Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zainabu Nuhu Mwamwindi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAINABU N. MWAMWINDI aliuliza:- Gereza la Wilaya ya Iringa ambalo lipo jirani na Hospitali ya Mkoa wa Iringa limekuwa likisababisha usumbufu kwa wananchi wanaotembea kwa miguu hasa nyakati za usiku. Je, Serikali ina mpango gani kwa kuondoa mwingiliano wa shughuli za kijamii na shughuli za gereza hilo?

Supplementary Question 1

MHE. ZAINABU N. MWAMWINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Issue siyo kujenga ukuta kuzuia mwingiliano kati ya wananchi wanaokwenda hospitali na magereza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika vikao vya RCC Mkoa wa Iringa, makubaliano na Wizara ya Mambo ya Ndani ilikuwa kupatiwa eneo mbadala ili Hospitali ya Mkoa wa Iringa ambayo sasa ni Hospitali ya Rufaa iweze kupanuliwa. Halmashauri ya Manispaa ya Iringa ilitekeleza agizo la vikao vya RCC, Magereza walipewa eneo mbadala ambalo liko katika eneo la Mlolo na Serikali kuanzia mwaka 1998 na 2000 imelipa fidia kwa wananchi wote waliokuwa wanamiliki eneo lile. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa swali, kama Serikali imeshawalipa wananchi fidia na eneo liko pale kubwa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kuhamishia matumizi ya Gereza pale, eneo lile ni dogo, Hospitali ya Rufaa inatakiwa iendelezwe na TANROADS waliokuwepo pale wameshaondoka, wamepisha eneo hilo kwa ajili ya eneo la Hospitali. Ni lini Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi itaondoa Jeshi la Mageraza pale ambapo ni eneo linalowatunza wafungwa pale?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, akubaliane na mimi kwamba Mheshimiwa Mwigulu amekuja Iringa ameona hali halisiā€¦
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujua, ni lini sasa magereza wataondoa matumizi yao pale na kuachia Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Iringa?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, anachokisema Mheshimiwa Mbunge ni kweli, na sisi kama Wizara tunakubaliana naye kwa asilimia 100 ya mapendekezo yake aliyoyasema. Niweke sawa sawa hivyo, maana yake nilikuwa naona Mheshimiwa Ritta Kabati hapa anajiandaa kusimama; sasa ili alielewe ni kwamba Wizara inaelewa kwamba kati ya hospitali na gereza kinachotakiwa kuondoka pale mjini ni gereza na siyo hospitali. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa hospitali ile inahitaji upanuzi, Wizara inakubaliana na gereza kuhama pale na kwenda kwenye eneo lingine ambalo na lenyewe liko ndani ya mji lakini pembeni kidogo kilometa kama saba kutoka pale mjini ili kuweza kuwa na nafasi ambayo hata kiusalama itaruhusu mazingira yale kuwa salama zaidi ya kutunza wafungwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, alichojibu Mheshimiwa Naibu Waziri ni kwamba wakati jambo hilo halijafanyika, kuna hatua za mpito ambazo tunazifanya zikiwemo hizo za barabara ile kupitika kwa dharura pamoja na masuala ya ukuta aliyoyasemea. Kadri bajeti inavyoruhusu na taratibu nyingine za ndani ya Wizara ya kutumia nguvu kazi inayoendelea, mpango ni huo huo kuhamisha gereza na kuacha fursa kwa Hospitali ya Mkoa kuweza kuwa na nafasi ya kutosha.

Name

Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. ZAINABU N. MWAMWINDI aliuliza:- Gereza la Wilaya ya Iringa ambalo lipo jirani na Hospitali ya Mkoa wa Iringa limekuwa likisababisha usumbufu kwa wananchi wanaotembea kwa miguu hasa nyakati za usiku. Je, Serikali ina mpango gani kwa kuondoa mwingiliano wa shughuli za kijamii na shughuli za gereza hilo?

Supplementary Question 2

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali moja dogo la nyongeza. Gereza la Kondoa linahudumia Wilaya ya Chemba na Wilaya ya Kondoa. Gereza hili limejengwa mwaka 1919, lina hali mbaya sana.
Je, Serikali haioni ipo haja sasa pengine hata Waziri aende tu aone pale kama kweli hawa wafungwa bado ni binadamu, lakini wanaishi kwenye mazingira mabaya sana. Askari wana hali mbaya sana, hata Mkuu wa Gereza anatembea na boda boda. Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari hata kwenda tu?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na mwaliko wa Mheshimiwa Juma Nkamia na mara kwa mara amekuwa mstari wa mbele kuunga mkono jitihada na mahitaji yanayotakiwa katika Wizara ya Mambo ya Ndani ikiwepo nyumba za Polisi, nyumba za Askari Magereza, Zimamoto pamoja na Uhamiaji. Kwa hiyo, sina tatizo na kwenda Wilayani kwake pamoja na Wilaya jirani ya kondoa ili kuweza kujiridhisha na mazingira hayo ili kuweza kuweka utekelezaji mzuri zaidi wa ujenzi wa gereza ili wafungwa pamoja na askari waweze kufanya kazi katika mazingira ya usalama zaidi. Nitafanya hivyo baada ya bajeti yetu kuwa imepita.