Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Mahakama ya Mwanzo katika Kata ya Upuge, Wilaya ya Uyui, imetelekezwa zaidi ya miaka kumi na kusababisha miundombinu yake kuanza kuharibika. • Je, ni kwa nini Mahakama hii imetelekezwa? • Je, ni kwa nini majengo ya Mahakama hiyo yasitumike na Idara nyingine za Serikali?

Supplementary Question 1

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniruhusu niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kabla ya kuuliza maswali, naomba nieleze yafuatayo, kwa mara ya kwanza nasema Serikali imeshindwa kujibu swali Bungeni.

Hakuna Mahakama, Mahakama haifanyi kazi miaka kumi iliyopita na majengo yote pamoja na nyumba za wafanyakazi milango imetolewa yote na madirisha yamechukuliwa. Mimi nimefanya kazi ya kupeleka umeme pale kwenye Mahakama ile na Kituo cha Afya, hakuna Mahakama pale.
Mheshimiwa Spika, naomba sasa niulize maswali yangu mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, je, ni kwa nini Mahakama ile imetelekezwa?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, ni kwa nini majengo ya Mahakama hiyo yasitumike na Idara nyingine za Serikali?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA - K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, katika utaratibu wa ufanyaji kazi wa kimahakama shughuli kubwa inayofanywa katika Mahakama ni suala zima la usikilizaji wa mashauri na uamuzi. Nakubalina na Mheshimiwa Mbunge kwamba ni kweli Mahakama ya Mwanzo ya Upuge ni chakavu sana, lakini shughuli za kimahakama zinaendelea wakati tunaendelea kujipanga kama Serikali ili baadaye tufanye ukarabati mkubwa wa kuweza kurahisisha ufanyaji kazi wa Mahakama.
Mheshimiwa Spika, tarehe 12/06/2017 kazi za Mahakama zilianza kufanyika kupitia katika baadhi ya ofisi pale katika Halmashauri na mpaka navyozungumza hivi sasa tayari mashauri 50 yalishawasilishwa pale Mahakamani na mashauri 41 yalishafanyiwa uamuzi. Pia pale katika Mahakama ya Upuge yupo Hakimu, mwanzoni tulikuwa tuna Hakimu anaitwa Bumi Mwakatobe ambaye alikuwa anatembelea, lakini sasa hivi yupo Hakimu wa kudumu anaitwa Jacqueline Lukuba ambaye yuko muda wote pale. Kwa hiyo, kuhusu suala la kwamba wananchi wanakosa fursa ya kupata huduma za kimahakama, wananchi wa Wilaya ya Uyui wanapata huduma hii kama ambavyo nimeisema hapo.
Mheshimiwa Spika, nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba nafahamu changamoto tulizonazo kubwa ni kuhusiana na masuala ya bajeti katika Mahakama, lakini tunaendelea na ukarabati wa Mahakama zetu za Mwanzo na Mahakama za Wilaya, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba pindi utaratibu utakapokamilika tutafanya marekebisho makubwa katika Mahakama hii ili wananchi wa Uyui waweze kufaidika na huduma za Mahakama.

Name

Sabreena Hamza Sungura

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALMAS A. MAIGE aliuliza:- Mahakama ya Mwanzo katika Kata ya Upuge, Wilaya ya Uyui, imetelekezwa zaidi ya miaka kumi na kusababisha miundombinu yake kuanza kuharibika. • Je, ni kwa nini Mahakama hii imetelekezwa? • Je, ni kwa nini majengo ya Mahakama hiyo yasitumike na Idara nyingine za Serikali?

Supplementary Question 2

MHE. SABREENA H. SUNGURA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kumekuwa na tatizo kubwa la vyumba vya uendeshaji wa shughuli za Mahakama hususan katika Mkoa wetu wa Dodoma na ukizingatia mkoa huu umeshakuwa Makao Makuu ya nchi.
Mheshimiwa Spika, nataka kujua Serikali ina mkakati gani sasa wa kupanua Mahakama ya Wilaya ya Dodoma kwa maana ya District Court ili sasa ule mlundikano wa Mahakimu watatu kukaa kwenye chumba kimoja na kusikiliza mashauri na kesi nyingi kuchelewa, hususan kwa kesi za watoto wanaobakwa na kulawitiwa na hivyo kuathiri masomo yao uweze kwisha? Ni lini sasa Serikali itafanya upanuzi wa Mahakama hii ili kero hii iweze kuondoka kwa wananchi? Nashukuru. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA - K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimekuwa nikisema mara zote, ni kwamba katika utaratibu tulionao sasa hivi katika utendaji kazi wa kimahakama, tunafanya kazi ya ukarabati wa majengo yetu mengi na upanuzi wa baadhi ya Mahakama. Kwa sababu sasa hivi tumeingia ubia pamoja na Chuo Kikuu cha Ardhi ambapo tunakwenda kujenga katika mfumo mzuri wa Moladi ambao unapunguza gharama, Waheshimiwa Wabunge waendelee kuvuta subira tu, pindi bajeti itakaporuhusu tutaendelea kufanya ukarabati na kupanua Mahakama ili kupeleka huduma za kimahakama zaidi kwa wananchi.