Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Faida Mohammed Bakar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR aliuliza:- Majukumu ya Mbunge kwa kuzingatia matakwa ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 63(3) yameainisha kwa ujumla wake bila kubagua aina ya Ubunge; lakini Sheria Namba 16 ya mwaka 2009 iliyounda Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo (CDCF) imeonesha ubaguzi mkubwa kwa kumtambua Mbunge wa Jimbo pekee ambaye ndiye aliyetajwa na sheria hiyo kama Mwenyekiti wa Kamati ya Usimamizi wa Mfuko huo na kuwatenga Wabunge wa Viti Maalum licha ya kwamba Wabunge wote wanatekeleza majukumu sawa ya kuwatumikia wananchi. Je, ni lini Serikali itarekebisha sheria hii ili ijumuishe Wabunge wote ikiwemo Wabunge wa Viti Maalum?

Supplementary Question 1

MHE. FAIDA MOHAMED BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu hayo ambayo hayajaniridhisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba sheria hii haina ubaguzi lakini mimi nasema ina ubaguzi. Kwa sababu iweje sheria ipingane na Katiba? Katiba imetutambua Wabunge wa Viti Maalum na Wabunge wa Majimbo sote ni sawa, tuna haki sawa, tunafanya kazi sawa za kuiletea maendeleo nchi yetu hii iweje leo useme haina ubaguzi?
Je, ni lini sheria hii italetwa hapa Bungeni ili tuirekebishe tupate haki sawa sote, Wabunge wa Majimbo na Wabunge wa Viti Maalum, kwa sababu sote tunafanya kazi sawa?
Pili, kwa kuwa Wabunge wa Viti Maalum tunafanya
kazi zaidi kwa sababu sisi tuna-handle mikoa, lakini Wabunge wa majimbo wanakuwa na majimbo. Jimbo liko ndani ya mkoa, Wabunge wa Viti Maalum tuko kwenye mkoa mzima tunafanya kazi za maendeleo, lakini tunatumia hela zetu za mfukoni tukipata posho, tukipata mshahara, ndiyo tunatumia Serikali haituhurumii?
Je, ni kitu gani chenye kigezo muafaka ambacho amekisema Naibu Waziri kati ya Jimbo na Mkoa upi wenye kigezo ambacho kinakubalika watu wengi, sijui Mkoa ni mkubwa kama alivyosema kuliko Jimbo...
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri anipe kigezo, bado hajaniambia kigezo.(Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa nimesema kwa sababu sijasema mimi kama Jafo, nimesema kwa mujibu wa sheria. Bahati nzuri mnafahamu ndugu zangu kwamba sheria hii ilitungwa humu Bungeni na sheria hii ilipata msuguano mkubwa sana, ndiyo maana ukija kuangalia ni kwamba sheria hii hata suala la vile vigezo vilivyotengwa ndiyo maana inaitwa Sheria ya Mfuko wa Jimbo. Kwa hiyo, kama itaonekana kwamba nini kifanyike hayo sasa ni mawazo mengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu lazima tufahamu kuna Wabunge wa Majimbo, kuna Wabunge wa Viti Maalum kutoka Mikoa, kuna Wabunge wengine wanateuliwa na Rais maana yake wanazungumza karibu Tanzania nzima. Kwa hiyo, kama tukitaka tufanye tafakari hiyo na kutakuwa na Wabunge wengine ambao wao wanahudumu Tanzania nzima ndiyo maana nimesema Bunge hili ndiyo lenye dhamana ya kutunga sheria ikionekana jambo hilo linahitajika lifanyike, Bunge litafanya maamuzi sahihi. Tufahamu vilevile hata mkoa hauwakilishwi na Mbunge mmoja. Inawezekana mikoa mingine ina Wabunge wa Viti Maalum saba. Ndiyo maana nimesema jambo hili linatakiwa ifanyike needs assessment kwa ujumla wake kupata maamuzi kama Taifa. (Makofi)
NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS,TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamshukuru Dada yangu Faida Bakar kuna sehemu ya pili alisema Wabunge wanatumia fedha zao. Naomba niwaambie hasa na Wabunge wa Majimbo, fedha za Mfuko wa Jimbo siyo fedha za kwenda kugawa kama zawadi. Fedha za Mfuko wa Jimbo zinapita katika akaunti maalum na zina Wajumbe maalum akiwepo Afisa Mipango ni Katibu wa Mfuko wa Jimbo, fedha ile inaingia mara moja kwa mwaka na Kamati inafanya maamuzi kutekeleza miradi, fedha ile siyo fedha ya kuingia mfukoni kwa mtu kwenda kutoa sadaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, niwatahadharishe Wabunge wa Majimbo kwamba mfahamu fedha hii inakwenda kujibu matatizo ya wananchi. Mlivyopita kuna mahitaji mbalimbali wananchi wameibua sasa katika vikao vyenu mnafanya maamuzi kwenda kujibu matatizo.(Makofi)

Name

Andrew John Chenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR aliuliza:- Majukumu ya Mbunge kwa kuzingatia matakwa ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 63(3) yameainisha kwa ujumla wake bila kubagua aina ya Ubunge; lakini Sheria Namba 16 ya mwaka 2009 iliyounda Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo (CDCF) imeonesha ubaguzi mkubwa kwa kumtambua Mbunge wa Jimbo pekee ambaye ndiye aliyetajwa na sheria hiyo kama Mwenyekiti wa Kamati ya Usimamizi wa Mfuko huo na kuwatenga Wabunge wa Viti Maalum licha ya kwamba Wabunge wote wanatekeleza majukumu sawa ya kuwatumikia wananchi. Je, ni lini Serikali itarekebisha sheria hii ili ijumuishe Wabunge wote ikiwemo Wabunge wa Viti Maalum?

Supplementary Question 2

MHE. ANDREW J. CHENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana kwa kunipatia nafasi hii, lakini pia niishukuru sana majibu ya Serikali kwa swali hilo, swali langu la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mgao wa mwisho wa fedha hizi za kuchochea maendeleo ya jimbo, baadhi ya majimbo nchini hapa likiwemo na Jimbo la Bariadi mgao wake wa kisheria ambao umetajwa na Mheshimiwa Waziri katika majibu yake, mgao wake haukuzingatiwa. Majimbo hayo likiwepo na la Bariadi walipewa fedha pungufu kinyume na vigezo hivyo. (Makofi)
Je, Serikali iko tayari kusahihisha dosari hiyo? Ahsante

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Waziri wangu mwenye dhamana alitoa maelezo hapa katika nyakati mbalimbali suala zima baadhi ya majimbo fedha kuwa pungufu zaidi na hasa katika Mkoa wa Mwanza. Ninafahamu kwamba Mkoa wa Mwanza ulikuwa umeathirika kwa kiwango kikubwa sana lakini mgao ule kipindi kile ulitokea kwa sababu bajeti yetu ilikuwa inalenga bajeti ya majimbo ya mwanzo, kwa hiyo, majimbo mengine yalivyoongezeka kutoka Majimbo 189 mpaka 220 ikasababisha zile fedha zikawa na mgao mdogo, hata hivyo kulikuwa na makosa ya kimahesabu ambayo ofisi yetu ilitoa maelekezo kwa ma-RAS kwamba zile fedha ambazo baaadhi ya majimbo yaliongezewa zirudi kwa ma-RAS wa mikoa, lengo kubwa ni kufanya usahihisho kwa bajeti ile ya mwaka 2016/2017.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti yetu ambayo tumeipitisha juzi hapa mwaka 2017/2018 ninaamini tumeshafanya marekebisho makubwa na Majimbo yote tarajieni katika bajeti ya mwaka huu unaokuja, imefanya mazingatio ya ongezeko la Majimbo mapya haya ambayo mimi nina imani hatutakuwa na shida tena huko tunakokwenda.

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR aliuliza:- Majukumu ya Mbunge kwa kuzingatia matakwa ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 63(3) yameainisha kwa ujumla wake bila kubagua aina ya Ubunge; lakini Sheria Namba 16 ya mwaka 2009 iliyounda Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo (CDCF) imeonesha ubaguzi mkubwa kwa kumtambua Mbunge wa Jimbo pekee ambaye ndiye aliyetajwa na sheria hiyo kama Mwenyekiti wa Kamati ya Usimamizi wa Mfuko huo na kuwatenga Wabunge wa Viti Maalum licha ya kwamba Wabunge wote wanatekeleza majukumu sawa ya kuwatumikia wananchi. Je, ni lini Serikali itarekebisha sheria hii ili ijumuishe Wabunge wote ikiwemo Wabunge wa Viti Maalum?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwanza Mbunge aliyeuliza swali kwamba Wabunge wanatumia zile pesa, namshukuru sana Naibu Waziri alivyoeleza kuhusu zile pesa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pesa Wabunge hawashiki, pesa zinakwenda kwa Mkurugenzi, Mwenyekiti yeye ni Mwenyekiti tu. Kuna Afisa Mipango, kuna Madiwani wawili, kuna watendaji wawili ndipo utagawa zile pesa, hatugusi hata senti tano moja sisi kuweka kwenye mafuta.(Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, huu Mfuko wa Jimbo nimezungumza tangu mara ya kwanza una matatizo. Kuna majimbo mengine na tujimbo twingine.
Huu mfuko hauwezi kufutwa kwa sababu kuna Wabunge wengine kama Viti Maalum, mzee wangu anasema Majimbo, Majimbo mengine yana watu 30, watu 40, mengine kata 10 Jimbo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napendekeza kama nilivyosema mara ya kwanza usimamishwe, wafanye tathmini upya, wagawe upya kutokana na idadi ya watu na ukubwa wa majimbo. Haiwezekani kuna majimbo mengine ni madogo wanapewa sawa na Jimbo kubwa haiwezekani. Ifanywe tathmini upya ili hela ziende kwa usawa bila ubaguzi wowote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, majimbo ambayo hayana vigezo, hayastahili kuapata mfuko wa Jimbo mkubwa, haiwezekani. Jimbo lako la Ilala kubwa lipate sawa na Jimbo...
Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima tuende na takwimu sahihi, haiwezekani.
Swali, Wabunge Viti Maalum hawaruhusiwi kupata Mfuko wa Jimbo na wasitegemee kuzipata, kwa sababu Mbunge wa Jimbo ndiyo anastahili kupata ule Mfuko wa Jimbo na ikiwezekana Wabunge wale wengine wachunguzwe walikotoka. Haiwezekani wewe uliyekuja kuzungumza hapa wakati ulikotoka wewe hauna hata wa...(Kicheko)

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Keissy ameuliza maswali ya nyongeza pia ametoa maelezo ya nyongeza. Hata hivyo katika maelezo yake kuna vitu vya msingi amevisema.
Kwanza ambacho ndicho nitakachokijibu vingine nitaviacha kwa sababu kwa mujibu wa Kanuni natakiwa kujibu swali moja. Ni kweli kwamba kuna vigezo vinavyotumika katika kugawa fedha hizi, vigezo hivi vimesemwa katika jibu la msingi. Kigezo cha kwanza ni idadi ya watu ambayo ni asilimia 45. Mgao sawa kwa kila Jimbo asilimia 25, kiwango cha umaskini asilimia 20, ukubwa wa eneo asilimia 10. Fedha yoyote itakayotengwa kwenye bajeti hapa itaingizwa katika hii formula.
Kwa hiyo, bahati mbaya sana kwa mwaka huu wa fedha, fedha iliyotengwa ilikua kidogo kwa sababu Hazina hawakutambua majimbo haya mapya, hatukuwa na mawasiliano mazuri. Nataka niwahakikishie kwamba kigezo hiki sasa kwa mwaka huu wa fedha tumesahihisha hayo makosa yote na sasa majimbo yote yanahesabika, yaliyoongezeka na kosa hilo halitafanyika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba kuna baadhi ya Majimbo yanapewa fedha kidogo kwa mujibu wa formula hii, hilo haliwezekani isipokuwa fedha zimeshuka tu kwa sababu zilikuwa kidogo na tulilazimika kuziingiza kwenye formula hii kama zilivyo, ndiyo maana ni tofauti na iliyotolewa nyuma na iliyotolewa sasa.

Name

Ester Michael Mmasi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR aliuliza:- Majukumu ya Mbunge kwa kuzingatia matakwa ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 63(3) yameainisha kwa ujumla wake bila kubagua aina ya Ubunge; lakini Sheria Namba 16 ya mwaka 2009 iliyounda Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo (CDCF) imeonesha ubaguzi mkubwa kwa kumtambua Mbunge wa Jimbo pekee ambaye ndiye aliyetajwa na sheria hiyo kama Mwenyekiti wa Kamati ya Usimamizi wa Mfuko huo na kuwatenga Wabunge wa Viti Maalum licha ya kwamba Wabunge wote wanatekeleza majukumu sawa ya kuwatumikia wananchi. Je, ni lini Serikali itarekebisha sheria hii ili ijumuishe Wabunge wote ikiwemo Wabunge wa Viti Maalum?

Supplementary Question 4

MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naitwa Mmasi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda tu nimkumbushe Kaka yangu Jafo. Kaka yangu Mheshimiwa Naibu Waziri tulipokuja hapa Bungeni mimi na wewe tulikula kiapo kimoja, tofauti yetu ilikuwa kwenye majina. Mimi nilitamka Ester Michael Mmasi na wewe ukatamka jina lako kadri ilivyo kwenye kumbukumbu za Bunge hili. Mheshimiwa Naibu Waziri kwenye maslahi ya Kibunge hususani katika payroll ya Bunge sote tuna maslahi sawa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, majibu hapa yametoka kwamba hawa wenzetu kupitia Mfuko wa Jimbo wanafanya kazi za wananchi, sisi ni akina nani na tunafanya kazi za nani?Hatufanyi kazi za familia zetu, tunafanya kazi za wananchi hawa hawa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia nchi ya Kenya, mathalani Wabunge...
MHE. ESTER M. MMASI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia Wabunge wa Kenya hili linafanyika. Nenda tukaangalie Wabunge wa Kenya (Woman MP’s) kwenye county level wana-Capital Development Funds for women MP’s, kwa nini Tanzania ishindikane?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa heshima kubwa naomba kujibu swali ambalo nadhani litakuwa swali maarufu la mwaka na limeulizwa kwa staili ambayo haijawahi kufanyika, ninakupongeza Mwenyekiti kwa utaalamu wa kujua Kanuni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali hili linahusu Mfuko wa Jimbo na Waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa Ester Mmasi, Mheshimiwa Munde Abdallah na wengine wengi Wabunge wa Viti Maalum wanataka na wao wapate mgao wa fedha za Mfuko wa Jimbo. Swali hili siyo kwamba linaulizwa kwa mara ya mwanzo leo, limekuwa likiulizwa na mara nyingi tumekuwa tukitoa majawabu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, majibu maarufu ambayo tumeyatoa kwamba tutakwenda kushughulikia tuone utaratibu wake, lakini kila tunaposhughulikia tunapata ugumu kwa sababu mfuko huu umezaliwa kwa mujibu wa sheria, sheria yenyewe inaitekeleza Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mfuko wenyewe unaitwa Mfuko wa Jimbo na kwa hiyo, kuupa jina linguine lolote lile ni kazi ngumu kweli. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, humu ndani kuna Wabunge
wa Majimbo, kuna Wabunge wa Viti Maalum, kuna Wabunge wa Mikoa, kuna Wabunge wanaoteuliwa na Mheshimiwa Rais. Bunge hili likitambua kwamba Wabunge wa aina hizi zote wapo, lilitunga Sheria ya Mfuko wa Jimbo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa kwenye instrument yangu kwa mujibu wa sheria nilizopewa kuzisimamia nina sheria inayosema nitasimamia Mfuko wa Jimbo, haisemi vinginevyo. Ndiyo maana kwenye jibu letu la msingi nimesema kama Bunge litaona vinginevyo suala hilo linakuja kwa utaratibu mwingine, lakini kwa sasa mimi ninasimamia Mfuko wa Jimbo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata wale Wabunge waliokuwa wanadai sana mfuko huu, waliokuwa wa Viti Maalum, walipopata majimbo na wenyewe msimamo wao umebadilika, ni kwa sababu ya majukumu anayoyapata Mbunge wa Jimbo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali mengine yameulizwa na Mheshimiwa Masoud Abdallah Salim ambaye ameuliza suala la fedha kuchelewa Zanzibar, hili tumelichukua, tunawasiliana na Ofisi ya Makamu wa Rais tuone utaratibu bora zaidi wa kuweza kufanya fedha hizo ziwafikie Wabunge wa Zanzibar, hasa tunatambua yapo mapendekezo ya kwamba bora zikapita katika Ofisi ya Bunge Zanzibar. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine dogo limeulizwa na Mheshimiwa Paresso kwamba Wabunge wa Viti Maalum hawaingii kwenye Kamati za Fedha. Kamati za Fedha zinatambua uwepo wa Madiwani na Mbunge unapoingia kwenye Halmashauri huwi Mbunge unakuwa Diwani, kule kwenye Kamati ya Fedha wanaoteuliwa kuingia kwenye Kamati ya Fedha huwa ni Madiwani. Sasa nadhani ni utaratibu wa Halmashauri zenu, kama wewe Mbunge kuteuliwa kuna baadhi ya Wabunge ambao wanaingia kwenye Kamati ya Fedha, lakini kule wameingia kwa tiketi ya Udiwani wao kwenye Halmashauri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa napata shida hapa
kwa sababu la kwanza, kwamba kwa Majimbo ambayo yana Wabunge wengi wa Viti Maalum, na mfahamu kikao kile kina utaratibu wa gharama zake na mambo mengine. Ingawa gharama siyo hoja kubwa, lakini kwa Jimbo ambalo lina Wabunge wa Viti Maalum nane, 10, sijui hali itakuwaje kwa sababu gharama za uendeshaji wa Halmashauri zitakuwa kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili ingelikuwa Wabunge labda ni mmoja au wawili pengine unaweza kuichukulia hili jambo likawezekana, lakini kwa hali ilivyo kuna tatizo kubwa sana na ninadhani ni vema hili jambo likabaki kama ilivyo na ndio utaratibu ulivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa tiketi ya Udiwani, Mbunge anaweza akateuliwa na Mwenyekiti kwa utaratibu ule akawa Mjumbe wa Kamati ya Fedha.(Makofi)

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR aliuliza:- Majukumu ya Mbunge kwa kuzingatia matakwa ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 63(3) yameainisha kwa ujumla wake bila kubagua aina ya Ubunge; lakini Sheria Namba 16 ya mwaka 2009 iliyounda Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo (CDCF) imeonesha ubaguzi mkubwa kwa kumtambua Mbunge wa Jimbo pekee ambaye ndiye aliyetajwa na sheria hiyo kama Mwenyekiti wa Kamati ya Usimamizi wa Mfuko huo na kuwatenga Wabunge wa Viti Maalum licha ya kwamba Wabunge wote wanatekeleza majukumu sawa ya kuwatumikia wananchi. Je, ni lini Serikali itarekebisha sheria hii ili ijumuishe Wabunge wote ikiwemo Wabunge wa Viti Maalum?

Supplementary Question 5

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.
Ubaguzi huu wa Wabunge kati ya Wabunge wa Viti Maalum na Wabunge wa Majimbo pamoja na kutokupewa Mifuko ya Jimbo, lakini pia hatuingii katika Kamati za Fedha kwenye Halmashauri zetu na jambo hili tumeshalisema muda mrefu, kwa nini Serikali inakuwa na kigugumizi kuruhusu Wabunge wa Viti Maalum katika Halmashauri tulizowapa tusiingie katika Kamati ya Fedha? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe rai kwa Waheshimiwa Wabunge wa Viti Maalum ni hofu tu, tutawang’oa Majimboni. (Makofi/Kicheko)

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa heshima kubwa naomba kujibu swali ambalo nadhani litakuwa swali maarufu la mwaka na limeulizwa kwa staili ambayo haijawahi kufanyika, ninakupongeza Mwenyekiti kwa utaalamu wa kujua Kanuni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali hili linahusu Mfuko wa Jimbo na Waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa Ester Mmasi, Mheshimiwa Munde Abdallah na wengine wengi Wabunge wa Viti Maalum wanataka na wao wapate mgao wa fedha za Mfuko wa Jimbo. Swali hili siyo kwamba linaulizwa kwa mara ya mwanzo leo, limekuwa likiulizwa na mara nyingi tumekuwa tukitoa majawabu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, majibu maarufu ambayo tumeyatoa kwamba tutakwenda kushughulikia tuone utaratibu wake, lakini kila tunaposhughulikia tunapata ugumu kwa sababu mfuko huu umezaliwa kwa mujibu wa sheria, sheria yenyewe inaitekeleza Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mfuko wenyewe unaitwa Mfuko wa Jimbo na kwa hiyo, kuupa jina linguine lolote lile ni kazi ngumu kweli. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, humu ndani kuna Wabunge
wa Majimbo, kuna Wabunge wa Viti Maalum, kuna Wabunge wa Mikoa, kuna Wabunge wanaoteuliwa na Mheshimiwa Rais. Bunge hili likitambua kwamba Wabunge wa aina hizi zote wapo, lilitunga Sheria ya Mfuko wa Jimbo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa kwenye instrument yangu kwa mujibu wa sheria nilizopewa kuzisimamia nina sheria inayosema nitasimamia Mfuko wa Jimbo, haisemi vinginevyo. Ndiyo maana kwenye jibu letu la msingi nimesema kama Bunge litaona vinginevyo suala hilo linakuja kwa utaratibu mwingine, lakini kwa sasa mimi ninasimamia Mfuko wa Jimbo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata wale Wabunge waliokuwa wanadai sana mfuko huu, waliokuwa wa Viti Maalum, walipopata majimbo na wenyewe msimamo wao umebadilika, ni kwa sababu ya majukumu anayoyapata Mbunge wa Jimbo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali mengine yameulizwa na Mheshimiwa Masoud Abdallah Salim ambaye ameuliza suala la fedha kuchelewa Zanzibar, hili tumelichukua, tunawasiliana na Ofisi ya Makamu wa Rais tuone utaratibu bora zaidi wa kuweza kufanya fedha hizo ziwafikie Wabunge wa Zanzibar, hasa tunatambua yapo mapendekezo ya kwamba bora zikapita katika Ofisi ya Bunge Zanzibar. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine dogo limeulizwa na Mheshimiwa Paresso kwamba Wabunge wa Viti Maalum hawaingii kwenye Kamati za Fedha. Kamati za Fedha zinatambua uwepo wa Madiwani na Mbunge unapoingia kwenye Halmashauri huwi Mbunge unakuwa Diwani, kule kwenye Kamati ya Fedha wanaoteuliwa kuingia kwenye Kamati ya Fedha huwa ni Madiwani. Sasa nadhani ni utaratibu wa Halmashauri zenu, kama wewe Mbunge kuteuliwa kuna baadhi ya Wabunge ambao wanaingia kwenye Kamati ya Fedha, lakini kule wameingia kwa tiketi ya Udiwani wao kwenye Halmashauri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa napata shida hapa
kwa sababu la kwanza, kwamba kwa Majimbo ambayo yana Wabunge wengi wa Viti Maalum, na mfahamu kikao kile kina utaratibu wa gharama zake na mambo mengine. Ingawa gharama siyo hoja kubwa, lakini kwa Jimbo ambalo lina Wabunge wa Viti Maalum nane, 10, sijui hali itakuwaje kwa sababu gharama za uendeshaji wa Halmashauri zitakuwa kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili ingelikuwa Wabunge labda ni mmoja au wawili pengine unaweza kuichukulia hili jambo likawezekana, lakini kwa hali ilivyo kuna tatizo kubwa sana na ninadhani ni vema hili jambo likabaki kama ilivyo na ndio utaratibu ulivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa tiketi ya Udiwani, Mbunge anaweza akateuliwa na Mwenyekiti kwa utaratibu ule akawa Mjumbe wa Kamati ya Fedha.(Makofi)

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR aliuliza:- Majukumu ya Mbunge kwa kuzingatia matakwa ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 63(3) yameainisha kwa ujumla wake bila kubagua aina ya Ubunge; lakini Sheria Namba 16 ya mwaka 2009 iliyounda Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo (CDCF) imeonesha ubaguzi mkubwa kwa kumtambua Mbunge wa Jimbo pekee ambaye ndiye aliyetajwa na sheria hiyo kama Mwenyekiti wa Kamati ya Usimamizi wa Mfuko huo na kuwatenga Wabunge wa Viti Maalum licha ya kwamba Wabunge wote wanatekeleza majukumu sawa ya kuwatumikia wananchi. Je, ni lini Serikali itarekebisha sheria hii ili ijumuishe Wabunge wote ikiwemo Wabunge wa Viti Maalum?

Supplementary Question 6

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ningependa nimuulize Mheshimiwa Waziri swali lifuatalo:-
Kwa kuwa fedha za Mfuko wa Jimbo pale ambapo zinaingizwa kwenye akaunti kwa upande wa Tanzania Bara, kwa upande wa Zanzibar zinachukua karibu miezi minne mpaka mitano kutokana na mlolongo mrefu ambapo fedha hizi zinaingizwa katika akaunti zetu za Majimbo ndani ya Wabunge wa Visiwa vya Unguja na Pemba.
Ningependa kumuuliza Mheshimiwa Waziri, je, ni sababu zipi za msingi zinazopelekea fedha zinapoingia katika akaunti za Majimbo ya Tanznaia Bara zinachukua miezi sita kwa upande wa Tanzania Zanzibar. Je, nini kifanyike ili fedha hizi ziweze kufika kwa wakati kama ambavyo zinavyoingia upande huu? Nashukuru sana.

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa heshima kubwa naomba kujibu swali ambalo nadhani litakuwa swali maarufu la mwaka na limeulizwa kwa staili ambayo haijawahi kufanyika, ninakupongeza Mwenyekiti kwa utaalamu wa kujua Kanuni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali hili linahusu Mfuko wa Jimbo na Waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa Ester Mmasi, Mheshimiwa Munde Abdallah na wengine wengi Wabunge wa Viti Maalum wanataka na wao wapate mgao wa fedha za Mfuko wa Jimbo. Swali hili siyo kwamba linaulizwa kwa mara ya mwanzo leo, limekuwa likiulizwa na mara nyingi tumekuwa tukitoa majawabu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, majibu maarufu ambayo tumeyatoa kwamba tutakwenda kushughulikia tuone utaratibu wake, lakini kila tunaposhughulikia tunapata ugumu kwa sababu mfuko huu umezaliwa kwa mujibu wa sheria, sheria yenyewe inaitekeleza Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mfuko wenyewe unaitwa Mfuko wa Jimbo na kwa hiyo, kuupa jina linguine lolote lile ni kazi ngumu kweli. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, humu ndani kuna Wabunge
wa Majimbo, kuna Wabunge wa Viti Maalum, kuna Wabunge wa Mikoa, kuna Wabunge wanaoteuliwa na Mheshimiwa Rais. Bunge hili likitambua kwamba Wabunge wa aina hizi zote wapo, lilitunga Sheria ya Mfuko wa Jimbo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa kwenye instrument yangu kwa mujibu wa sheria nilizopewa kuzisimamia nina sheria inayosema nitasimamia Mfuko wa Jimbo, haisemi vinginevyo. Ndiyo maana kwenye jibu letu la msingi nimesema kama Bunge litaona vinginevyo suala hilo linakuja kwa utaratibu mwingine, lakini kwa sasa mimi ninasimamia Mfuko wa Jimbo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata wale Wabunge waliokuwa wanadai sana mfuko huu, waliokuwa wa Viti Maalum, walipopata majimbo na wenyewe msimamo wao umebadilika, ni kwa sababu ya majukumu anayoyapata Mbunge wa Jimbo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali mengine yameulizwa na Mheshimiwa Masoud Abdallah Salim ambaye ameuliza suala la fedha kuchelewa Zanzibar, hili tumelichukua, tunawasiliana na Ofisi ya Makamu wa Rais tuone utaratibu bora zaidi wa kuweza kufanya fedha hizo ziwafikie Wabunge wa Zanzibar, hasa tunatambua yapo mapendekezo ya kwamba bora zikapita katika Ofisi ya Bunge Zanzibar. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine dogo limeulizwa na Mheshimiwa Paresso kwamba Wabunge wa Viti Maalum hawaingii kwenye Kamati za Fedha. Kamati za Fedha zinatambua uwepo wa Madiwani na Mbunge unapoingia kwenye Halmashauri huwi Mbunge unakuwa Diwani, kule kwenye Kamati ya Fedha wanaoteuliwa kuingia kwenye Kamati ya Fedha huwa ni Madiwani. Sasa nadhani ni utaratibu wa Halmashauri zenu, kama wewe Mbunge kuteuliwa kuna baadhi ya Wabunge ambao wanaingia kwenye Kamati ya Fedha, lakini kule wameingia kwa tiketi ya Udiwani wao kwenye Halmashauri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa napata shida hapa
kwa sababu la kwanza, kwamba kwa Majimbo ambayo yana Wabunge wengi wa Viti Maalum, na mfahamu kikao kile kina utaratibu wa gharama zake na mambo mengine. Ingawa gharama siyo hoja kubwa, lakini kwa Jimbo ambalo lina Wabunge wa Viti Maalum nane, 10, sijui hali itakuwaje kwa sababu gharama za uendeshaji wa Halmashauri zitakuwa kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili ingelikuwa Wabunge labda ni mmoja au wawili pengine unaweza kuichukulia hili jambo likawezekana, lakini kwa hali ilivyo kuna tatizo kubwa sana na ninadhani ni vema hili jambo likabaki kama ilivyo na ndio utaratibu ulivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa tiketi ya Udiwani, Mbunge anaweza akateuliwa na Mwenyekiti kwa utaratibu ule akawa Mjumbe wa Kamati ya Fedha.(Makofi)

Name

Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR aliuliza:- Majukumu ya Mbunge kwa kuzingatia matakwa ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 63(3) yameainisha kwa ujumla wake bila kubagua aina ya Ubunge; lakini Sheria Namba 16 ya mwaka 2009 iliyounda Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo (CDCF) imeonesha ubaguzi mkubwa kwa kumtambua Mbunge wa Jimbo pekee ambaye ndiye aliyetajwa na sheria hiyo kama Mwenyekiti wa Kamati ya Usimamizi wa Mfuko huo na kuwatenga Wabunge wa Viti Maalum licha ya kwamba Wabunge wote wanatekeleza majukumu sawa ya kuwatumikia wananchi. Je, ni lini Serikali itarekebisha sheria hii ili ijumuishe Wabunge wote ikiwemo Wabunge wa Viti Maalum?

Supplementary Question 7

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa fursa hii na mimi niweze kuuliza swali.
Kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri amesema kwamba pesa zile za Jimbo huwa zinakwenda kutumika kwa wananchi; na kwa kuwa Wabunge wa Viti Maalum wanafanya kazi na wananchi hao hao; na kwa kuwa tumelisema suala hili kuanzia mwaka 2011 mpaka leo hii na Serikali bado ina kigugumizi, bado inaona ugumu kuwapa pesa Wabunge wa Viti Maalum, huenda bajeti ya Serikali haiko vizuri.
Je, Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari sasa kwa nia njema kabisa ya kusaidia Wabunge hawa wa Viti Maalum, walau kila Mbunge wa Jimbo husika kwa mfano kwangu mimi nina Majimbo 11, kila Mbunge wa Jimbo husika walau akakatwa asilimia 10 ya Mfuko wa Jimbo ikakaa kwa Mkurugenzi, amount ya pesa zile wakagaiwa Wabunge wa Majimbo siyo kugaiwa cash, zikakaa kwa Mkurugenzi labla mimi nikawa na milioni nne tu, nikaenda eneo fulani nikakuta hamna gloves nikawaambia zile milioni nne Mkurugenzi m-deposit kwa ajili ya kina mama? (Makofi)

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa heshima kubwa naomba kujibu swali ambalo nadhani litakuwa swali maarufu la mwaka na limeulizwa kwa staili ambayo haijawahi kufanyika, ninakupongeza Mwenyekiti kwa utaalamu wa kujua Kanuni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali hili linahusu Mfuko wa Jimbo na Waheshimiwa Wabunge, Mheshimiwa Ester Mmasi, Mheshimiwa Munde Abdallah na wengine wengi Wabunge wa Viti Maalum wanataka na wao wapate mgao wa fedha za Mfuko wa Jimbo. Swali hili siyo kwamba linaulizwa kwa mara ya mwanzo leo, limekuwa likiulizwa na mara nyingi tumekuwa tukitoa majawabu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, majibu maarufu ambayo tumeyatoa kwamba tutakwenda kushughulikia tuone utaratibu wake, lakini kila tunaposhughulikia tunapata ugumu kwa sababu mfuko huu umezaliwa kwa mujibu wa sheria, sheria yenyewe inaitekeleza Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mfuko wenyewe unaitwa Mfuko wa Jimbo na kwa hiyo, kuupa jina linguine lolote lile ni kazi ngumu kweli. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, humu ndani kuna Wabunge
wa Majimbo, kuna Wabunge wa Viti Maalum, kuna Wabunge wa Mikoa, kuna Wabunge wanaoteuliwa na Mheshimiwa Rais. Bunge hili likitambua kwamba Wabunge wa aina hizi zote wapo, lilitunga Sheria ya Mfuko wa Jimbo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa kwenye instrument yangu kwa mujibu wa sheria nilizopewa kuzisimamia nina sheria inayosema nitasimamia Mfuko wa Jimbo, haisemi vinginevyo. Ndiyo maana kwenye jibu letu la msingi nimesema kama Bunge litaona vinginevyo suala hilo linakuja kwa utaratibu mwingine, lakini kwa sasa mimi ninasimamia Mfuko wa Jimbo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata wale Wabunge waliokuwa wanadai sana mfuko huu, waliokuwa wa Viti Maalum, walipopata majimbo na wenyewe msimamo wao umebadilika, ni kwa sababu ya majukumu anayoyapata Mbunge wa Jimbo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali mengine yameulizwa na Mheshimiwa Masoud Abdallah Salim ambaye ameuliza suala la fedha kuchelewa Zanzibar, hili tumelichukua, tunawasiliana na Ofisi ya Makamu wa Rais tuone utaratibu bora zaidi wa kuweza kufanya fedha hizo ziwafikie Wabunge wa Zanzibar, hasa tunatambua yapo mapendekezo ya kwamba bora zikapita katika Ofisi ya Bunge Zanzibar. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine dogo limeulizwa na Mheshimiwa Paresso kwamba Wabunge wa Viti Maalum hawaingii kwenye Kamati za Fedha. Kamati za Fedha zinatambua uwepo wa Madiwani na Mbunge unapoingia kwenye Halmashauri huwi Mbunge unakuwa Diwani, kule kwenye Kamati ya Fedha wanaoteuliwa kuingia kwenye Kamati ya Fedha huwa ni Madiwani. Sasa nadhani ni utaratibu wa Halmashauri zenu, kama wewe Mbunge kuteuliwa kuna baadhi ya Wabunge ambao wanaingia kwenye Kamati ya Fedha, lakini kule wameingia kwa tiketi ya Udiwani wao kwenye Halmashauri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa napata shida hapa
kwa sababu la kwanza, kwamba kwa Majimbo ambayo yana Wabunge wengi wa Viti Maalum, na mfahamu kikao kile kina utaratibu wa gharama zake na mambo mengine. Ingawa gharama siyo hoja kubwa, lakini kwa Jimbo ambalo lina Wabunge wa Viti Maalum nane, 10, sijui hali itakuwaje kwa sababu gharama za uendeshaji wa Halmashauri zitakuwa kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo hili ingelikuwa Wabunge labda ni mmoja au wawili pengine unaweza kuichukulia hili jambo likawezekana, lakini kwa hali ilivyo kuna tatizo kubwa sana na ninadhani ni vema hili jambo likabaki kama ilivyo na ndio utaratibu ulivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa tiketi ya Udiwani, Mbunge anaweza akateuliwa na Mwenyekiti kwa utaratibu ule akawa Mjumbe wa Kamati ya Fedha.(Makofi)