Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Serikali imekuwa na dhamira ya dhati ya kuboresha maslahi ya Watumishi hususan Walimu kwa kutoa nyaraka mbalimbali ikiwemo Waraka wa Utumishi wa Serikali Na. 3 wa tarehe 20/10/2014 unaohusu mishahara na Posho ya Madaraka kwa Viongozi wa elimu (Responsibility Allowance):- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kutekeleza waraka huo? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa Posho ya Kufundishia (Teaching Allowance) ili kuleta ufanisi wa kazi?

Supplementary Question 1

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, naishukuru Serikali kwa hatua hiyo. Naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; tangu mwaka 2016 mpaka sasa hakuna ongezeko lolote la mshahara kwa watumishi. Serikali inatoa tamko gani kwa watumishi hawa ambao wamekuwa na moyo mkubwa sana wa kujitolea?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; tangu mwaka 2016 mpaka sasa hakuna kupandishwa daraja kwa mtumishi yeyote hususan Mwalimu. Je, Serikali itakuwa tayari sasa kulipa malimbikizo ya mshahara kwa Mtumishi ambaye alistahili kupanda mwaka 2016 mpaka sasa? (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, tukifanya rejea ya takriban siku mbili, Mheshimiwa Waziri anayehusika na mambo ya Utumishi (Waziri wa Utumishi na Menejimenti ya Utumishi wa Umma) alitoa maelekezo hapa kwamba katika hoja yetu ya Bajeti Kuu ilivyokuwa inapita watu walikuwa wanasema kwamba kwa nini sasa fungu hili la mshahara halipo?
Mheshimiwa Naibu Spika, tukumbuke kwamba Mheshimiwa Rais alizungumza wazi alipokuwa katika viwanja vya Mkoa wa Kilimanjaro katika siku ya Mei Mosi. Jambo hili limezingatiwa katika bajeti yetu hii tunayokwenda nayo hivi sasa. Ndiyo maana hata juzi Waziri wa Utumishi wa Umma alikuwa anatoa maelekezo kwamba kuna nyongeza ya fedha hapa ambayo itaenda ku-address jambo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la kupanda madaraja, hali kadhalika eneo hilo madaraja yalisimamishwa kutokana na zoezi maalum la uhakiki hasa wa vyeti feki na watumishi hewa. Vile vile naomba nifanye rejea ya Waziri wetu wa Utumishi wa Umma alipozungumza wazi kwamba suala la kupanda madaraja sasa limewekewa utaratibu mzuri, kila mtu atapanda kwa stahiki yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwaambie kwamba kila mtu atapata stahili yake kwa kadri inavyotakiwa na hili Mheshimiwa Waziri amelizungumza wazi kwa sababu yeye ndiyo anahusika na Utumishi kwamba kila mtu atapata stahiki yake na jambo hili sasa hivi linakamilika na kila mtu atapanda daraja kama ilivyokusudiwa. (Makofi)

Name

Musa Rashid Ntimizi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Serikali imekuwa na dhamira ya dhati ya kuboresha maslahi ya Watumishi hususan Walimu kwa kutoa nyaraka mbalimbali ikiwemo Waraka wa Utumishi wa Serikali Na. 3 wa tarehe 20/10/2014 unaohusu mishahara na Posho ya Madaraka kwa Viongozi wa elimu (Responsibility Allowance):- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kutekeleza waraka huo? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa Posho ya Kufundishia (Teaching Allowance) ili kuleta ufanisi wa kazi?

Supplementary Question 2

MHE. MUSA R. NTIMIZI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Moja ya matatizo ya Walimu wetu ni kukosa makazi katika maeneo wanayofundishia katika vijiji vyetu. Je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha kwamba inajenga nyumba za kutosha kwa Walimu wetu ili kuwapa motisha kufundisha vizuri katika maeneo yetu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la kuimarisha miundombinu hasa kwa Walimu, ni kweli tumekuwa na changamoto ya nyumba, ndiyo maana hata baadhi ya Watumishi wengine wakishaajiriwa wanakumbana na changamoto kubwa sana ya makazi. Ndiyo maana toka mwaka 2016 katika Sekta ya Elimu tulitumia fedha nyingi takriban shilingi bilioni 64 kujenga miundombinu ya madarasa, vyoo na nyumba za Walimu.
Mheshimiwa Naibu Spika, tulifanikiwa katika Shule ya Sekondari; mpango wa MMES II tumejenga nyumba takriban 283. Hata hivyo, naomba nishukuru sana Waheshimiwa Wabunge na wadau mbalimbali. Tumeshiriki kwa pamoja kujenga nyumba katika maeneo mbalimbali, lakini hata hivyo, katika mpango wa Serikali, mwaka huu tutaenda kushirikiana tena na wadau na fungu letu la Serikali kuhakikisha tunaongeza idadi ya nyumba. Lengo kubwa ni Walimu wetu na wataalam mbalimbali ambapo sio kada ya Walimu peke yake, waweze kupata makazi bora.
Mheshimiwa Naibu Spika, najua hii bado ni changamoto kubwa, lakini naomba tushirikiane kwa pamoja, na Serikali imeweka nguvu za kutosha kuhakikisha kwamba tunajenga nyumba za Walimu na wa kada nyingine katika maeneo mbalimbali.

Name

Riziki Shahari Mngwali

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Serikali imekuwa na dhamira ya dhati ya kuboresha maslahi ya Watumishi hususan Walimu kwa kutoa nyaraka mbalimbali ikiwemo Waraka wa Utumishi wa Serikali Na. 3 wa tarehe 20/10/2014 unaohusu mishahara na Posho ya Madaraka kwa Viongozi wa elimu (Responsibility Allowance):- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kutekeleza waraka huo? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa Posho ya Kufundishia (Teaching Allowance) ili kuleta ufanisi wa kazi?

Supplementary Question 3

MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza na ninalo dogo sana. Naomba niseme kwamba Serikali isituambie hapa kama vile inaanza upya.
Mheshimiwa Naibu Spika, taratibu zote hizi za kupandisha vyeo na mengineyo yalikuwepo kabla; lakini sasa hivi kilichotokea kibaya, kuna watu walipandishwa cheo wakalipwa mshahara mpaka miezi mitatu, wakasitishiwa mshahara, wakarejeshwa pale pale. Hivi Mheshimiwa Waziri anatoa kauli gani kuhusu hili? Naomba nijibiwe kwa ufasaha zaidi ili watu waweze kufuatilia.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nashukuru sana maana ningekosa kupata hili swali, roho ya mama yangu Mheshimiwa Riziki ingepata shida sana kwa sababu nilikuwa namwona hapa, hasa nikijua mama yangu ni Mwalimu, kwa hiyo, alikuwa anataka kujua katika kero hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimwambie kwamba; bahati nzuri juzi nilipata viongozi wa Chama cha Walimu kutoka Mkoa wa Rukwa, nilikuwa nao pale ofisini na hiyo ni miongoni mwa concern ambayo waliileta pale ofisini kwetu. Ni kweli kuna watu ambao walipata mishahara ile miezi miwili, lakini baadaye mshahara ukakasitishwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa changamoto kubwa ni kwamba kuna wengine wanaenda kustaafu. Sasa wakistaafu jambo hili linafanyika vipi? Leo hii mtu akistaafu atahesabiwa katika mshahara wa mwanzo wakati alipanda. Ndiyo maana nimesema jambo hili, kama Serikali, tumelichukua kwa uzito wa hali ya juu, tunafanya analysis. Kuna watu wengine ambao watastaafu hivi karibuni. Ina maana tusipo-address vizuri tutakuwa na changamoto kubwa katika hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna watu wengine walipanda, lakini kwa sababu ya utaratibu mzuri uliowekwa naomba niwaondoe hofu Waheshimiwa Wabunge, jambo hili tumelichukua sisi kama viongozi na tumelijua ni tatizo kubwa, lazima tuliweke vizuri. Yalifanyika kwa nia njema kwa sababu huko nyuma hali yetu ilikuwa siyo shwari. Suala zima la watumishi hewa lilikuwa ni jambo kubwa, watumishi takriban 19,000 plus, lilikuwa ni tatizo kubwa sana!
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mpango huu ulikuwa ni mpango mkakati wa Serikali kusaidia kulinda mapato, lakini kupeleka fedha kwa watu wanaostahili . Kwa hiyo, naomba niwatoe hofu wafanyakazi kwamba kila mtu atapata stahili yake na Serikali inafanya kazi kufanya analysis kwa undani zaidi kuondoa hilo tatizo.

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Serikali imekuwa na dhamira ya dhati ya kuboresha maslahi ya Watumishi hususan Walimu kwa kutoa nyaraka mbalimbali ikiwemo Waraka wa Utumishi wa Serikali Na. 3 wa tarehe 20/10/2014 unaohusu mishahara na Posho ya Madaraka kwa Viongozi wa elimu (Responsibility Allowance):- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kutekeleza waraka huo? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa Posho ya Kufundishia (Teaching Allowance) ili kuleta ufanisi wa kazi?

Supplementary Question 4

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa niulize swali la nyongeza. Katika jibu la msingi la Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba Teaching Allowance ipo kwenye mshahara. Sasa tunapata tabu sana tukikutana na Walimu wanapotuambia juu ya kurudisha Teaching Allowance. Je, Serikali itakuwa tayari sasa kutamka ndani ya Bunge hili ili waweze kutambua kwamba Teaching Allowance yao iko kwenye mshahara?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo kubwa tulilokuwa nalo ambalo Waheshimiwa Wabunge wengi sana hapa leo wanalizungumza ni suala zima la maslahi mapana ya watumishi. Ndiyo maana hata hicho kilichokuwepo kama kidogo au kikubwa hakioneshi vizuri ni kwa sababu huenda lile fungu lenyewe, purchasing power imekuwa ni ndogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kupitia Ofisi ya Menejimenti ya Utumishi wa Umma, juzi juzi kulikuwa na kikao maalum kinafanyika kwa sababu kunaundwa bodi maalum ya kuja kupitia maeneo yote hayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukiacha Teaching Allowance, kuna mambo mengine; kuna suala la haki za watu wanaofanya kazi katika mazingira magumu. Kwa hiyo, jambo hili tutakuja kulitamka rasmi sasa baadaye kuhusu mchakato huu unavyokwenda. Hiyo Bodi iliyoundwa sasa kupitia mishahara, siyo kwa Walimu peke yake, isipokuwa watumishi wote ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tutaona jinsi gani kila mtumishi atapata stahili yake na nyongeza kwa kiasi gani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hili tutakuja kulitoleaa tamko rasmi hapa baadaye Bungeni likiwa katika utaratibu mzuri baada ya kutoa hii documentation vizuri.

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. MUSSA R. SIMA aliuliza:- Serikali imekuwa na dhamira ya dhati ya kuboresha maslahi ya Watumishi hususan Walimu kwa kutoa nyaraka mbalimbali ikiwemo Waraka wa Utumishi wa Serikali Na. 3 wa tarehe 20/10/2014 unaohusu mishahara na Posho ya Madaraka kwa Viongozi wa elimu (Responsibility Allowance):- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kutekeleza waraka huo? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa Posho ya Kufundishia (Teaching Allowance) ili kuleta ufanisi wa kazi?

Supplementary Question 5

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Katika Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya kuna shule Shikizi nyingi ambazo zina Walimu wa kujitolea na hawapati posho. Je, ni lini Serikali itaanza kuwalipa posho hawa Walimu wanaofundisha kwenye Shule Shikizi? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, katika jambo hili nadhani kila Halmashauri ina mkakati wake ku-address matatizo ya watumishi katika maeneo mbalimbali; na kuna baadhi ya maeneo mengine utakuta watu wanatumia own source kuonesha jinsi gani wana-address hili jambo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu kuna mambo specific katika eneo la Mheshimiwa Njeza, tutalichukua halafu tuangalie jinsi gani tutafanya kuona nini kimetokea huko ilimradi tuliweke sawa ili kila mtu apate stahiki yake. Kama kuna maeneo mahususi katika Halmashauri husika, basi tutayatoa kwa lengo la kuweka mustakabali mzuri katika maeneo yetu hayo.