Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA aliuliza:- Manispaa ya Mtwara Mikindani ina migogoro mikubwa ya ardhi inayokaribia kusababisha uvunjifu wa amani:- Je, Serikali ipo tayari hivi sasa kutatua migogoro hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. MAFTAH A. NACHUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kabla sijauliza swali la nyongeza, naomba nifanye masahihisho kidogo. Mheshimiwa Naibu Waziri kasema eneo la Libya ni shamba la chumvi.
Mheshimiwa Spika, mgogoro huu siyo shamba la chumvi ni makazi ya watu ambao nilizungumza wakati wa bajeti hapa kwamba waliamka asubuhi wakakuta wamewekewa beacon kwamba eneo lao limeuza. Siyo shamba la chumvi. Naomba Mheshimiwa Naibu Waziri afanye masahihisho.
Mheshimiwa Spika, sasa naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. La kwanza, Machi 5 mwaka huu wa 2017, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alikuwa Mtwara, pamoja na mambo mengine Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi alikuwepo Mtwara Mjini na alilalamikiwa kuhusu suala la mgogoro wa ulipaji wa fidia katika maeneo ambayo yamechukuliwa mwaka 2013; Mji Mwema. Akaahidi kwamba wananchi wale watalipwa pesa zao mwishoni mwa mwezi Julai, lakini mpaka leo tunapewa taarifa kwamba yule CEO wa UTT amesema hawezi kuwalipa wale watu.
Mheshimiwa Spika, naomba kujua majibu ya Wizara hii kwamba ni kweli inawatendea wananchi hawa wa Mtwara Mjini haki? Kwa sababu tangu mwaka 2013 wamechukuliwa maeneo yao, halafu leo Serikali inasema haiwezi kulipa zile pesa. Naomba tupate ufafanuzi.

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, eneo hili la Libya ambalo ni maarufu kama Mangowela, lakini wale waliochukua lile eneo kwa kuwanyang’anya wananchi eti wanawaeleza wawahamishe, wamebatiza jina wakaita Libya, lakini asili yake ni Mangowela. Sasa naomba kujua, yule mtu ambaye amewanyang’anya wananchi wale ni taasisi inaitwa Azimio na Serikali imemchukulia hatua maeneo mengi. Je, Serikali iko tayari hivi sasa kumnyang’anya ardhi ile ambayo ameidhulumu kwa wananchi na badala yake wananchi wale wameambiwa waende Mahakamani wakati wanajua kabisa kwamba anafanya ujanja kule Mahakamani? Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, kwanza niseme tu nilikuwepo huko mwezi uliopita na bahati nzuri nilionana na uongozi wa mkoa pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mtwara- Mikindani.
Mheshimiwa Spika, sasa wale kama wameshindwa kulipa au wameshindwa kuchukua, hatuwezi kuendelea kuwalazimisha kwa sababu ile ardhi ni mali. Kama wameshindwa, maana yake ni kwamba mnunuzi yeyote ambaye anataka kuwekeza pale, anaruhusiwa kuja. Wale wamesha-declare kwamba hawawezi na hatuwezi kuwalazimisha. Kama wame-declare hawawezi, maana yake ni kwamba tunaangalia utaratibu mwingine na hili liko chini ya Mkuu wa Mkoa analisimamia.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Wizara yangu inasubiri wao wenyewe wahusika kwa maana ya Manispaa pamoja na Mkoa husika kwamba watakuja na mpango upi au watakuja na utaratibu upi ambao watakuwa wamejiwekea? Kwa maana ya UTT, hawawezi tena na wamesha-declare kwamba hawawezi kuchukua.
Mheshimiwa Spika, suala la pili analolizungumzia, lipo Mahakamani na siwezi kulijadili hapa na ndiyo maana nimetaja na namba ya shauri lilipo Mahakamani. Tusubiri shauri hilo liishe ndiyo waweze kulileta hapa.