Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Susan Limbweni Kiwanga

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. SUSAN L. KIWANGA aliuliza:- Katika Jimbo zima la Mlimba hakuna Mahakama hata moja, jambo linalosababisha mahabusu kupelekwa Jimbo la Kilombero umbali wa takriban kilometa 260 kuhudhuria mahakama:- Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama katika Jimbo la Mlimba ili kuwaondolea wananchi adha ya kusafiri umbali mrefu katafuta huduma ya Mahakama?

Supplementary Question 1

MHE. SUSAN L. KIWANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ni kweli kwamba kuna mpango wa kujenga Mahakama pale Mlimba, lakini sijui itachukua muda gani; ingawa hapo anaposema kwamba ni Mahakama, ni kibanda tu cha TAZARA wameazima na mara nyingi Mahakimu huwa hawapo muda mrefu sana. Labda kwa sababu hakuna Mahakama ambayo inatambulika rasmi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna Mahakama eneo la Utengule, kule alikotoka Chief Kiwanga, kwenyewe hakuna kabisa Hakimu. Kwa hiyo, watu wanapata shida sana katika kupata huduma. Je, pamoja na kuwa na mpango wa Serikali kujenga hiyo Mahakama hapo Mlimba ambapo ni Makao Makuu ya Jimbo, Serikali iko tayari sasa kupeleka Mahakimu kwenye maeneo ambayo kuna Mahakama lakini hakuna Mahakimu? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu Waziri huyu ameteuliwa hivi karibuni, je, yuko tayari sasa kufanya ziara kwenye Jimbo la Mlimba kuangalia hali halisi na miundombinu ili anapokwenda kwenye bajeti tuone kwamba anaikumbuka Mlimba na kuiwekea mafungu ambayo yanastahili ili wananchi wapate haki zao? (Makofi)

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana na ombi lake la kuhakikisha kuwa Mahakama za Mwanzo katika Wilaya ya Kilombero, yaani Jimbo la Mlimba na Kilombero zinapata Mahakimu ili kusogeza huduma ya utoaji haki katika eneo hilo; hasa tukizingatia kuwa Wilaya ya Kilombero kama ilivyo Wilaya ya Loliondo, Kiteto, Manyoni ni Wilaya ambazo kijiografia maeneo yake ni makubwa sana na umbali ni mkubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naamini kabisa Wizara pamoja na Mahakama tutahakikisha Wilaya za aina hiyo, yaani Kilombero, Kiteto Loliondo na Manyoni, zinapata aina ya msisitizo katika kuhakikisha kwamba Mahakama zake za mwanzo zina Mahakimu wengi ili kupunguza umbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni dhahiri kabisa unapotoka Mlimba mpaka kwenda Kilombero kilometa 260 ni mikoa kwa sehemu nyingine. Kwa hiyo, tutalizingatia kabisa katika kuhakikisha kwamba Mahakama hizo kutegemea na Ikama iliyotolewa na Serikali, zinapata Mahakimu wa mwanzo wengi ikiwa ni pamoja na Utengule alipotoka Chifu Kiwanga.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la ziara ya kwenda Mlimba, naipokea kwa mikono miwili; huu ni wakati wa mavuno; kwa hiyo, nitapata mchele na pepeta; siyo kama takrima, lakini kama ukarimu wa watu wa Mlimba.(Makofi)

Name

Issa Ali Abbas Mangungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. SUSAN L. KIWANGA aliuliza:- Katika Jimbo zima la Mlimba hakuna Mahakama hata moja, jambo linalosababisha mahabusu kupelekwa Jimbo la Kilombero umbali wa takriban kilometa 260 kuhudhuria mahakama:- Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama katika Jimbo la Mlimba ili kuwaondolea wananchi adha ya kusafiri umbali mrefu katafuta huduma ya Mahakama?

Supplementary Question 2

MHE. ISSA A. MANGUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Hali inayojitokeza Mlimba ni sawasawa na inavyojitokeza Jimbo la Mbagala. Niliwahi kuuliza swali la msingi, nikaambiwa kwamba mwaka huu watajenga Mahakama katika Jimbo la Mbagala, lakini tatizo ni viwanja. Tayari tumeshapata viwanja eneo la Kijichi na Chamazi. Je, ni nini tamko la Serikali kuhusu kujenga Mahakama katika Jimbo la Mbagala? (Makofi)

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, tuna mpango wa kujenga Mahakama ya Mwanzo huko Temeke; na sasa tutahakikisha tunajua Temeke sehemu gani?Hata hivyo, nimelipokea suala la Mbagala, tutalifanyia kazi na kuona hii Mahakama ya Mwanzo ambayo imepangwa kujengwa Temeke mwaka 2017/2018 itakuwa sehemu ipi na kama siyo Mbagala, basi suala la Mbagala tutalichukulia kwa umakini unaostahili.

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. SUSAN L. KIWANGA aliuliza:- Katika Jimbo zima la Mlimba hakuna Mahakama hata moja, jambo linalosababisha mahabusu kupelekwa Jimbo la Kilombero umbali wa takriban kilometa 260 kuhudhuria mahakama:- Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama katika Jimbo la Mlimba ili kuwaondolea wananchi adha ya kusafiri umbali mrefu katafuta huduma ya Mahakama?

Supplementary Question 3

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa Wilaya ya Mlele haina Mahakama kabisa, ni lini watajenga Mahakama ya Wilaya ya Mlele? (Makofi)

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mipango iliyopo katika Mahakama, Wilaya ya Mlele imepangwa kujengewa Mahakama ya Wilaya mwaka 2017/2018 na nimalizie hapo hapo na Wilaya za Mpanda na Tanganyika mwaka 2019/2020. (Makofi)

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. SUSAN L. KIWANGA aliuliza:- Katika Jimbo zima la Mlimba hakuna Mahakama hata moja, jambo linalosababisha mahabusu kupelekwa Jimbo la Kilombero umbali wa takriban kilometa 260 kuhudhuria mahakama:- Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama katika Jimbo la Mlimba ili kuwaondolea wananchi adha ya kusafiri umbali mrefu katafuta huduma ya Mahakama?

Supplementary Question 4

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Jimbo la Lupembe, Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ina Mahakama moja iliyopo Lupembe na Mahakama hii jengo lake ni chakavu sana na ina nyufa nyingi, lakini pia ipo kwenye hifadhi ya barabara. Tayari wananchi wameshatoa eneo kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Mahakama hii? Ahsante sana.

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, maadam wameshapata ardhi na wameshachukua hatua za mwanzo, namwomba Mheshimiwa Hongoli tuonane ili nijue taratibu nyingine zinazostahili kufuatwa ili tukamilishe jambo hilo na Mahakama iweze kuanza kujengwa mapema iwezekanavyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Hongoli tuonane ili nipate taarifa hizo ili nami nizifikishe kwa Mtendaji wa Mahakama halafu tuone tunafanya vipi kwa sababu tayari maandalizi ya awali ya kiwanja na naamini kina hati; kama ni hivyo, basi hatua zinazofuata zitakuwa ni rahisi zaidi.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. SUSAN L. KIWANGA aliuliza:- Katika Jimbo zima la Mlimba hakuna Mahakama hata moja, jambo linalosababisha mahabusu kupelekwa Jimbo la Kilombero umbali wa takriban kilometa 260 kuhudhuria mahakama:- Je, ni lini Serikali itajenga Mahakama katika Jimbo la Mlimba ili kuwaondolea wananchi adha ya kusafiri umbali mrefu katafuta huduma ya Mahakama?

Supplementary Question 5

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na nina swali moja la nyongeza. Najua kwenye Wizara Mheshimiwa Waziri hana muda mrefu sana, lakini Mahakama ya Mkoa wa Manyara iliyojengwa pale Babati Mjini, Mtaa wa Negamsi ni Mahakama ya Mwanzo, ya Wilaya, mpaka ya Mkoa, kuna baadhi ya wananchi hawajalipwa fidia zao, mpaka leo wameachia eneo hilo kwa Mahakama. Ni miaka 14 sasa tangu 2004. Pamoja na ugeni wake katika Wizara, je, yuko tayari kufuatilia kwa karibu ili wananchi wale, ndugu zake, wajomba zake wapate fidia zao?

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakubaliana kabisa na maoni aliyoyatoa na nitafuatilia kuona fidia ya hao watu ambao walitoa ardhi yao kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama hizo, linafanyiwa kazi haraka. Nitalifuatilia kwa karibu na najua watu wengine wanaweza kuwa wanashangaa ukaribu huo umetoka wapi? Ni kwa sababu katika mishipa yangu pia nina damu ya Kibarbaigi.(Kicheko)