Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Halmashauri za Wilaya ya Nkasi na Sumbawanga Mjini hazina Hospitali ya Wilaya; wanawake na watoto wanapata shida ya matibabu wakati wa kujifungua na huduma za watoto. Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali katika Wilaya hizo?

Supplementary Question 1

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini maswali mawili ya nyongeza ni kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa Sera ya Afya inasema itajenga zahanati kila kijiji na pia itajenga vituo vya afya kila kata na pia itajenga Hospitali za Wilaya kila wilaya. Je, ni lini sera hii itatekelezwa kikamilifu?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa afya ni kipaumbele cha mwanadamu hasa kwa mama na mtoto, je, Serikali haioni umuhimu wa kuupa kipaumbele Mkoa wa Rukwa kwa kuwa hauna Hospitali ya Wilaya hata moja? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli sera yetu inatueleza hivyo na ndiyo maana ukiangalia mchakato wa Serikali kwa kushirikiana na ninyi Waheshimiwa Wabunge, wananchi na wadau mbalimbali mnaona ni jinsi gani tunajitahidi kwa kadri iwezekanavyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli naomba nitoe pongezi zangu za dhati, katika maeneo mbalimbali nilikopita nimekuta Wabunge wengi sana na wengine wakitumia Mfuko wa Jimbo na kuungana nguvu na wananchi katika suala zima la ujenzi wa zahanati na vituo vya afya. Nilishawahi kuzungumza hapa siku za nyuma kwamba katika bajeti ya mwaka 2017/2018 tumetenga shilingi bilioni 251 lakini katika hizo shilingi bilioni 68 ni kwa ajili ya ku-top up shughuli hizo za ujenzi wa zahanati huko tunakokwenda kumalizia haya maboma.
Kwa hiyo, mpango wa Serikali ni kuhakikisha kwamba tunafanya kila liwezekanalo sera hii iweze kutekelezwa. Najua kila jambo lina time frame, katika miaka hii mitano mtaona mabadiliko makubwa sana katika sekta ya afya.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini mahsusi katika Mkoa wa Rukwa, ni kweli kuna changamoto kubwa sana ndiyo maana Serikali tukaona katika Halmashauri zake kutokana na changamoto lazima tuboreshe kwanza vituo vya afya vilivyopo. Leo hii kwa kaka yangu Mheshimiwa Ally Keissy kule Nkasi amepigia kelele sana Kituo chake cha Kirando, tumefanya utaratibu tunaenda kujenga theatre na majengo mengine. Ukienda pale Sumbawanga DC halikadhalika kuna suala la ujenzi wa Kituo cha Afya cha Mirepa lakini hilo tutafanya kwa kadri iwezekanavyo na ndiyo maana katika Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo hivi sasa tumepeleka karibia shilingi milioni 340 kwa ajili ya zoezi la ujenzi wa Hospitali ya Wilaya.
Kwa hiyo, ni jukumu la Serikali kuhakikisha Mkoa wa Rukwa nao uweze kujengewa miundombinu ili wananchi wa kule waweze kupata huduma nzuri za afya.

Name

Omary Ahmad Badwel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Halmashauri za Wilaya ya Nkasi na Sumbawanga Mjini hazina Hospitali ya Wilaya; wanawake na watoto wanapata shida ya matibabu wakati wa kujifungua na huduma za watoto. Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali katika Wilaya hizo?

Supplementary Question 2

MHE. OMARY A. BADWEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii ili nami niulize swali moja dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Wilaya ya Bahi nayo ni miongoni mwa Wilaya hizo kadhaa ambazo hazina Hospitali ya Wilaya na kumekuwa na matatizo mengi sana, lakini pale Bahi tuna kituo cha afya ambacho hakijafikia level ya upasuaji.
Je, Mheshimiwa Waziri anaweza kuwaambia wananchi wa Bahi kwamba labda upo mpango wowote mzuri wa kusaidia kile Kituo cha Afya Bahi ili angalau hatua ya upasuaji hasa akina mama na huduma zingine muhimu ziwepo? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nimefika mara mbili kwenye Halmashauri ya Bahi na juzi juzi tulikuwa na Mheshimiwa Mbunge jimboni kwake takribani mwezi mmoja na nusu na bahati mbaya Bahi hawana Hospitali ya Wilaya wala vituo vya vya afya na kile kimoja kiko katika hali mbaya. Kutokana na maombi ya Mbunge tayari tumeshapeleka shilingi milioni 500 ndani ya wiki hii. Tunaenda kukiimarisha Kituo cha Afya cha Bahi, tunakijengea miundombinu ya upasuaji na maabara. Nia yetu ni kwamba Bahi pale huduma zote za msingi ziweze kupatikana kwa ukaribu zaidi. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge, ombi lako limekubaliwa na Serikali na tunalifanyia kazi. Lengo letu ni kwamba wananchi wa Bahi wapate huduma nzuri kama wananchi wengine.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Halmashauri za Wilaya ya Nkasi na Sumbawanga Mjini hazina Hospitali ya Wilaya; wanawake na watoto wanapata shida ya matibabu wakati wa kujifungua na huduma za watoto. Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali katika Wilaya hizo?

Supplementary Question 3

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa kuwa ni zaidi ya miaka 53 toka nchi imepata uhuru sehemu yenye hadhi ya mkoa kama Mkoa wa Rukwa hatuna Hospitali ya Wilaya hata moja. Serikali haioni umuhimu sasa wa kuondoa aibu hiyo angalau hata wilaya mbili zipate hospitali ya wilaya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, nafahamu, Wabunge wote wa Rukwa wakisimama hapa ajenda kubwa ni afya kwa sababu ni kweli siyo jambo la uongo. Ndiyo maana hata nilivyokuwa nikimjibu Mheshimiwa Bupe swali lake lile la msingi la kwanza nilizungumza kwa ujumla wake. Ndiyo maana tumesema mipango ya Serikali katika Halmashauri ya Kalambo sasa hivi kati ya shilingi bilioni 1.4 tuliyoitenga tumepeleka karibu shilingi milioni 340 lakini hili tutalisimamia vizuri katika mwaka huu wa fedha angalau Kalambo ujenzi uende kukamilika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hali kadhalika ukiangalia pale Sumbawanga DC hali ni mbaya vilevile, lakini hivi sasa katika Kituo cha Afya cha Mwimbe tumepeleka fedha karibuni shilingi milioni 500 lakini kule Nkasi tumeshaanza kushughulikia matatizo yake. Jukumu hili lote ni la Serikali. Naomba muwe na imani kwamba Serikali hii ya Awamu ya Tano, commitment yake ile mikoa ambayo ina changamoto kubwa sana tutafanya kila liwezekanalo kuhakikisha wananchi wa mikoa hiyo wanapatiwa huduma.
Kwa hiyo, Mheshimiwa dada yangu naomba nikusihi kwamba Serikali hii iko nanyi Wabunge wa Rukwa wala msiwe na hofu, tutajitahidi kufanya kila liwezekanalo kuhakikisha huduma ya afya inapatikana vizuri zaidi.

Name

Halima Abdallah Bulembo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Halmashauri za Wilaya ya Nkasi na Sumbawanga Mjini hazina Hospitali ya Wilaya; wanawake na watoto wanapata shida ya matibabu wakati wa kujifungua na huduma za watoto. Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali katika Wilaya hizo?

Supplementary Question 4

MHE. HALIMA A. BULEMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. RCC ya Mkoa wa Kagera ilishatoa kibali kuhusu ujenzi wa Hospitali ya Wilaya ya Karagwe, lakini suala hilo linakwamishwa na Wizara ya TAMISEMI kwa sababu haitaki kutoa usajili ili hospitali hiyo itengewe bajeti na ujenzi uanze mara moja. Je, ni lini Wizara ya TAMISEMI itaamua kutoa usajili huo ili ujenzi uanze mara moja ili kuokoa akina mama na watoto?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la dada yangu Mheshimiwa Halima Bulembo na kwanza nimpe hongera sana kwa kazi kubwa aliyofanya katika sekta hii ya afya, hongera sana. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, bahati nzuri nimefika Karagwe, bahati nzuri pia anafahamu hata pale Karagwe kulikuwa hakuna DMO. Sisi TAMISEMI ndiyo tukamchukua kijana mmoja anaitwa Sobo tukampeleka pale, ni daktari mzuri sana wa upasuaji. Hata Karagwe pale tulikuwa hatuna centre ya Serikali ya kufanya upasuaji sasa hivi upasuaji pale Karagwe katika kituo cha afya umeanza.
Si hivyo tu, lilivyotokea tetemeko la ardhi, Serikali imefanya juhudi kubwa sana kuboresha kile kituo cha afya na hivi sasa tunapeleka takribani shilingi milioni 500 kufanya wananchi wa Karagwe wanapata huduma nzuri ya Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwahakikishie kwamba katika ofisi yetu hakuna kibali kitakachokwama isipokuwa wakati mwingine ni changamoto ya bajeti. Tunachukua mawazo yote ya Wabunge wa Karagwe, tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo kutekeleza vipaumbele vyenu mlivyoweka katika mpango wa bajeti maana siyo suala la kibali, kibali sisi hamna tatizo isipokuwa ni pamoja na kuona ni jinsi gani tutenge bajeti kuhakikisha tunajenga hospitali ya wilaya.
Kwa hiyo, ni jukumu la Serikali, tutafanya kila liwezekanalo wananchi wa Karagwe kama tunavyofanya sasa tutaendelea kufanya hivyo ili mradi huduma ya afya ipatikane vizuri katika Wilaya ya Karagwe na Halmashauri yake kwa ujumla. (Makofi)

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Halmashauri za Wilaya ya Nkasi na Sumbawanga Mjini hazina Hospitali ya Wilaya; wanawake na watoto wanapata shida ya matibabu wakati wa kujifungua na huduma za watoto. Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali katika Wilaya hizo?

Supplementary Question 5

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Tanganyika ni miongoni mwa wilaya mpya ambazo hazina huduma ya hospitali ya wilaya. Kwa nyakati tofauti, Serikali imekuwa ikiahidi Kituo cha Afya kijiji cha Majalila ambako ni Makao Makuu ya Wilaya. Nilikuwa nataka kujua kauli ya Serikali, je, Kituo kile cha Majalila, ni lini kitaanza kupewa fedha na hatimaye kuanzisha ujenzi wa kituo cha afya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Wilaya ya Tanganyika imegawanyika kutoka Mpanda na mimi Mbunge nafahamu tulifika pale kwake ni kweli kuna tatizo kubwa sana. Kwa mfano wananchi wanaotoka Mwese wakija Mpanda Mjini ni tatizo na tulifika pale Majalila ambapo Makao Makuu ya Wilaya ile inataka ijengwe, nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hivi sasa tumetenga shilingi milioni 500 kwa ajili ya Halmashauri yako ya Wilaya. Juzi nilikuwa naongea na Mkurugenzi wako wa Mpanda DC kuangalia jinsi gani tutafanya.
Kwa hiyo, kuna shilingi milioni 500 tunawaletea na hii sisi tunasema kama ni kingiambago tu, ni fedha ya kwanza tutatoa fedha nyingine kwa ajili ya kununua vifaa ambayo jumla yake itakuwa karibuni shilingi milioni 720. Kwa hiyo, naomba niwahakikishie wananchi wa Tanganyika hili ni jukumu la Serikali kuwafikia watu wote hata ndugu yangu wa Kakonko tulifanya jambo hili kwa sababu siku ile tuliyofika shida ilikuwa kubwa. Hii ni kazi ya Serikali na itafanya kazi kila mahali kwa manufaa ya wananchi wake wa Tanzania.