa Serikali ilitoa ahadi ya kujenga Kituo cha Polisi katika bonde la Yaeda Chini na muda umepita sasa na wananchi wanaibiwa mifugo na kutokea mauaji katika lile bonde.
Je, ni lini sasa Serikali itatekeleza ahadi ya kutengeneza Kituo cha Polisi ya Yaeda Chini? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Flatei jambo hili amelileta mara nyingi sana nami nampongeza kwa hamasa ambayo ameifanya Jimboni kwake kuhusu masuala haya ya ulinzi na usalama. Nilimhakikishia kwamba baada ya Bunge hili la Bajeti kuisha nitazungukia maeneo hayo ambayo kuna uhalifu umekuwa ukijitokeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namuahidi kwamba punde tutakapoanza utaratibu wa ujenzi wa vituo hivyo, eneo lake ni moja ya eneo la kipaumbele kufuatana na uhalifu ambao umekuwa ukijitokeza katika eneo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata kwenye jibu nililojibu la masuala ya magari, Mheshimiwa Flatei pamoja na ndugu yake (pacha yake) Mheshimiwa Issaay, Mbunge wa Mbulu Mjini, alikuja jana tu kusemea mambo ya aina hiyo yakihusisha pia na mambo ya magari.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Flatei pamoja na Mheshimiwa Issaay, niwahakikishie kwamba tutawapa kipaumbele kwenye vituo pamoja na upatikanaji wa magari kufuatana na jiografia ya Majimbo yao na Wilaya yao.