Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantakaje Haji Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Bububu

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA aliuliza:- Kumekuwa na wimbi la mabweni na hata shule kuungua moto, hususan Tanzania Bara. Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti hali hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, je, ni vikundi ngapi zilizochukuliwa hatua mpaka sasa?
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri, je, ni vikundi ngapi zilizochukuliwa hatua mpaka sasa?
Mheshimiwa Naibu Spika, samahani ni shule ngapi zilizochukuliwa hatua mpaka sasa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda kumshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa sababu ameonesha concern kubwa ya suala zima la janga la moto katika maeneo yetu. Hili nimelisema katika jibu langu la msingi takribani shule 29.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la chanzo nani alisababisha imeonekana maeneo mbalimbali ni hitilafu ya umeme, lakini bado hatujabaini hasa watu mahsusi ambao wameshughulika katika suala la kuhujumu miundombinu hii na ndiyo maana tumeunda Kamati hizi shirikishi katika jamii zetu hasa katika ngazi za shule, lengo ni kuzuia baadae watu watakapobainika basi tuweze kuwachukulia hatua katika maeneo hayo.

Name

Wilfred Muganyizi Lwakatare

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Bukoba Mjini

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA aliuliza:- Kumekuwa na wimbi la mabweni na hata shule kuungua moto, hususan Tanzania Bara. Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti hali hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. WILFRED M. LWAKATARE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Ningependa kumuuliza Mheshimiwa Waziri na kwa niaba ya Serikali, kwamba matukio ya moto ambayo yanatokea katika shule, yamekuwa pia yakitokea katika maeneo mbalimbali yakisababisha maafa makubwa. Lakini tatizo kubwa ambalo limeonekana kuchangia maafa kuwa makubwa ni pale ambapo vikosi vyetu vya Zimamoto vinapofika kwenye eneo la tukio na vikishafika pale magari yanaonekana yanakuja tu, labda kuja kutembea yanakuwa hayana maji na wala hawana vifaa, matokeo yake wakati mwingine wamekuwa wakiambulia kipigo au matusi kutoka kwa wananchi wenye hasira kali.
Je, Serikali inasemaje juu ya hili na wamejipangaje kuliondoa?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kunachangamoto nyingi ambazo panatokea maendeleo na zenyewe zinajitokeza. Kwa mfano, miji inapokua majengo yanapojengwa, kuna maeneo mengine yanakuwa hayajatoa provision za magari ya kisasa kuweza kufanya kazi ile ya zimamoto.
Kwa hiyo, sasa hivi tunashirikiana na Wizara zingine zinazohusika ili tuweke provison hizo ambazo zitawezesha wenzetu wa zimamoto waweze kufanya hivyo. Lakini pia hilo jambo alilolisema lilishajitokeza maeneo mengi tumechukua hatua kuweza kuhakikisha kwamba, magari yanakuwa yako standby na vitendea kazi vyote vinavyotakiwa kwa ajili ya kwenda kuzima moto ili wasije wakafika kwanza halafu wakajikuta kwamba walikuwa na upungufu wa vitendeakazi vinavyotakiwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumelizingatia na hata tulivyopitisha kwenye bajeti tulilielezea jinsi ambavyo tunakiunda upya kikosi kile kiweze kuwa na vitendeakazi vinavyostahili kwa ajili ya kukabiliana na matukio ya aina hiyo aliyoyasema. (Makofi)

Name

Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA aliuliza:- Kumekuwa na wimbi la mabweni na hata shule kuungua moto, hususan Tanzania Bara. Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti hali hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kwa nini shule za Serikali hawaweki provision ya kuwa na fire extinguisher ambayo inaweza ikatumika mara tu kama huduma ya kwanza wakati magari ya zimamoto yanaposubiriwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ukiangalia kesi hizi za majanga ya moto na siyo shuleni peke yake hata katika maeneo mbalimbali, ni kwa sababu katika kipindi kirefu tulikuwa tumejisahu kuweka fire extinguisher. Ndiyo maana sasa tumetoa maelekezo katika shule zetu mbalimbali miongini mwa vitu ambavyo tunatakiwa tuviweke viwe vya msingi ni suala la fire extinguisher. Hata hivyo, katika ujenzi wa mabweni yetu, zamani mabweni yalikuwa yakifunguka yanafungukia ndani, hata janga la moto likitokea watoto wanavyogombania kufungua mlango kumbe ndiyo wanazidi kuufunga.
Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo maana katika suala la specification tukasema na mabweni yetu sasa hivi yote milango inafungukia kwa nje ili kwamba inapotokea hatari ya moto basi watoto wakiwa wanatoka mlangoni, iwe ni rahisi sana kuweza katoka katika eneo lile pindi janga la moto linapotokea.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni agizo letu na ninaomba niwasihi sana ni waagize Wakurugenzi wote katika Halmashauri zetu kuhakikisha katika maeneo ya shule zetu zote zinakuwa na fire extinguisher as a back up strategy, endapo moto unapotokea, wakati unasubiria kupata magari ya kuzima moto yaje, tuwe na mbinu mbadala wa kuweza kudhibiti moto mapema zaidi.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA aliuliza:- Kumekuwa na wimbi la mabweni na hata shule kuungua moto, hususan Tanzania Bara. Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti hali hiyo?

Supplementary Question 4

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi nami niulize swali.
Kwa kuwa ukiangalia shule nyingi zilizoungua, chanzo kikuu huwa ni vibatari au mshumaa, hii ni kwa sababu ya kukosekana kwa umeme; kwa kuwa Serikali imeshatoa maelekezo kwamba kila sehemu yenye taasisi kama shule na sehemu nyingine muhimu umeme upite, lakini mpaka leo baadhi ya sehemu wamekosa haki hiyo ya kupelekewa umeme. Je, Serikali inasemaje?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tu kwamba shule zote katika Halmashauri zote kwa nchi nzima tumeshaanza sasa kuchukua stock taking kuona shule za msingi na sekondari ambazo zimekamilika ili zipelekewe umeme kupitia mradi wa REA ambao umeshaanza.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge na nimhakikishie kwamba Halmashauri zote kwa kutumia nafasi hii, Wakurugenzi wote ambao hawajafanya hivyo niwaagize wafanye hivyo ili mradi utakapofika waweze kupitishiwa umeme haraka sana.

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA aliuliza:- Kumekuwa na wimbi la mabweni na hata shule kuungua moto, hususan Tanzania Bara. Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti hali hiyo?

Supplementary Question 5

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona.
Mkoa wa Arusha ni miongoni mwa Mikoa iliyoathirika na tukio hili la uchomaji wa shule za sekondari, waathirika wakubwa ni wanafunzi. Ningependa tu Waziri atufahamishe kwamba ni hatua gani za haraka zinazochukuliwa na Serikali katika kuhakikisha kwamba wanafunzi wanaendelea na masomo badala ya kuziacha shule hizo kwa muda mrefu pasipo kupewa msaada wowote na badala yake ni wananchi ndiyo wanaojitolea na wasamaria wema. Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Mkoa wa Arusha ni miongoni mwa Mikoa ambayo ilipata janga la moto. Tukumbuke kwamba janga hili liliikumba maeneo mbalimbali. Bahati nzuri unafahamu wewe ni mwenyeji wa Mkoa wa Mbeya, shule yetu ya Iyunga, Mbeya kulikuwa na sintofahamu kubwa sana, lakini ni nini tumekifanya katika maeneo mbalimbali. Tulichokifanya kama Serikali si kwamba Serikali ilikuwa inaangalia hivi na kuacha, hapana. Tumefanya harakati maeneo mbalimbali hasa kutumia Halmashauri husika na ngazi Mikoa na Serikali Kuu. Ndiyo maana wanaofahamu kama mashahidi katika Mkoa wa Mbeya, shule ya Iyunga na mimi nilikuwepo site moto ule ulivyokuwa umewaka pale, tumefanya kazi kubwa sana shule yote ya Iyunga pale imebadilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, shule ya Mpwapwa kwa Mzee wangu Mheshimiwa Lubeleje nimefika pale site hivi sasa bweni tunamaliza kulipaua. Pia maeneo mbalimbali harakati hizi zinaendelea, lakini tunaenda awamu kwa awamu, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Amina Mollel kwamba Kamati yetu ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Arusha bahati nzuri wakati moto unawaka Monduli nilikuwepo pale. Nilienda na nilifanya tathmini hiyo, lengo kubwa ni kwamba tutajitahidi kwa kadri iwezekanavyo sehemu yenye mapungufu yote tutashirikiana na jamii husika kuondoa tatizo hili la watoto wetu ili wasikose maeneo ya kukaa.