Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Faida Mohammed Bakar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR (K.n.y. MHE. TAUHIDA CASSIAN GALLOS NYIMBO) aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kunusuru mauaji ya vikongwe nchini?

Supplementary Question 1

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR: Mheshimiwa Naibu Spika, asante sana. Pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, vitendo hivi vya kuwaua wazee wetu ama tunavyoita vikongwe lakini hao mimi kwa lugha hii ya vikongwe hata siipendi, wazee wetu! Wazee ni dhamana yetu sisi vijana ama wananchi wote, lakini kuna watu katika mikoa mingine wanawaua wazee wetu, wengine wakiwa hai wanawafukia. Hiyo tunaoneshwa kabisa katika vyombo mbalimbali vya habari. Wengine wanawaua watu kwa kuwafukia kwa sababu wazee wetu wana macho mekundu na watu hawajui kwamba kuwa na macho mekundu ni kupikia kuni kwa wingi, sasa...
MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR: Na mavi ya ng‟ombe, wengine wanasema kinyesi cha ng‟ombe, wanapikia kinyesi cha ng‟ombe wengine macho yanakuwa mekundu.
Je tutawasaidiaje wazee hawa kuwaondoshea kuwa na macho mekundu kwa kuwapelekea gesi kwa wingi kule vijijini ili waweze kuwa na macho mazuri, wasipate kuuliwa kwa itikadi za kishirikina? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri amejibu hapa kama kunatolewa elimu.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Faida hilo ni swali la nyongeza au la pili?
MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR: La pili la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri amesema kwamba hapa Serikali inatoa elimu, hata sisi Wabunge tunapaswa kutoa elimu katika maeneo yetu, lakini sasa athari hii ya kuwaua wazee wetu itakwenda vizazi na vizazi vijavyo huko mbele. Watoto wetu wanajifunza nini kuhusiana na jambo hili hapo mbele?
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inawachukulia hatua gani kuwaondosha hawa watu wanaowaua wazee wetu? Inawachukulia hatua gani kali kukomesha hasa katika mikoa hiyo ya Mwanza, Shinyanga, Tabora na kwingineko, wazee wetu wanauliwa sana? Naomba jibu maridhawa.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna mikakati mbalimbali ambayo tayari imeshaanza kuchukuliwa na Serikali kuhakikisha kwamba matumizi ya kuni ama hayo mavi ya ng‟ombe kwa ajili ya kupikia yanapungua, ikiwemo kuanzisha kwa nishati mbadala, matumizi ya majiko bunifu na kadhalika, lakini pia harakati za Serikali kusambaza umeme vijijini zinasaidia sana kuhakikisha wananchi wanatumia nishati iliyokuwa bora zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, suala lake la pili anazungumzia kwamba hatua gani ambazo Serikali imechukua ili kudhibiti matukio kama haya. Nataka tu nimhakikishie kwamba takwimu ambazo tunazo kuanzia mwezi Julai, 2015 mpaka Machi, 2016 tayari kuna watuhumiwa 135 ambao wameshakamatwa na kesi kama 222 ambazo zinaendelea mahakamani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Jeshi la Polisi ama Serikali kupitia Jeshi la Polisi, linafanya kazi kubwa sana kuhakikisha kwamba linawadhibiti wale wananchi wote ambao wamekuwa wakijichukulia sheria mkononi.