Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lucy Fidelis Owenya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY F. OWENYA aliuliza:- Halmashauri ya Manispaa ya Moshi imekuwa na tatizo la kukatika umeme mara kwa mara. (a) Je, ni sababu zipi zinazosababisha hali hiyo? (b) Je, ni lini tatizo hili litakwisha?

Supplementary Question 1

MHE. LUCY F. OWENYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza.
Namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kunipa majibu yenye matumaini.
Mheshimiwa Spika, tatizo la kukatika kwa umeme limeleta madhara makubwa sana kwa wateja. Watu wamekuwa wakiunguliwa nyumba zao wengine vifaa ndani ya nyumba vikiungua kama friji, television na kadhalika. Tatizo
la hitilafu ya kukatikakatika kwa umeme na kuunguza vifaa vya wateja si tatizo la mteja, ni tatizo la TANESCO. Nataka kujua kutoka kwa Mheshimiwa Waziri ni lini sasa TANESCO itaanza kufidia wananchi kwa kuunguliwa na vitu kwa sababu siyo tatizo lao, kama ilivyo kwenye nchi za Ulaya ambako huwa wanafidia wananchi wakati matatizo yakitokea na kupata hitilafu?
Mheshimiwa Spika, swali la pili. Sasa hivi tunakwenda katika Tanzania ya viwanda, na Mheshimiwa Waziri amesema Kilimanjaro tutakuwa na umeme wa uhakika. Nataka nijue na uwahakikishie wananchi wa Kilimanjaro, je, umeme huu utaweza kutosheleza kwa wafanyakazi na wafanyabiashara wa Mkoa wa Kilimanjaro ambao wanataka kuwekeza katika viwanda? Ahsante sana.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Spika, kwanza niongee tatizo la kukatikakatika umeme.
Waheshimiwa Wabunge njia nyingi za umeme nchini ni zile ambazo TANESCO ilianza nazo mwaka 1964. Hata mimi kwetu Musoma Mjini umeme ulikuja mwaka 1967, hata pale kwetu hazijabadilika. Sasa ni uamuzi wetu, tuamue kuwa na uvumilivu tuzime tutengeneze au tuendelee na matatizo uwe unawaka unakatikakatika. Kwa hiyo, nadhani jibu zuri ni kwamba tuvumilie miundombinu ni ya zamani na tunairekebisha, hilo la kwanza.
Mheshimiwa Spika, kuhusu suala ambalo Mheshimiwa Mbunge amesema TANESCO ina taratibu za kutoa fidia ikiwa kama vyombo vimeharibika na kosa ni la umeme, kosa ambalo ni la TANESCO, wana taratibu zao unapeleka madai unajaza fomu wanafanya tathmini, huo utaratibu upo.
Sasa niongelee hili la kukatikakatika kwa ujumla lingine la umeme wa uhakika. Kilimanjaro kama alivyosema
Mheshimiwa Naibu Waziri ni kwamba inawekwa miundombinu mipya halafu Kilimanjaro na Arusha kuna sub
station tutakwenda kuifungua ya KIA ambayo ni mpya, umeme umeongezeka pale tumeweka substation. Lakini
isitoshe ni kwamba tunaongeza umeme wa msongo mkubwa. Hii Waheshimiwa Wabunge na Watanzania
wanaonisikiliza ni kwamba njia za kusafirishia umeme nchini zilikuwa za KV 220, sasa hivi tunaweka 440, ni karibu mara mbili.
Kwa hiyo, njia ya kutoka Iringa, Dodoma kwenda mpaka Shinyanga tayari, ndiyo maana siku hizi umeme
haukatikikatiki kwa sababu tuna umeme mwingine unasafirishwa humu, na uwezo wake unaweza ukachukua
mpaka MW 5000 kutoka Iringa kwenda Shinyanga. Kwa hiyo, inabidi tujaze mle umeme ni kama ambavyo unajaza maji zaidi kwenye bomba, kwa hiyo, umeme mwingi unakuja.
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa Kaskazini tunajenga transmission line mpaka kutoka Singida kwenda
Namanga ambayo nayo ni ya kilovolts 400; itachukua huo umeme. Juzi nilikuwa naongea na mkandarasi anataka
kujenga transmission line ya kutoka Dar es Salaam kuja Dodoma.
Ndugu zangu wa pembeni mwa Ziwa Tanganyika, tunakamilisha majadiliano ya njia kubwa ya umeme kutoka
Iringa, Sumbawanga, Mpanda, Kigoma na Nyakanazi. Kuna ambayo imeshaanza kujengwa na Balozi anataka akaizindue ya kutoka Makambako kwenda Songea kusudi Songea iwe kwenye Gridi ya Taifa. Kwa hiyo, ndugu zangu Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote hii nchi ya viwanda itajengwa na Wizara ya Nishati na Madini, ndiyo yenye uwezo wa kuijenga msiwe na wasiwasi.