Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. QAMBALO W. QULWI aliluliza:- Wilaya ya karatu ina umri wa zaidi ya mika 20 lakini bado haina Hospitali ya Wilaya jambo ambalo linawatesa wakazi wengi hasa wazee, akinamama na watoto. Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Kituo cha Afya cha Karatu kuwa Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 1

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti nakushukuru kwa kunipa nafasi tena naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala hili la kupandishwa
hadhi kituo hiki limekwisha kujadilikwa katika mamlaka zilizopo pale wilayani na hata mkoani, kwa hiyo kama ni suala la mamlaka iliyobaki kushughulikia jambo hili ni mamlaka iliyoko juu ya hizo mbili. Je, ni lini sasa timu hiyo ya ukaguzi
itatumwa ili upandishwaji hadhi wa kituo hiki uweze kukamilika?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa safari ya kuelekea kupata Hospitali ya Wilaya ya Karatu imeanza, Mheshimiwa Waziri yuko tayari sasa kutenga fedha katika bajeti ya kuanzia mwaka huu na kuendelea ili miundombinu michache iliyobakia iweze kukamilika? Ahsante

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nili-cross check mpaka jana kuangalia taarifa hizi status zikoje, lakini kwa
taarifa nilizozipata kule inaonekana mchakato ulikuwa haujakamilika vizuri. Kwa hiyo, naomba tushauriane tu, tutaangalia jinsi gani tutafanya ili wenzetu wa Halmashauri ili kama lile jambo limekwama halijafika katika mamlaka husika, hasa katika Wizara ya Afya waweze kufanya hivyo ili
Waziri wa Afya aweze kufanya maamuzi, nadhani jambo hilo litakuwa halina shida kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Wizara kuweza
kutenga fedha, ni kweli, na unakumbuka nilikuja pale jimboni kwako na nilitoa maelekezo kadhaa ambapo nilikua sijaridhika na kufika pale nilikuta watu wamefunikwa mablanket ambayo yametolewa store baada ya kusikia Naibu Waziri anakuja pale; kwa hiyo nimegundua changamoto
mbalimbali pale.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mchakato wa ujenzi wa Hospitali ya Wilaya tutaendelea kufanya hivyo. Naomba niwasihi hasa ndugu zetu wa Halmashauri, anzeni mpango huo sasa kuanzia bajeti zenu za Halmashauri ikifika kwetu sisi
Wizarani jambo letu kubwa liwe ni ku-compile vizuri na kufanya taratibu vizuri ili mchakato wa ujenzi wa hospitali ufanyike. Hoja yako ni hoja ya msingi na bahati nzuri eneo lile ni eneo la kitalii lazima tuwekeze vya kutosha tuwe na hospitali yenye maana pale hata mgeni akija aweze kupata
huduma nzuri.

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. QAMBALO W. QULWI aliluliza:- Wilaya ya karatu ina umri wa zaidi ya mika 20 lakini bado haina Hospitali ya Wilaya jambo ambalo linawatesa wakazi wengi hasa wazee, akinamama na watoto. Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Kituo cha Afya cha Karatu kuwa Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 2

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Mwenyekiti nashukuru kunipa nafasi ili na mimi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti tatizo la Karatu linafanana
na tatizo la Korogwe Mjini. Korogwe Mjini haina hospitali, kwa maana ya Halmashauri ya Mji, na Wilaya yetu tumeamua kwa makusudi kabisa kujenga kwanza kituo cha afya ambacho tutakifanya kiwe hospitali.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuweza kutusaidia kutupiga jeki kwa sababu tunajenga kituo cha afya chenye ghorofa tatu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza naomba niweke kumbukumbu sawa ni kwamba nipende kumshukuru Mama Mary Chatanda, Profesa Maji Marefu pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Korogwe kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya ambapo nimetembelea mara kadhaa katika eneo lile. Nilivyofika pale nimekuta initiative mbalimbali wanazozifanya hasa katika suala zima la sekta
ya elimu na sekta aya afya na bahati nzuri wanatumia hospitali ya ndugu yangu Profesa Maji Marefu, iko vijijini lakini obvious kijiografia iko mjini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kwa sababu
mmeanza harakati za ujenzi, na kile kituo cha afya ni kituo cha afya makini inaonekana kuna viongozi makini eneo lile, Serikali itachukua wazo lile jema kuangalia wapi mmeishia, tukishirikiana nanyi kwa pamoja tufanyeje, kwa kuangalia resource tulizo nazo tusukume ili eneo la pale ambalo ni katikati; watu wanaotoka Arusha hata ikipatikana ajali
lazima watakimbizwa pale, tuweze le tuweze kushirikiana kwa pamoja tujenge Hospitali ya Wilaya pale.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. QAMBALO W. QULWI aliluliza:- Wilaya ya karatu ina umri wa zaidi ya mika 20 lakini bado haina Hospitali ya Wilaya jambo ambalo linawatesa wakazi wengi hasa wazee, akinamama na watoto. Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Kituo cha Afya cha Karatu kuwa Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 3

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa
Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, nianze kwanza kwa kuishukuru Serikali kwa kusikiliza kilio cha
watu wa Kilolo kwa ujenzi wa hospitali. Pamoja na hiyo, Mheshimiwa Waziri, itachukua muda mrefu hiyo hospitali kuweza kuisha. Lakini tatizo ambalo lipo ni kwamba Wagonjwa inabidi wapelekwe Kituo cha Afya Kidabaga ambacho hakijakamilika, hakina wodi ya watoto, wodi ya wazazi wala upasuaji, lakini inabidi sasa wasafirishwe waende
kwenye hospitali ambayo iko zaidi ya kilometa 120. Tatizo hakuna gari Mheshimiwa Naibu Waziri kwa hiyo utatusaidiaje ilituweze either kukarabatiwa vizuri kituo cha Kidabaga au tupate gari?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge anafahamu tulifanya ziara pamoja na tukakuta hospitali yao ya Wilaya pale iko taabani. Tukafanya mawazo ya pamoja, na bahati nzuri ndani ya muda mfupi wakapaa shilingi bilioni 1.2. Lakini, kama hiyo haitoshi niwapongeze; kwasababu wameshafanya harakati na ujenzi unaendelea kule site na Mungu akitujaalia ndani ya wiki mbili hizi wakati tuko Bungeni nitakwenda kutembelea ili kuona ni jinsi gani ujenzi unaendelea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Kituo cha Afya cha Kidabaga nadhani unafahamu kwamba Serikali tutaweza kuweka nguvu kubwa pale kwa sababu tukiangalia jiografia yake ni tata sana, tutaangalia namna ya kufanya. Tutapeleka fedha kwa ajili ya kujenga theatre ikiwezekana na wodi ya wazazi. Lengo kubwa wananchi wa eneo lile waweze kupata huduma bora.

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. QAMBALO W. QULWI aliluliza:- Wilaya ya karatu ina umri wa zaidi ya mika 20 lakini bado haina Hospitali ya Wilaya jambo ambalo linawatesa wakazi wengi hasa wazee, akinamama na watoto. Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Kituo cha Afya cha Karatu kuwa Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 4

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Hospitali nyingi za Wilaya zina mkataba kati ya Serikali na mashirika hasa ya dini, Hospitali ya Kilema ikiwa moja wapo. Tunajenga maabara ya kisasa, nini commitment
ya Serikali katika hospitali ya Kilema ili iweze ikatoa huduma zilizo bora katika Taifa hili?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niseme ujenzi wa maabara ni jambo jema sana na sisi Seriali tunaappreciate
hiyo juhudi kubwa inayofanyika na ukiona hivyo
maana yake tunasaidia juhudi za Serikali jinsi gani iweze kusaidia wananchi wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, juu ya commitment ya
Serikali katika hilo naomba tuangalie jinsi gani tutafanya katika suala zima la mikataba hata suala zima la watendaji; kwa sababu wakati mwingine tunaweza tukawa na maabara lakini tukawa na watu ambao hawawezi kuendesha vizuri ile maabara. Kwa hiyo, commitment ya Serikali ni kuangalia jinsi gani tutafanya ili maaabara ikikamilika tuweze ku-deploy watu wazuri pale wa kuweza kufanya analysis ya maabara, wananchi wetu wakienda pale waweze kupata huduma bora hata magonjwa yao yaweze kudundulika vizuri zaidi.

Name

Saumu Heri Sakala

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. QAMBALO W. QULWI aliluliza:- Wilaya ya karatu ina umri wa zaidi ya mika 20 lakini bado haina Hospitali ya Wilaya jambo ambalo linawatesa wakazi wengi hasa wazee, akinamama na watoto. Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Kituo cha Afya cha Karatu kuwa Hospitali ya Wilaya?

Supplementary Question 5

MHE. SAUMU H. SAKALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, nina swali moja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kituo cha afya ambacho
kiko katika kijiji cha Mwera, Kata ya Mwera ni kituo ambacho kwa muda mrefu sana kimepandishwa hadhi ya kuwa kituo cha afya; lakini kituo kile hakina huduma zinazokidhi kuwa
kaama kituo cha afya. Hakina gari la wagonjwa, lakini pia vipimo vya damu salama bado havipo katika hospitali ile.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kujua ni lini
Serikali itakipa hadhi sahihi kituo kile ya kuwa kituo cha afya katika Wilaya ya Pangani?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kusema lini kwanza naomba tuweke rekodi sawa za Mheshimiwa Mbunge kwamba kipindi kile mlinialika na Mheshimiwa Aweso tumefika pale Mwera na nikatoa maagizo kwamba
kituo kile kutokana na yule mwekezaji pale japo anawekeza aweze kujenga theatre.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwashukuru kwa sababu wodi ya wazazi imeedelea kujengwa, lakini hata hivyo Serikali kuufanya kuwe kituo cha afya lazima miundombinu ikamilike vizuri, ndiyo maana tukaona sasa hivi tujenge jengo la theatre pale kubwa lakini pia kujenga na wodi zingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na ndiyo maana
nikamuelekeza Mheshimiwa Aweso kwamba awaambie watu waiandae mapema ile BOQ. Tuta deploy pesa pale, kwa sababu watu wa pale wakikosa huduma, suala la kuvuka Mto Pangani ni changamoto kubwa sana na usiku vivbuko hakuna. Kwa ajili ya kuwaokoa Watanzania
tumeamua kuweka nguvu kubwa za kutosha, fedha za kutosha kujenga jengo lile litakamilika huenda kabla ya mwezi wa saba mwaka huu ujenzi utakuwa umeshaanza.