Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER M. MMASI aliuliza:- Kupitia fursa ya ujenzi wa bomba la mafuta Mkoani Tanga, ni dhahiri kwamba vijana takribani 15,000 watapata ajira kwenye mradi kwa upande wa Tanzania:- (a) Je, Serikali imejipangaje kuona kuwa vijana wa Kitanzania wanapata ajira katika soko la Tanzania kupitia fursa hii ya uwekezaji? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuingiza mtaala wa mafuta na gesi katika mitaala ya VETA ili kuwajengea uwezo, maarifa na ujuzi vijana wa Kitanzania katika sekta hiyo muhimu?

Supplementary Question 1

MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa mradi wa bomba la mafuta kutoka Hoima (Uganda) kuja Bandari ya Tanga nchini Tanzania ulitarajiwa kuanza mwezi Juni, 2017. Kwa kuwa pia majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ni kwamba Serikali itakuwa tayari kuwaandaa vijana wetu kupitia mitaala ya oil and gas kwenye Vyuo vya VETA mnamo mwaka 2018. Je, Serikali kwa kufanya hivi haioni ni sawa kabisa na kuweka rehani ajira ya kijana wa Kitanzania hususan vijana wanaotoka katika Mkoa wa Tanga?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, mchakato wa uchimbaji, uchanjuaji na uchakataji wa zao la oil and gas Mikoani Lindi na Mtwara ulitarajia kuanza mwaka 2013, lakini hakuanza kutokana na sababu za ndani ya Serikali na kubwa ikiwa ni ukamilishwaji wa local content policy pamoja na msamaha wa kodi. Nini kauli ya Serikali kwa vijana wahitimu kwa nchi ya Tanzania hasa ukiangalia kwamba vijana wengi wanahangaika kutafuta kazi pasipokuwa na imani yoyote? Ahsante sana.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimpongeze Mheshimiwa Mmasi, tumekuwa na yeye tangu mwaka 2013 katika jitihada za kufungua mafunzo kwa VETA kwa wanafunzi wa oil and gas. Kwa hiyo hongera sana Mheshimiwa Mmasi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na maswali yake haya mawili, la kwanza, Serikali haioni kwamba ni muhimu sasa kuwapatia mafunzo hasa wanafunzi wa VETA kwa oil and gas. Ni kweli kabisa upo umuhimu na mwaka 2012/2013 kama nilivyosema, tulianza kutoa mafunzo hayo kwa ajili ya kuwafundisha vijana wetu wa VETA Lindi na Mtwara kwa ajili ya uchomeleaji, ufundi sanifu pamoja na theories za kawaida za utafiti wa kuchimba na kutafiti mafuta na gesi hapa nchini. Kwa hiyo, tunaona umuhimu Mheshimiwa Mmasi na tumeshafika hatua nzuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, matarajio ya mpango wa Serikali, kweli kabisa mwaka 2018 tunatarajia taratibu zote za taaluma ili kuingiza sasa mtaala katika Vyuo vya VETA kwa upande wa mafuta na gesi itafika sasa muda muafaka hasa kwa VETA ambavyo ni vyuo vipya ukiondoa vile vyuo ambavyo vimeshaanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninavyowasiliana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, tumefika hatua nzuri, Serikali ya Norway pamoja na Serikali yetu itatenga shilingi milioni 20 kwa ajili ya kukamilisha hatua hii. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mmasi, tutakapofika katika hatua hiyo tutashirikiana pamoja tuone namna ya kuwapatia vijana wetu mafunzo haya ambayo ni muhimu sana kwa ustawi wa nchi yetu.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. ESTER M. MMASI aliuliza:- Kupitia fursa ya ujenzi wa bomba la mafuta Mkoani Tanga, ni dhahiri kwamba vijana takribani 15,000 watapata ajira kwenye mradi kwa upande wa Tanzania:- (a) Je, Serikali imejipangaje kuona kuwa vijana wa Kitanzania wanapata ajira katika soko la Tanzania kupitia fursa hii ya uwekezaji? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuingiza mtaala wa mafuta na gesi katika mitaala ya VETA ili kuwajengea uwezo, maarifa na ujuzi vijana wa Kitanzania katika sekta hiyo muhimu?

Supplementary Question 2

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona ili niweze kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa kuwa bomba hili la mafuta ghafi linaishia Bandari ya Tanga, je, Serikali imejipangaje kuona kuwa vijana wa Kitanzania hasa vijana wa Mkoa wa Tanga wanapata ajira hii katika soko la Kitanzania kupitia fursa hii ya uwekezaji?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nimhakikishie Mheshimiwa Shekilindi, hili bomba la mafuta kutoka Hoima (Uganda) kuja Tanga (Tanzania) lina urefu mpana sana, lina jumla ya kilometa 1,443, lakini sehemu kubwa ya bomba hilo ambayo ni urefu wa kilometa 1,047 ni za hapa Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, bomba hilo litapita karibu mikoa sita ya Kagera, Geita, Shinyanga, Dodoma hadi Tanga, kwa hiyo ni manufaa makubwa sana. Hivyo basi, ipo fursa kubwa sana kwa bomba hili kutoa ajira kubwa kwa Watanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Shekilindi na wananchi wa Tanga kwamba ajira na fursa nyingi sana za kazi zitapatikana. Sambamba na hayo, tunawasiliana kwa karibu sana na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji ili kutoa fursa nzuri sasa kwa Watanzania kuwekeza kwa kutumia fursa hiyo ya bomba la Hoima hadi Bandari ya Tanga.

Name

Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTER M. MMASI aliuliza:- Kupitia fursa ya ujenzi wa bomba la mafuta Mkoani Tanga, ni dhahiri kwamba vijana takribani 15,000 watapata ajira kwenye mradi kwa upande wa Tanzania:- (a) Je, Serikali imejipangaje kuona kuwa vijana wa Kitanzania wanapata ajira katika soko la Tanzania kupitia fursa hii ya uwekezaji? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuingiza mtaala wa mafuta na gesi katika mitaala ya VETA ili kuwajengea uwezo, maarifa na ujuzi vijana wa Kitanzania katika sekta hiyo muhimu?

Supplementary Question 3

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa kuwa ajira hizi zimekuwa zikitajwa kwa ujumla wake, je, ni lini Serikali itatengeneza mchanganuo ili kupata uwakilishi mzuri kwa pande zote mbili za Muungano?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ni lini, kinachofanyika sasa tupo katika hatua ya pili, hatua ya kwanza tumekamilisha utambuzi wa eneo ambapo bomba litapita. Hatua ya pili, tunakamilisha mazungumzo ili kuainisha maeneo na fursa muhimu kwa nchi zetu mbili lakini pia kwa nafasi za Tanzania Bara na Tanzania Zanzibar kwa masuala ya mafuta. Kwa sababu suala la ajira siyo la Muungano lakini fursa ziko palepale, utaratibu utakamilika baada ya majadiliano ndani ya mwaka huu lakini hatua ya pili itakuwa kuainisha fursa. Kwa hiyo, tutakapofikia hatua hiyo Mheshimiwa Mbunge tutawasiliana ili tuone namna ya kukamilisha na kuzinufaisha pande zote za Muungano.