Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA S. MOLLEL aliuliza:- Haki ya kupata taarifa ni haki ya msingi kwa kila Mtanzania na vyombo vyetu vya habari havina wakalimani wa lugha ya alama kwa ajili ya kuwawezesha viziwi kupata habari kwa uelewa uliotimilifu kama raia wengine. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa vyombo vya habari hasa tv vinaajiri wakalimani hasa katika taarifa za habari ili waweze kufuatilia matukio yanayooneshwa?

Supplementary Question 1

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali ya nyongeza ninayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, awali ya yote ninalipongeza Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pongezi ziende kwa Spika wa Bunge kwa kuwa tayari wamekwishaanza kutoa huduma hii katika matangazo haya, wakalimani wamekwishaanza kutafsiri na kuwawezesha wenzetu viziwi kupata taarifa.
Kwa kuwa kilio cha haki ya kupata taarifa ni cha muda mrefu katika mjadala pia wa bajeti ya Wizara tulilizungumzia hili. Ningependa kupata commitment ya Serikali; je, ni lini sasa utekelezaji huu utaanza na kwa kuwa TBC ni televisheni ya umma, commitment ya Serikali kwamba Shirika hili litaajiri lini wakalimani wa lugha ya alama ili basi wenzetu viziwi waweze kupata taarifa?
Swali langu la pili, kwa kuwa haki ya kupata habari ni haki ya Kikatiba, je, Serikali inatoa muda gani kwa wamiliki wa vyombo binafsi vya habari ili na wao basi waone umuhimu na kutekeleza haki hii ya Kikatiba ambayo ni ya Ibara ya 18(d)? Ahsante.

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nashukuru sana kwa pongezi ambazo ametoa na tunazipokea, tunasema ahsante sana. (Makofi)
Katika swali lake la kwanza ambalo anahitaji kujua
sasa ni lini TBC itaajiri, nichukue nafasi hii kwa namna ya pekee kabisa kumpongeza Mheshimiwa Amina Mollel kwa jinsi ambavyo amekuwa amepambania haki za walemavu, na kwa kweli nakumbuka kabisa kwamba hata katika mjadala wa bajeti ya Wizara yetu alichangia suala hili na alitaka kujua ni lini hasa vyombo vya utangazaji vitakuwa vikitoa ukalimani wa lugha ya alama.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika majibu yangu ya msingi ni kwamba, katika kikao ambacho kilifanyika wadau wale walijipangia majukumu mbalimbali. Kwa upande wetu Wizara tuliipangia TBC iwe ni chombo cha mfano, ianze mara moja kutoa ukalimani wa lugha ya alama, na kwa kuanzia TBC tayari imeishatuma maombi ya kupata kibali cha kuajiri wakalimani wawili, hivyo wakati wowote kibali kitakapotoka basi TBC itaajiri ili iweze kuwa chombo cha mfano kwa vyombo vingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kwamba ni muda gani tumeweka kwa vyombo vya habari. Kama mlivyosikia katika jibu la msingi ni kwamba, TCRA imepewa jukumu la kuchukua kanzi data kutoka TASLI ambayo ni orodha ya wale wakalimani ambao wana uwezo wa kutoa ukalimani katika vyombo vya habari, wakiishachukua taarifa hizi watakuwa wakipeleka kwa vyombo vya habari.
Sasa tatizo ambalo tunalo ni kwamba vyombo vya habari ni vingi, vyombo vya habari vya utangazaji televisheni, ni vingi takribani 32, lakini kwa mujibu wa TASLI wapo wakalimani 70 na kati ya hao wakalimani 15 tu ndiyo ambao wanaonekana kwamba wana ujuzi na uwezo wa kufanya ukalimani katika vyombo vya habari au utangazaji wa televisheni. Ndiyo maana sasa VETA na CHAVITA wamepewa jukumu la kutoa mafunzo kwa hawa wakalimani wengine waliobaki ili na wao waweze kufikia uwezo wa kutangaza katika vituo vya televisheni. Ahsante.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. AMINA S. MOLLEL aliuliza:- Haki ya kupata taarifa ni haki ya msingi kwa kila Mtanzania na vyombo vyetu vya habari havina wakalimani wa lugha ya alama kwa ajili ya kuwawezesha viziwi kupata habari kwa uelewa uliotimilifu kama raia wengine. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa vyombo vya habari hasa tv vinaajiri wakalimani hasa katika taarifa za habari ili waweze kufuatilia matukio yanayooneshwa?

Supplementary Question 2

MHE. SHAABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ni muda mrefu sasa wananchi wa Wilaya ya Lushoto hawapati mawasiliano hasa ya redio ya Taifa na hili swali nimekuwa nikiliuliza mara kwa mara.
Je, ni lini Serikali itajenga mitambo hiyo ili wananchi wa Wilaya ya Lushoto waweze kupata taarifa kama ilivyokuwa kwa wananchi wengine waishio mjini?

Name

Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Answer

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tu kumuomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira swali linalokuja linaongelea masuala ya usikivu wa redio katika nchi ya Tanzania.